josephdeo
Member
- Nov 23, 2015
- 96
- 208
Makaburi yamezika ndoto nyingi, ndio! wala sina uwezo kulikataa hilo ila tu ninalo la kuongezea kwenye hilo. Kama ilivyo kwa makaburi pia mapenzi nayo yamechangia sehemu nyingine kubwa ya kuzika ndoto za watu wengi. Nasema haya nikiwa muhanga na si mhamasishaji.
Naweza kusema maisha ni fumbo gumu kulitatua, haswa ujuzi wa Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema udhihirika pale ambapo alitunyima fursa wanadamu kutokuijua kesho yetu. Kwa sehemu kubwa maisha yetu yamekuwa jana na sasa huku kesho na baadae vikiendelea kuwa fumbo ambalo kupatikana jibu lake itachukua kumalizika kwa ulimwengu.
Nakiri wazi pasina uficho kuwa niliteleza na kukosea ila dunia ilinichagulia njia ngumu mno kwa upande wangu kupita mara baada ya kutoka kwenye njia ya awali. Njia ambayo ilinikumbusha na kunifunza kuwa ikiwa malezi ya wazazi hayakuingia vyema akilini basi ulimwengu ungekupa malezi ya kikatili mno. Wahusika wakuu wa malezi hayo wakiwa ni walimwengu wenyewe ambao wasingeweza kukukosoa kwa makosa yako bali kukuadhibu. Hata wasikupe nafasi ya kujutia ili ujisahihishe bali wangeongeza kidonda juu ya kovu.
Mengi nimeyapia achilia mbali kuyaona na laiti kama ningejua kuwa ningekwenda kukabiliana nayo basi ningechagua chaguzi lingine tofauti na hilo. Nashukuru nipo hapa sasa hata baada ya kuzipita nyakati hizi zilizoacha kumbukumbu isiyofutika kamwe.
Mauti pekee ndio yatafanyika kuwa tamati wa hiki ambacho upita akilini mwangu. Sasa zinapita kama kumbukumbu mbaya maishani ila nilithibitisha kuwa mpaka binadamu kufariki basi anakuwa kakiepuka kifo mara kadhaa kabla. Hili nalikubali kwani hata wakati mwingine siamini kama niko hai, eti nami bado niko kwenye ulimwengu huu!. Nikisema ya kuwa wakati mwingine siamini kama bado niko hai basi fahamu kuwa sitanii kwani ni zaidi ya mara moja nimekiepuka kifo.
Ninacho kisema hapa ni ile hali ya kukiona kifo mahili kadhaa toka ulipo simama kisha kinakupita na kwenda zake. Nawe unaweza kujitiza ili kuhakikisha hilo ni mara ngapi umepitia nyakati kama hizo za kuhisi ulipenya na kukikwepa kifo. Basi tuachane na hayo kwani si tija kwenye simulizi yetu badala yake nilitaka kukuonyesha tu.
Hata kwa theluthi ya punje ya mchele sikuwahi kuwaza ya kuwa ipo siku eti nami nitakuja kuwa mvuvi. Sikuwahi kwa kuwa nyumbani hakuna ambaye amewahi kujihusisha na shughuli hii. Zaidi ya hapo labda kula samaki wabichi ambao sikujua hata wanapatikanaje. Kwa wakati huu ungeniambia kuwa baada ya miaka kadhaa mbele nami nitakuwa kati ya wazalishaji wa bidhaa hii ya samaki basi ningekukatilia katu.
Kamwe nisingekubaliana na wewe! Ubishani mkali ungezuka baina yetu. Ndoto yangu ilikuwa nije kuwa askari mpelekezi na ndicho kilichokuwa akilini mwangu pekee, si uvuvi!. Ila maisha haya yaache yaitwe maisha kwa sababu kuna wakati inatubidi kukubali kuishi kati ya kile unachokihitaji na uhalisia wa maisha yako. Japo sikuwa kati ya wanafunzi bora katika darasa letu ila nilikuwa kati ya wanafunzi walioyahimili vyema masomo.
