Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 58,636
- 220,349
Middle class watamudu total lockdown. Wale wenye uwezo wa kuwa na:
Kilo 10 mchele
“. “. Unga wa mahindi
“. “ unga wa ngano
“. 5. Sukari
Galoni la mafuta ya kupikia
Hii ni 15%ya Watanzania wanamudu maisha haya, wengi wao ni wenye ajira na biashara za za kuzungusha milioni kuendelea.
Kuna vijana wanaishi kwenye chumba. Hawa wametoka vijijini kujaribu maisha mjini. Huwa wana ishi 5-6 katika chumba kimoja. Wana handset moja kila mtu ana SIM card yake. Anaetaka kutumia simu anaingiza sim card.
Hawa wanaratiba ya kununua chakula. Kila mtu na wiki yake. Asubuhi inabidi waamke wakasake vibarua. Ile wiki ya kununua chakula huwezikuweka kitu. Inabidi ununue unga, mboga, mkaa, na mazagazaha kama yote. Upike chakula ule na wenzako.
Usipokuwa kwenye zamu ya chakula ndiyo unaweka pesa. Lengo ni kupata mtaji wa kusimama. Ukishasimama unaondoka mwingine anapigiwa simu kijijini aje mjini.
Hawa utawakuta sehemu kama Mahakama ya ndizi, wanashusha mizigo ya mazao na kupakia mizigo iliyonunuliwa kwenye magari ya wateja.
Kuna wajane, walikopa mikopo kwenye vikoba sasa wanapika mama ntilie, maandazi na chapati. Kila wiki kuna hela ya kurudisha kwenye vikoba, kodi ya nyumba na chakula cha watoto.
Kuna Wauza baa nao wanatakiwa kulipa kodi.
Kilo 10 mchele
“. “. Unga wa mahindi
“. “ unga wa ngano
“. 5. Sukari
Galoni la mafuta ya kupikia
Hii ni 15%ya Watanzania wanamudu maisha haya, wengi wao ni wenye ajira na biashara za za kuzungusha milioni kuendelea.
Kuna vijana wanaishi kwenye chumba. Hawa wametoka vijijini kujaribu maisha mjini. Huwa wana ishi 5-6 katika chumba kimoja. Wana handset moja kila mtu ana SIM card yake. Anaetaka kutumia simu anaingiza sim card.
Hawa wanaratiba ya kununua chakula. Kila mtu na wiki yake. Asubuhi inabidi waamke wakasake vibarua. Ile wiki ya kununua chakula huwezikuweka kitu. Inabidi ununue unga, mboga, mkaa, na mazagazaha kama yote. Upike chakula ule na wenzako.
Usipokuwa kwenye zamu ya chakula ndiyo unaweka pesa. Lengo ni kupata mtaji wa kusimama. Ukishasimama unaondoka mwingine anapigiwa simu kijijini aje mjini.
Hawa utawakuta sehemu kama Mahakama ya ndizi, wanashusha mizigo ya mazao na kupakia mizigo iliyonunuliwa kwenye magari ya wateja.
Kuna wajane, walikopa mikopo kwenye vikoba sasa wanapika mama ntilie, maandazi na chapati. Kila wiki kuna hela ya kurudisha kwenye vikoba, kodi ya nyumba na chakula cha watoto.
Kuna Wauza baa nao wanatakiwa kulipa kodi.
