KENZY
JF-Expert Member
- Dec 27, 2015
- 35,744
- 86,370
Dhana ya Uongo imekuwa ni maisha yetu ya kila siku japo si jambo linalojadiliwa kwa upana sana ila athari zake zipo kila sekunde!.
Katika jamii nyingi uongo si jambo linalopendwa na vyombo vya sheria humtia hatiani mtu yoyote atakaebainika kusema uongo!, Hata hivyo ukiuzungumzia uongo basi upo karibu kuuzungumzia "UKWELI" hizi dhana mbili ni kama sarafu yani kichwa na mwenge.
Sifa moja wapo ya ukweli ni huwa unathibitika na ukishindwa kuuthibitisha ukweli maana yake ukweli huo ni uongo!, ila kuna baadhi ya vitu ni kama sheria za ulimwengu zinatuwia ugumu kwenye kuthibitisha.
Kwa maisha yetu haya yaliyogubikwa na kila aina ya shughuli za kisiasa,uchumi, mapenzi, sayansi na sanaa ni ngumu sana kuuepuka "UONGO!".
Kwani kwa hulka zetu mtu hudanganya kwasababu anazozifahamu yeye na kwa manufaa yake, kwa wengine uongo ni sanaa na kwa wengine uongo ni sayansi, kwa lugha ya picha naweza kusema uongo ni kama shuka linalofunika ukweli.
Kwanini watu tunadanganya..?
watu tunadanganya kwasababu ya hisia na vilevile kimantiki.
Kihisia huwa tunaficha jambo fulani ili lisijulikane maana tunajua tukisema ukweli tunaweza kuchukuliwa hatua, kimantiki imekaa sana kifaida hii inaingia sana kwenye maswala ya uchumi napia mtu hudanganywa kutokana na vile anapenda kusikia nini!.
Binafsi kwenye hili ndio naona ni kama hesabu kwani unamdanganya mtu kutokana na vile anahitaji nini kusikia hata kama haina faida kwako!.
Tunadanganya pia kwasababu uongo muda mwengine hununua muda, huponya navilevile huweza kuwafanya watu watizame kitu katika namna yatofauti ama vile anavyohitaji mdanganyaji!.
sio kwamba naupamba uongo ni vile uongo unaweza kuwa namanufaa fulani fulani ukiwa upande wa unufaikaji!.
yapo pia madhara ya uongo ila hutegemea na jambo gani kwani uongo pia huweza kupelekea hata kifo!.
Uongo hutumika kwenye uongozi kama dhana yakuwatuliza watu kwani muda mwengine watu kuambiwa ukweli huweza kuleta mtafaruku ambao huvunja amani yote!. kwajinsi nikilitazama hili swala la uongo sisiti kusema uongo ni sehemu ya maisha ya binadamu kwani watu huweza hata kuongopa kwa kutumia matendo!.
Uongo katika ujasusi ni kama siraha hili sote twafahamu majasusi hutumia dhana hii aidha kujilinda au kuangamiza ama kuhitaji jambo fulani.
Uongo kama uponyaji ama tulizo, zipo baadhi ya taarifa kuwapatia watu wenye matatizo ya afya huwaletea shida sana hivyo dhana hii hutumika pia ili kuweza kuwatuliza ili yasiwafike yakuwafika hapa tunasema kutumia hekima ya kibinadamu!.
Kwa uchache naweza kusema dhana hii ni pana sana hivyo sitaweza kugusia katika kona zote ila iwe ni kwa siri ama sio kwa siri inahitajika uwe na uelewa mpana katika kuimudu dhana ya uongo yani ipo hivi.
Kwa mdanganyaji hii ni siraha inayohitaji uwe na akili sana yakuitumia pia kwa mdanganywaji huu ni mtego usipoweza kuutegua utakuangamiza!.
Nina swali kwako msomaji je, unafikiri ipo haja yakuanzisha sheria yakumlinda mtu aliesema uongo ambao umeweza kumsaidia mtu mwengine...?
Vilevile nina hoja na swali ndani ya hoja!.
Katika vitabu vya dini yani biblia na Quran vinautaja uongo kama dhambi na kitu kisichofaa ambacho kinaweza kumpeleka mtu motoni!, sasa je, vipi ikiwa uongo huo unamsaidia mtu kiafya (kumuepusha asife n.k) ni vyema kumuongopea au ni bora kumuambia ukweli pasipokujali kitakachomkuta ikiwa unafahamu ukimuambia ukweli nini kinaweza kumkuta, je kwenye hili tunaacha dini iongee au hekima..?
