Amri kuu ni Upendo
JF-Expert Member
- Oct 18, 2012
- 789
- 474
Pindi mtakaposhituka mtakuja jua tu hakuna kitu inaitwa sayari yaani bali ni nyimbo tu za kijinga za kukaririshana majina ya miungu ya kiroma na kigiriki!Mkuu Einstein, udadisi mkubwa ambao unafanywa hivi sasa katika sayari ya Mars, tukianza na NASA kupitia chombo chao cha "Perseverance" huku kimkakati washirikiana kwa karibu na Elon Musk kupitia SPACE X. Na pia CNSA na chombo chao cha "Zhurong" pamoja na kile kingine cha India yaani "Mangalayaan" vyote kwa pamoja vinachunguza kuhusu uwepo wa uhai ama maji katika sayari.
Udadisi huu kutokana na ukaribu wa sayari hii na dunia, ni kitu ambacho kinaweza kuamsha udadisi wa kwa nini vifanyike katika sayari na wala siyo nyingine. Ile hamu ya watu hawa kutaka kwenda kuishi huko inaonyesha pengine kuna habari ya siri za huko. Gharama kubwa zinazotumika ya kwenda huko, licha ya umbali na baridi kali iliyoko huko inaweza kudhihirisha ukweli huo.
Yapo makundi ya siri ambao hujiita kuwa wao ndiyo wamefunuliwa mambo ya siri na Shetani mwenyewe. Pengine hii ndiyo sababu yenye kuifanya Mars kuwa sayari lengwa kuifanya kuwa koloni jipya na hatimaye kama makazi mapya kwa mwanadamu.
Kama kawaida, nukuu ifuatavyo kutoka katika maandiko matakatifu inaweza kutupa uwepo wa makazi sehemu fulani mbinguni, ambayo huitwa kama mbingu ya tatu. Sehemu ambayo Shetani hajawahi kuifahamu hapo awali.
2 Wakorintho 12
2 Namfahamu mtu aliyekuwa ndani ya Kristo ambaye miaka kumi na minne iliyopita alijikuta katika mbingu ya tatu. Kama alikuwa katika mwili au katika roho mimi sijui, Mungu anajua.
3 Na ninafahamu ya kuwa huyu mtu alijikuta yuko Paradiso, kama alikuwa katika mwili au katika roho mimi sijui, Mungu anajua.
4 Naye alisikia mambo ambayo hayawezi kusimuliwa, ambayo mtu hawezi kuyatamka.
Na mkishituka vizuri mtajua tu zaidi kuwa hayo mashirika ya anga yote ni dini moja, nia Moja, kauli moja na msimamo mmoja kunidanganya mimi mjingamjinga hapa!!