Majaliwa hana mamlaka Zanzibar

Majaliwa hana mamlaka Zanzibar

GHIBUU

JF-Expert Member
Joined
Jan 13, 2011
Posts
4,432
Reaction score
3,016
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa hana mamlaka ya kuingilia na kutoa maagizo kwa mambo ya #Zanzibar yasiyo mambo ya Muungano. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 na Katiba ya Zanzibar ya 1984 imeainisha waziwazi mamlaka ya Serikali mbili zilizopo." @MazruiNasso
Adjustments.JPG


====
Zanzibar. Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara na Viwanda, Juma Hassan Reli ahakikishe anazuia utoaji wa vibali vya kuingiza sukari kutoka nje hadi sukari inayozalishwa na kiwanda cha sukari cha Zanzibar kilichopo Mahonda iishe.

Amesema haiwezekani kiwanda hicho cha pekee kinachozalisha tani 6,000 za sukari kwa mwaka kikakosa wateja wakati mahitaji ya sukari Zanzibar ni tani 36,000 kwa mwaka.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo Jumamosi, Januari 18, 2020 wakati alipotembelea kiwanda cha kuzalisha sukari cha Zanzibar kilichopo katika eneo la Mahonda wilaya ya Kaskazini ‘A’ mkoa wa Kaskazini Unguja.

Amesema ni vizuri wizara ikahakikisha sukari inayozalishwa na kiwanda hicho inapewa kipaumbele cha kwanza kwa kununuliwa kwa sababu wana uhakika na ubora wake kwa kuwa wameshuhudia uzalishaji wake kuanzia hatua ya awali miwa ikiwa shambani.

“Wizara ya viwanda lazima mbadilike na muweke utaratibu mzuri wa kusimamia uingizwaji wa sukari kutoka nje. Haiwezekani sukari inayozalishwa ndani ikakosa soko kutokana na uingizwaji wa sukari kutoka nje. Hatuwezi kumfurahisha mtu mmoja huku wengi wakiumia.”

Mwananchi
 
Kwahiyo!!!!!

Atulie kimya, Zanzibar uchumi wake ni kodi import na export tulitegemea sukari kuuza tanganyika mkaizuiya sukari huko huko, Maajaaliwa ataka awalaximishe wazanzibari wanunue , impossible

Hana mamlaka kuingilia mambo yasio kuwa ya muungano hata rais wa muungano vile vile kwa mujibu wa katiba .
 
Zanzibar. Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara na Viwanda, Juma Hassan Reli ahakikishe anazuia utoaji wa vibali vya kuingiza sukari kutoka nje hadi sukari inayozalishwa na kiwanda cha sukari cha Zanzibar kilichopo Mahonda iishe.

Amesema haiwezekani kiwanda hicho cha pekee kinachozalisha tani 6,000 za sukari kwa mwaka kikakosa wateja wakati mahitaji ya sukari Zanzibar ni tani 36,000 kwa mwaka.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo Jumamosi, Januari 18, 2020 wakati alipotembelea kiwanda cha kuzalisha sukari cha Zanzibar kilichopo katika eneo la Mahonda wilaya ya Kaskazini ‘A’ mkoa wa Kaskazini Unguja.

Amesema ni vizuri wizara ikahakikisha sukari inayozalishwa na kiwanda hicho inapewa kipaumbele cha kwanza kwa kununuliwa kwa sababu wana uhakika na ubora wake kwa kuwa wameshuhudia uzalishaji wake kuanzia hatua ya awali miwa ikiwa shambani.

“Wizara ya viwanda lazima mbadilike na muweke utaratibu mzuri wa kusimamia uingizwaji wa sukari kutoka nje. Haiwezekani sukari inayozalishwa ndani ikakosa soko kutokana na uingizwaji wa sukari kutoka nje. Hatuwezi kumfurahisha mtu mmoja huku wengi wakiumia.”

