Maisha na kusudi

Maisha na kusudi

Mjusi Sharobalo

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2025
Posts
7,442
Reaction score
12,710
Kusudi la maisha sio kuwa na furaha. Ni kuwa na manufaa, kuwa na heshima, kuwa na huruma, na mabadiliko chanya kuwa uliishi na uliishi vema.

Sisi sio wanadamu tunaopitia uzoefu wa kiroho. Sisi ni viumbe wa kiroho tunaopitia uzoefu wa kibinadamu.

Maisha yakiishiwa vizuri, ni marefu ya kutosha. Usiulize dunia inahitaji nini. Jiulize ni nini kinachokufaa uwe hai, kisha nenda kakifanye.

Sababu dunia inahitaji watu walio hai. Hatukumbukwi kwa siku tulizozaliwa wala kufa, bali kwa vile vitu vidogo tulivyovifanya katikati.

Mjusi na tafakari.
 
Aliyekwambia Dunia inahitaji watu walio hai ni nani?

Dunia haihitaji mtu yeyote. Hata binadamu wote tukatoweka saa hii, Dunia itabaki. Tena itanawiri. Uoto wa asili uta ongezeka.

Binadamu ndio anahitaji Dunia, ili aweze kuishi.

Hii Dunia ime exist miaka billion iliyopita bila hata kuwepo binadamu.

Binadamu ameikuta Dunia na kila binadamu ataiacha dunia.
 
Wewe ndio una ishi kwa imani , ebu fikia dunia ambayo binadamu hayupo itakavyo kuwa nzuri , hakuna uharibifu wa mazingira na kila kitu kitarudi katika mazingira tulivu na ya asili kabisa
Kwa maana kwamba unajitakia kifo siyo, ili dunia iwe ya kupendeza!
 
Unavyo lopoka dunia imekaa miaka mingi bila uwepo wa bidamu kama ulikuwepo, tumia akili usitumie mihemko.
lopoka❌️

Ropoka ✅️

Wewe hata kuandika hujui.

Hujui kutofautisha "L" na "R" katika uandishi.

Inabidi urudi chekechea ukajifunze somo la mwandiko.

You ain't mentally enough for intellectual argument.
 
lopoka❌️

Ropoka ✅️

Wewe hata kuandika hujui.

Hujui kutofautisha "L" na "R" katika uandishi.

Inabidi urudi chekechea ukajifunze somo la mwandiko.

You ain't mentally enough for intellectual argument.
Sipangiwi cha kuandika muhimu umenielewa.
 
Binadamu ni kiumbe aliyekuja kuiharibu Dunia,wala Dunia himuhitaji Binadamu bali binadamu ndiye anayeihitaji Dunia ili aishi,

Unaweza kuweka hapa mambo ambayo Dunia inafaidika kwa uwepo wa Binadamu?
Kabisa , dunia inaweza kuendelea vizuri sana hata bila uwepo wetu , ni sisi tu tunajipa umuhimu tusiokuwa nao
 
Binadamu ni kiumbe aliyekuja kuiharibu Dunia,wala Dunia himuhitaji Binadamu bali binadamu ndiye anayeihitaji Dunia ili aishi,

Unaweza kuweka hapa mambo ambayo Dunia inafaidika kwa uwepo wa Binadamu?
Pumzika kwanza msosi wa mchana usafiri vema, hayo maswali tutasanyasanya badae ukiwa mwepesi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom