Majambazi Yateka Magari kadhaa; wakwapua Sadaka toka Kwa Padri - Utimule!

Osaka

JF-Expert Member
Jun 21, 2011
1,762
551
Salaam wana Jamvi!

Jana jioni majira ya saa 11, Ma Padri watatu wa kanisa katoliki walipata wakati mgumu baada kukuta kizuizi barabarani wakati wakirudi toka Sehemu ijulikanayo kama kata ya Kitunda (wilaya ya Sikonge) njia kuu kuelekea Mbeya ukitokea Tabora. Ma Padri hao walikwenda kitunda kwa ajili ya maandalizi ya ujio wa Askofu wa Jimbo kuu la Tabora (Paul Ruzoka). Baada ya kufika Utimule walikuta miti miwili mikubwa ikiwa imekatwa na kuangukia barabarani; muda ule ule majambazi takribani manane yalitokea yakiwa na SMG mbili na kuteka hao watumishi wa Mungu na kuchukua sadaka kiasi zaidi ya Tshs. Million moja na ushehe. Aidha magari mengine madogo mawili yalitekwa pamoja na lori moja na kuporwa mali kadhaa.

Source: askari polisi wa Sikonge.
Nilikuwa nikitokea Rukwa kulekea Mwanza Via Tbr. Nimekutana na polisi hao pale Ipole, njia panda ya kwenda Mbeya na Rukwa ukitokea Tabora. Inasemekana eneo hilo la Utimule liko karibu sana na sehemu yalipotokea maafa ya ' mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe'. Inasikitisha!
 
Hiyo barabara haifai kabisa kwa ujambazi, nimewahi koswakoswa mara mbili....
 
Hiyo barabara haifai kabisa kwa ujambazi, nimewahi koswakoswa mara mbili....

Kweli hiyo barabara ni hatari sana; Nakumbuka miaka ya nyuma kidogo, basi la Sabena lilishawahi koswa koswa kutekwa na majambazi likitokea Mbeya kuelekea Tabora. Sehemu yenyewe ni porini sana hata mtandao wa simu haupatikani.
 
Inasemekana kuwa muda mchache baada ya Watumishi hao wa Mungu kutekwa, lilionekana gari dogo likikaribia eneo la utekaji lakini dereva wa gari lile alishtukia mtego na kurudi nyuma haraka sana. Majambazi yale haraka yalitumia gari la Ma Padri kufukuza gari lile dogo. Majambazi yale hayakuweza kufanikiwa kusudio lao kwani gari la Ma Padri tayari magurudumu ya nyuma yalishapigwa risasi hivyo speed ya gari ilikuwa ndogo kwa kutembelea rim. kuona vile, Watumishi wa Mungu waliona hiyo ndiyo chance nzuri ya kutokomea porini. Ktk harakati za kukimbilia porini, mtu mmoja aliyekuwa safari moja na watumishi hao alikoswa koswa risasi ya kichwa na kutokomea kunako pori! Ktk kukagua gari la watumishi wa Bwana, majambazi hao, walikuta vifaa vya kanisani kama vitambaa vyenye misalaba, vikombe vya divai, Biblia, maji ya baraka, mishumaa nk. Jambazi mmojawapo alishika kichwa baada ya kuona vifaa vile!
 
Jaman dah dunia inaenda wapi?they'l pay 4it!
Mkuu,apo kwenye '...jambazi,akashika kichwa apo,hmmmm...'
 
Salaam wana Jamvi!

Jana jioni majira ya saa 11, Ma Padri watatu wa kanisa katoliki walipata wakati mgumu baada kukuta kizuizi barabarani wakati wakirudi toka Sehemu ijulikanayo kama kata ya Kitunda (wilaya ya Sikonge) njia kuu kuelekea Mbeya ukitokea Tabora. Ma Padri hao walikwenda kitunda kwa ajili ya maandalizi ya ujio wa Askofu wa Jimbo kuu la Tabora (Paul Ruzoka). Baada ya kufika Utimule walikuta miti miwili mikubwa ikiwa imekatwa na kuangukia barabarani; muda ule ule majambazi takribani manane yalitokea yakiwa na SMG mbili na kuteka hao watumishi wa Mungu na kuchukua sadaka kiasi zaidi ya Tshs. Million moja na ushehe. Aidha magari mengine madogo mawili yalitekwa pamoja na lori moja na kuporwa mali kadhaa.

Source: askari polisi wa Sikonge.
Nilikuwa nikitokea Rukwa kulekea Mwanza Via Tbr. Nimekutana na polisi hao pale Ipole, njia panda ya kwenda Mbeya na Rukwa ukitokea Tabora. Inasemekana eneo hilo la Utimule liko karibu sana na sehemu yalipotokea maafa ya ' mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe'. Inasikitisha!

Ilikuwa millioni moja na uaskofu sio na ushehe
 
Inasemekana kuwa muda mchache baada ya Watumishi hao wa Mungu kutekwa, lilionekana gari dogo likikaribia eneo la utekaji lakini dereva wa gari lile alishtukia mtego na kurudi nyuma haraka sana. Majambazi yale haraka yalitumia gari la Ma Padri kufukuza gari lile dogo. Majambazi yale hayakuweza kufanikiwa kusudio lao kwani gari la Ma Padri tayari magurudumu ya nyuma yalishapigwa risasi hivyo speed ya gari ilikuwa ndogo kwa kutembelea rim. kuona vile, Watumishi wa Mungu waliona hiyo ndiyo chance nzuri ya kutokomea porini. Ktk harakati za kukimbilia porini, mtu mmoja aliyekuwa safari moja na watumishi hao alikoswa koswa risasi ya kichwa na kutokomea kunako pori! Ktk kukagua gari la watumishi wa Bwana, majambazi hao, walikuta vifaa vya kanisani kama vitambaa vyenye misalaba, vikombe vya divai, Biblia, maji ya baraka, mishumaa nk. Jambazi mmojawapo alishika kichwa baada ya kuona vifaa vile!

Huu uzi una maswali kdg
Mkuu naomba unijuze nani alie muona huyo jambazi alie shika kichwa mara baada ya kuona (kwenye nyekundu tafadhari)
 
Binadamu wa sasa wamekuwa na roho ngumu sana hawafai hata kufananishwa na kiumbe kingine chochote dunia hii!
 
Huu uzi una maswali kdg
Mkuu naomba unijuze nani alie muona huyo jambazi alie shika kichwa mara baada ya kuona (kwenye nyekundu tafadhari)

Inasemekana Padri mmoja alijificha ktk kichaka karibu na eneo la tukio, so aliweza kuona nini kinaendelea. Mkuu usiwe na shaka kuhusu hili.
 
Polisi wa wilaya ya Sikonge hawakuweza kupata fununu yoyote kuhusu majambazi hayo wakidai hawakupata taarifa mapema. Taarifa imepatikana jana asubuhi. Kutoka Sikonge hadi sehemu ya tukio ni zaidi ya km 100 na barabara husika ni mbaya hakuna mfano! Juhudi za kumpata rafiki yangu Father Makusanya, Baba Paroko wa Sikonge ambaye alikuwa kiongozi wa Ma Padri hao, hazija zaa matunda.
 
Majambazi kutoka nchi jirani hasa Rwanda na Burundi yamekuwa yakitusumbua sana wakazi wa mikoa ya karibu na kwao Hasa mikoa ya Kigoma,Tabora na Kagera kwa muda mrefu sana sijui usalama wa mipakani kwenye nchi yetu ukoje aisee!!
 
Back
Top Bottom