Maisha ya Pwani ni shida

moyafricatz

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2015
Posts
2,905
Reaction score
4,940
Jamaa kagombana na mkewe, akasusa kula koni kurudi kazini kamkuta mkewe amevaa kanga imeandikwa UKISUSA WENZIO WALA

Ilipofika asubuhi mke akavaa kanga imeandikwa UKITOKA MWENZIO ANAINGIA

Jamaa akagoma kwenda kazini, mke akabadili kanga na kuvaa iloandikwa NIMEMDHIBITI NDO MANA HATOKI

Jamaa akaenda kuomba ushauri kwa rafiki yake akaambiwa twende nyumbani kwako, walipofika walimkuta mke kavaa kanga imeandikwa ULIDHANI RAFIKI YAKO KUMBE ADUI YAKO

Jamaa akaamua kusafiri siku tano ili kupunguza hasira. Aliporudi akamkuta mke amevaa kanga imeandikwa NI BORA NIMPE JIRANI KULIKO KIOZEE NDANI

Jamaa yuko ICU!

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2]
 
😂 Najivunia kuwa Mtanzania, najivunia Lugha yangu Adhimu Kiswahili.
 
huyo afe huko huko wenzake wajilie kiroho swafi
 
wow
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…