Katika jamii nyingi uongo si jambo linalopendwa na vyombo vya sheria humtia hatiani mtu yoyote atakaebainika kusema uongo!, Hata hivyo ukiuzungumzia uongo basi upo karibu kuuzungumzia "UKWELI" hizi dhana mbili ni kama sarafu yani kichwa na mwenge.
Sifa moja wapo ya ukweli ni huwa unathibitika na ukishindwa kuuthibitisha ukweli maana yake ukweli huo ni uongo!, ila kuna baadhi ya vitu ni kama sheria za ulimwengu zinatuwia ugumu kwenye kuthibitisha.
Kwa maisha yetu haya yaliyogubikwa na kila aina ya shughuli za kisiasa,uchumi, mapenzi, sayansi na sanaa ni ngumu sana kuuepuka "UONGO!".
Kwani kwa hulka zetu mtu hudanganya kwasababu anazozifahamu yeye na kwa manufaa yake, kwa wengine uongo ni sanaa na kwa wengine uongo ni sayansi, kwa lugha ya picha naweza kusema uongo ni kama shuka linalofunika ukweli.
Kwanini watu tunadanganya..?
watu tunadanganya kwasababu ya hisia na vilevile kimantiki.
Kihisia huwa tunaficha jambo fulani ili lisijulikane maana tunajua tukisema ukweli tunaweza kuchukuliwa hatua, kimantiki imekaa sana kifaida hii inaingia sana kwenye maswala ya uchumi napia mtu hudanganywa kutokana na vile anapenda kusikia nini!.
Binafsi kwenye hili ndio naona ni kama hesabu kwani unamdanganya mtu kutokana na vile anahitaji nini kusikia hata kama haina faida kwako!.
Tunadanganya pia kwasababu uongo muda mwengine hununua muda, huponya navilevile huweza kuwafanya watu watizame kitu katika namna yatofauti ama vile anavyohitaji mdanganyaji!.
sio kwamba naupamba uongo ni vile uongo unaweza kuwa namanufaa fulani fulani ukiwa upande wa unufaikaji!.
yapo pia madhara ya uongo ila hutegemea na jambo gani kwani uongo pia huweza kupelekea hata kifo!.
Uongo hutumika kwenye uongozi kama dhana yakuwatuliza watu kwani muda mwengine watu kuambiwa ukweli huweza kuleta mtafaruku ambao huvunja amani yote!. kwajinsi nikilitazama hili swala la uongo sisiti kusema uongo ni sehemu ya maisha ya binadamu kwani watu huweza hata kuongopa kwa kutumia matendo!.
Uongo katika ujasusi ni kama siraha hili sote twafahamu majasusi hutumia dhana hii aidha kujilinda au kuangamiza ama kuhitaji jambo fulani.
Uongo kama uponyaji ama tulizo, zipo baadhi ya taarifa kuwapatia watu wenye matatizo ya afya huwaletea shida sana hivyo dhana hii hutumika pia ili kuweza kuwatuliza ili yasiwafike yakuwafika hapa tunasema kutumia hekima ya kibinadamu!.
Kwa uchache naweza kusema dhana hii ni pana sana hivyo sitaweza kugusia katika kona zote ila iwe ni kwa siri ama sio kwa siri inahitajika uwe na uelewa mpana katika kuimudu dhana ya uongo yani ipo hivi.
Kwa mdanganyaji hii ni siraha inayohitaji uwe na akili sana yakuitumia pia kwa mdanganywaji huu ni mtego usipoweza kuutegua utakuangamiza!.
Nina swali kwako msomaji je, unafikiri ipo haja yakuanzisha sheria yakumlinda mtu aliesema uongo ambao umeweza kumsaidia mtu mwengine...?
Vilevile nina hoja na swali ndani ya hoja!.
Katika vitabu vya dini yani biblia na Quran vinautaja uongo kama dhambi na kitu kisichofaa ambacho kinaweza kumpeleka mtu motoni!, sasa je, vipi ikiwa uongo huo unamsaidia mtu kiafya (kumuepusha asife n.k) ni vyema kumuongopea au ni bora kumuambia ukweli pasipokujali kitakachomkuta ikiwa unafahamu ukimuambia ukweli nini kinaweza kumkuta, je kwenye hili tunaacha dini iongee au hekima..?