Si tu shuleni bali mpaka nyumba nilikuwa nikiweza kumheshimisha mzee wangu na kumfanya kutamba mtaani kwa matokeo ya mitihani yangu. Familia iliweka matumaini yao mengi kwangu kwa minajili ya kuja kuwakomboa na janga la umasikini hapo baadae. Labda waliweka matarajio makubwa kuliko uhalisia wenyewe na ndio ikawa sababu ya kunichukia pale ambapo niliteleza na kuanguka.
Ila ilikuwa ni haki kwao kwani sikuwaangusha kwenye mtihani wa kumaliza darasa la saba nilipata wastani wa 210 kati ya 250 uliokuwepo. Sikuishia hapo bali hata masomo ya shule ya upili nayo niliyahimili vyema. Ila safari yangu ilifanana na moto wa mabua ambao uliwaka kwa kasi mno mwanzoni ila ulishindwa kuhimili kasi yake baada ya mda mfupi baadae. Nasema hivyo kwa kuwa nilikuja kukengeuka.
Hilo lilijitokeza mara baada ya kupata balehe na sauti yangu kuwa ya kiume tofauti na ya kivulana niliyokuwa nayo. Kwa mbali mazalia ya ndevu yakaanza kukipamba kidevu changu huku kifua nacho hakikukubali kuachwa nyuma nacho kilianza kustawisha nywere ndongo ndongo. Shida yote ilianza mara baada ya haya kutokea kweli adhabu zetu huanza mara baada ya kupata vile tulivyovitamani. Ndio nami adhabu yangu ilipoanzia hapo mara baada ya kupata balehe niliyokuwa nikihitamani.
Macho yangu kwa wakati huu yalipomtizama binti hayakuwa yale ya kirafiki tena bali matamanio ya kujua kile alichokistiri ndani kilifananaje. Sijatokwa na kumbukumbu za maisha ya shule bado kwani mtihani wa kidato cha pili niliofanya mwaka 2012 nilikuwa mwanafunzi pekee kutoka mtaa wetu niliyefaulu kwenda kidato cha tatu. Wengine wanne ambao tulisoma kidato kimoja ila shule zikiwa tofauti hawakufanikiwa kwenda mbele na wawili kati yao waliacha shule.
Kwanini mzee wangu alitembee kifua mbele?, Sababu za kufanya vile zilikuwa wazi kabisa. Alisomesha kati ya watoto wenye akili ambao mtaa wetu ulibarikiwa kuwa nao. Lakini sikuendelea kumuheshimisha mzee wangu kama alivyokuwa akitaka na hii ilikuwa ni baada ya kuwafahamu wasichana. Taratibu kama mwendo wa kinyonga mambo yalianza kuharibika. Bahati iliyokuwa mbaya kabisa ni kuwa yalihariba kwa taratibu pasina kutoa onyo wala ishara yoyote ile kwangu.
Ndio maana siku zote huwasisitizia watu kuwa unapoambiwa na wengine kuhusu mabadiliko ya kitu fulani kwako wasikilize na jitathimini. Kwa sababu ni ngumu kwako wewe kuweza kung'amua mabadiliko yanayotokea kwako. Ikiwa utapata nafasi ya kuyatambua basi nafasi ya kuyarekebesha inakuwa haipo tena. Kwangu mabadiliko yalianza katika ratiba yangu ya kwenda shule, nilikwenda shule kwa mda niliotaka.
Hata nilipofika shuleni pia sikuwa najishughulisha na lengo mama la mwanafunzi shuleni, kujifunza!. Badala yake nilitumia wakati mwingi kutafuta na kumchambua ni binti gani ambaye angenasa haraka kwenye mtego wangu. Maisha yakaenda hivyo na kwa kuwa sikuwa na yeyote aliyeyatambua kwa mapema mabadiliko yale, wazazi waliwiwa na uzito wa majukumu ya familia. Maendeleo yangu shuleni yakaanza kudorola taratibu na sikupata nafasi ya kung'amua.
