fangfangjt
JF-Expert Member
- Apr 25, 2008
- 571
- 139
Majambazi waua Polisi wawili kituoni
Shija Felician, Kahama
MAJAMBAZI 10 waliokuwa wanashikiliwa katika kituo kidogo cha Polisi cha Kagongwa, wilayani hapa, wamewaua polisi wawili wa kituo hicho kwa risasi na kisha kutoroka.Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa tukio hilo lilitokea juzi wakati majambazi hao walipokuwa kwenye chumba cha mahabusu kituoni hapo.
Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga, Mrakibu Mwandamizi, Justus Kamugisha alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 12:45 usiku baada ya majambazi hao waliokuwa wakituhumiwa kwa makosa
ya mauaji na unyang'anyi wa kutumia silaha, kumwita mmoja wa askari hao ndani ya mahabusu.
Kwa mujibu wa Kamanda Kamugisha, majambazi hao walimwita askari F5344, PC Salumu Mwanakatwe wakisema kuwa wana shida."Alipofungua mlango wa chumba cha mahabusu walimvuta ndani na kumfunika sweta kichwani kisha kumnyang'anya silaha aliyokuwa nayo aina ya SMG namba 14303612 na kuitumia kumuua," alisema.
Kamanda Kamugisha alisema, baada ya kusikia mlio wa bunduki, askari mwingine mwenye namba F 4964, PC Ngwegwe Dira alikwenda kutoa msaada."Kabla hajafika alipigwa risasi kifuani na kufariki dunia hapohapo na majambazi hao walichukua bastola aina ya Chinese yenye namba XR 7526 aliyokuwa nayo askari huyo na kutokomea nayo," alisema.
Baada ya mauaji hayo, majambazi hayo walitoroka na kati yao wawili ambao walikuwa wamefungwa pingu pamoja, waliikata kwa risasi na kukimbia na bastola lakini mmoja alishindwa kukimbia.
"Jambazi huyo (aliyeshindwa kukimbia) aliyekuwa anajulikana kwa jina la Audax Bubel akakamatwa na wananchi na kupigwa shoka kichwani lililomwua hapohapo," alisema na kuongeza: "Majambazi tisa waliobaki, walitoroka na bunduki mbili." Kamanda Kamugisha alisema majambazi hao walikuwa wamekamatwa wakihusishwa na matukio mbalimbali ya mauaji na unyanganyi wa kutumia silaha katika Mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Tabora na walikuwa wamewekwa mahabusu kwa lengo la kufanyiwa utambuzi.
Kamugisha alitoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi ambalo linaendeleza msako wa majambazi hayo.
Shija Felician, Kahama
MAJAMBAZI 10 waliokuwa wanashikiliwa katika kituo kidogo cha Polisi cha Kagongwa, wilayani hapa, wamewaua polisi wawili wa kituo hicho kwa risasi na kisha kutoroka.Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa tukio hilo lilitokea juzi wakati majambazi hao walipokuwa kwenye chumba cha mahabusu kituoni hapo.
Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga, Mrakibu Mwandamizi, Justus Kamugisha alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 12:45 usiku baada ya majambazi hao waliokuwa wakituhumiwa kwa makosa
ya mauaji na unyang'anyi wa kutumia silaha, kumwita mmoja wa askari hao ndani ya mahabusu.
Kwa mujibu wa Kamanda Kamugisha, majambazi hao walimwita askari F5344, PC Salumu Mwanakatwe wakisema kuwa wana shida."Alipofungua mlango wa chumba cha mahabusu walimvuta ndani na kumfunika sweta kichwani kisha kumnyang'anya silaha aliyokuwa nayo aina ya SMG namba 14303612 na kuitumia kumuua," alisema.
Kamanda Kamugisha alisema, baada ya kusikia mlio wa bunduki, askari mwingine mwenye namba F 4964, PC Ngwegwe Dira alikwenda kutoa msaada."Kabla hajafika alipigwa risasi kifuani na kufariki dunia hapohapo na majambazi hao walichukua bastola aina ya Chinese yenye namba XR 7526 aliyokuwa nayo askari huyo na kutokomea nayo," alisema.
Baada ya mauaji hayo, majambazi hayo walitoroka na kati yao wawili ambao walikuwa wamefungwa pingu pamoja, waliikata kwa risasi na kukimbia na bastola lakini mmoja alishindwa kukimbia.
"Jambazi huyo (aliyeshindwa kukimbia) aliyekuwa anajulikana kwa jina la Audax Bubel akakamatwa na wananchi na kupigwa shoka kichwani lililomwua hapohapo," alisema na kuongeza: "Majambazi tisa waliobaki, walitoroka na bunduki mbili." Kamanda Kamugisha alisema majambazi hao walikuwa wamekamatwa wakihusishwa na matukio mbalimbali ya mauaji na unyanganyi wa kutumia silaha katika Mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Tabora na walikuwa wamewekwa mahabusu kwa lengo la kufanyiwa utambuzi.
Kamugisha alitoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi ambalo linaendeleza msako wa majambazi hayo.