Mwananchi
 
Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Sijui ni mamlaka yapi zaidi kama cheo chake ndiyo hicho.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hilo jina huwa nalishangaa sana wakati yeye ni escott 4 na Rais wa SMZ ni escott 3..Kiuhalisia vyeo vya serikali kuu vimekaa shaghala baghala tu ilimradi liende. Sasa escott 3 hana mamlaka na Tanganyika wakati escott 4 ana mamlaka na Zanzibar. Pia kwenye cabinet makamu wa Rais na Rais wa SMZ wanakaa next to president wakati waziri mkuu anakaa next to VP.
 
Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Sijui ni mamlaka yapi zaidi kama cheo chake ndiyo hicho.

Sent using Jamii Forums mobile app
Jibu liko kwenye jina lake chief...kuna sehemu za jamuhuri yetu hajawahi kuikanyaga au kutoa maagizo yanayohusu sehemu husika..haina maana kwamba sio waziri mkuu wao. Pia KAZI namba moja ya PM ni kuongoza shughuli za serikali Bungeni pale Dodoma..akitembelea maeneo ni Kwa ajili ya kufanya mipango na kujionea Kwa macho..Area commissioners siku hizi wako Chini ya Rais mwenyewe, before immediate boss wao alikua PM.
 
Japo napita lakini natoa ushauri tu! Zanzibar ni sehemi ya Tanzania na uchumi was Zanzibar ukidolola kutokana na kuiujumu Zanzibar na watu wake ni mzigo kwa Tanzania kwa ujumla! Kama wizara ya viwanda na biashara ya Tanzania inalo jambo la kufanya kunusuru viwanda vya Zanzibar dhidi ya wahujumu uchumi
 
Hilo jina huwa nalishangaa sana wakati yeye ni escott 4 na Rais wa SMZ ni escott 3..Kiuhalisia vyeo vya serikali kuu vimekaa shaghala baghala tu ilimradi liende. Sasa escott 3 hana mamlaka na Tanganyika wakati escott 4 ana mamlaka na Zanzibar. Pia kwenye cabinet makamu wa Rais na Rais wa SMZ wanakaa next to president wakati waziri mkuu anakaa next to VP.
Harmonization chief... sometimes kuna vitu inabidi vionekane/vibaki kama vilivyo kama havina athari katika jamii Kwa mfano Mkuu wa wilaya na Mkurugenzi katika wilaya..mmoja anatembea na bendera ya Taifa mwingine kashikilia Economic power ya wilaya nzima Hadi mafuta ya kutembeza GX ya DC anatoa yeye.
 
Majaliwa ni Waziri Mkuu wa JMT, Zanzibar ni sehemu ya JMT, hivyo ana mamlaka yote kuhusu Zanzibar kwa jambo lolote hata la Zanzibar as far as JMT itahusika.

Biashara sio jambo la muungano, lakini biashara ya sukari ya Zanzibar imekuwa na siasa ambazo serikali ya JMT inahusika direct, hivyo Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa yulo very right kuingilia kati.

Zanzibar inakiwanda cha sukari kinazalisha sukari ya kutosheleza soko la Zanzibar, huku wafanyabiashara ya uagizaji sukari, wakiagiza sukari kutoka nje at cheaper prices kuliko hiyo sukari ya Zanzibar na matokeo yake ni sukari ya Zanzibar imedodea kiwandani wakataka kuiingiza bara, tukawagomea!.
P
 
Atulie kimya, Zanzibar uchumi wake ni kodi import na export tulitegemea sukari kuuza tanganyika mkaizuiya sukari huko huko, Maajaaliwa ataka awalaximishe wazanzibari wanunue , impossible

Hana mamlaka kuingilia mambo yasio kuwa ya muungano hata rais wa muungano vile vile kwa mujibu wa katiba .
Tutabomoa hivyo visiwa mkose pakukaa ohooo!
 
Back
Top Bottom