Naweza kusema maisha ni fumbo gumu kulitatua, haswa ujuzi wa Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema udhihirika pale ambapo alitunyima fursa wanadamu kutokuijua kesho yetu. Kwa sehemu kubwa maisha yetu yamekuwa jana na sasa huku kesho na baadae vikiendelea kuwa fumbo ambalo kupatikana jibu lake itachukua kumalizika kwa ulimwengu.
Nakiri wazi pasina uficho kuwa niliteleza na kukosea ila dunia ilinichagulia njia ngumu mno kwa upande wangu kupita mara baada ya kutoka kwenye njia ya awali. Njia ambayo ilinikumbusha na kunifunza kuwa ikiwa malezi ya wazazi hayakuingia vyema akilini basi ulimwengu ungekupa malezi ya kikatili mno. Wahusika wakuu wa malezi hayo wakiwa ni walimwengu wenyewe ambao wasingeweza kukukosoa kwa makosa yako bali kukuadhibu. Hata wasikupe nafasi ya kujutia ili ujisahihishe bali wangeongeza kidonda juu ya kovu.
Mengi nimeyapia achilia mbali kuyaona na laiti kama ningejua kuwa ningekwenda kukabiliana nayo basi ningechagua chaguzi lingine tofauti na hilo. Nashukuru nipo hapa sasa hata baada ya kuzipita nyakati hizi zilizoacha kumbukumbu isiyofutika kamwe.
Mauti pekee ndio yatafanyika kuwa tamati wa hiki ambacho upita akilini mwangu. Sasa zinapita kama kumbukumbu mbaya maishani ila nilithibitisha kuwa mpaka binadamu kufariki basi anakuwa kakiepuka kifo mara kadhaa kabla. Hili nalikubali kwani hata wakati mwingine siamini kama niko hai, eti nami bado niko kwenye ulimwengu huu!. Nikisema ya kuwa wakati mwingine siamini kama bado niko hai basi fahamu kuwa sitanii kwani ni zaidi ya mara moja nimekiepuka kifo.
Ninacho kisema hapa ni ile hali ya kukiona kifo mahili kadhaa toka ulipo simama kisha kinakupita na kwenda zake. Nawe unaweza kujitiza ili kuhakikisha hilo ni mara ngapi umepitia nyakati kama hizo za kuhisi ulipenya na kukikwepa kifo. Basi tuachane na hayo kwani si tija kwenye simulizi yetu badala yake nilitaka kukuonyesha tu.
Hata kwa theluthi ya punje ya mchele sikuwahi kuwaza ya kuwa ipo siku eti nami nitakuja kuwa mvuvi. Sikuwahi kwa kuwa nyumbani hakuna ambaye amewahi kujihusisha na shughuli hii. Zaidi ya hapo labda kula samaki wabichi ambao sikujua hata wanapatikanaje. Kwa wakati huu ungeniambia kuwa baada ya miaka kadhaa mbele nami nitakuwa kati ya wazalishaji wa bidhaa hii ya samaki basi ningekukatilia katu.
Kamwe nisingekubaliana na wewe! Ubishani mkali ungezuka baina yetu. Ndoto yangu ilikuwa nije kuwa askari mpelekezi na ndicho kilichokuwa akilini mwangu pekee, si uvuvi!. Ila maisha haya yaache yaitwe maisha kwa sababu kuna wakati inatubidi kukubali kuishi kati ya kile unachokihitaji na uhalisia wa maisha yako. Japo sikuwa kati ya wanafunzi bora katika darasa letu ila nilikuwa kati ya wanafunzi walioyahimili vyema masomo.
Si tu shuleni bali mpaka nyumba nilikuwa nikiweza kumheshimisha mzee wangu na kumfanya kutamba mtaani kwa matokeo ya mitihani yangu. Familia iliweka matumaini yao mengi kwangu kwa minajili ya kuja kuwakomboa na janga la umasikini hapo baadae. Labda waliweka matarajio makubwa kuliko uhalisia wenyewe na ndio ikawa sababu ya kunichukia pale ambapo niliteleza na kuanguka.
Ila ilikuwa ni haki kwao kwani sikuwaangusha kwenye mtihani wa kumaliza darasa la saba nilipata wastani wa 210 kati ya 250 uliokuwepo. Sikuishia hapo bali hata masomo ya shule ya upili nayo niliyahimili vyema. Ila safari yangu ilifanana na moto wa mabua ambao uliwaka kwa kasi mno mwanzoni ila ulishindwa kuhimili kasi yake baada ya mda mfupi baadae. Nasema hivyo kwa kuwa nilikuja kukengeuka.
Hilo lilijitokeza mara baada ya kupata balehe na sauti yangu kuwa ya kiume tofauti na ya kivulana niliyokuwa nayo. Kwa mbali mazalia ya ndevu yakaanza kukipamba kidevu changu huku kifua nacho hakikukubali kuachwa nyuma nacho kilianza kustawisha nywere ndongo ndongo. Shida yote ilianza mara baada ya haya kutokea kweli adhabu zetu huanza mara baada ya kupata vile tulivyovitamani. Ndio nami adhabu yangu ilipoanzia hapo mara baada ya kupata balehe niliyokuwa nikihitamani.
Macho yangu kwa wakati huu yalipomtizama binti hayakuwa yale ya kirafiki tena bali matamanio ya kujua kile alichokistiri ndani kilifananaje. Sijatokwa na kumbukumbu za maisha ya shule bado kwani mtihani wa kidato cha pili niliofanya mwaka 2012 nilikuwa mwanafunzi pekee kutoka mtaa wetu niliyefaulu kwenda kidato cha tatu. Wengine wanne ambao tulisoma kidato kimoja ila shule zikiwa tofauti hawakufanikiwa kwenda mbele na wawili kati yao waliacha shule.
Kwanini mzee wangu alitembee kifua mbele?, Sababu za kufanya vile zilikuwa wazi kabisa. Alisomesha kati ya watoto wenye akili ambao mtaa wetu ulibarikiwa kuwa nao. Lakini sikuendelea kumuheshimisha mzee wangu kama alivyokuwa akitaka na hii ilikuwa ni baada ya kuwafahamu wasichana. Taratibu kama mwendo wa kinyonga mambo yalianza kuharibika. Bahati iliyokuwa mbaya kabisa ni kuwa yalihariba kwa taratibu pasina kutoa onyo wala ishara yoyote ile kwangu.
Ndio maana siku zote huwasisitizia watu kuwa unapoambiwa na wengine kuhusu mabadiliko ya kitu fulani kwako wasikilize na jitathimini. Kwa sababu ni ngumu kwako wewe kuweza kung'amua mabadiliko yanayotokea kwako. Ikiwa utapata nafasi ya kuyatambua basi nafasi ya kuyarekebesha inakuwa haipo tena. Kwangu mabadiliko yalianza katika ratiba yangu ya kwenda shule, nilikwenda shule kwa mda niliotaka.
Hata nilipofika shuleni pia sikuwa najishughulisha na lengo mama la mwanafunzi shuleni, kujifunza!. Badala yake nilitumia wakati mwingi kutafuta na kumchambua ni binti gani ambaye angenasa haraka kwenye mtego wangu. Maisha yakaenda hivyo na kwa kuwa sikuwa na yeyote aliyeyatambua kwa mapema mabadiliko yale, wazazi waliwiwa na uzito wa majukumu ya familia. Maendeleo yangu shuleni yakaanza kudorola taratibu na sikupata nafasi ya kung'amua.