GE2020 Maisha baada ya uchaguzi yameanza

ZeMarcopolo

Platinum Member
Joined
May 11, 2008
Posts
14,279
Reaction score
7,685
Wana JF,

Tunashukuru Mungu uchaguzi wetu umekuwa huru na haki. Sasa maisha baada ya uchaguzi yameanza rasmi.

Neno linalotamkwatamkwa sana katika kipindi hiki cha maisha baada ya uchaguzi ni "mawakala".

Napenda kuwakumbusha wanasiasa na vyama vya siasa kutambua yafuatayo kwa ajili ya chaguzi zijazo.

Unapomchagua wakala ni wajibu wako na chama chako kuhakikisha wakala huyo;

1. Anao uwezo wa kiafya kimwili na kiakili kufanya kazi hiyo.

2. Anao uaminifu na utayari wa kuifanya kazi hiyo.

3. Amepata mafunzo ya kumuwezesha kutambua wajibu na haki zake katika kazi hiyo.

4. Umeweka utaratibu wa kumpa support anapopata changamoto.

5 Umeweka utaratibu wa kumsimamia.

6. Umelinda maslahi yake binafsi.

7. Amefika kazini na kuifanya kazi.

Kwahiyo, wakala akishindwa kufanya kazi maana yake mgombea na chama chake hawana mfumo wa kuwapata, kuwaandaa na kuwasimamia mawakala. Ni aibu mgombea au chama kulalamika hadharani kuwa wameshindwa kusimamia watu wachache tu, hasahasa kwa chama kinachotafuta ridhaa ya kuongoza nchi.

Nawapongeza watanzania wote kwa uchaguzi mzuri.

Tuendelee kupokea matokeo rasmi kwa utulivu na amani.

Maisha baada ya uchaguzi yameanza, tujikite kwenye kuijenga nchi yetu.
 
Ni kweli lakini je baadhi ya mawakala wanaodai kufanyiwa fujo je hata kama vyama vyao vimetimiza wajibu inakuwaje.
 
Ya kweli haya
 
Mtoa mada comment yako kwenye mjadala flani umeiona inafaa kuanzishia uzi na umeleta hii.
 
Pongezi huko Mbeya kwa kuanza maisha baada ya uchaguzi kwa kasi.
 
Wakuu wa nchi siye tunaochukuwa masomo ya ukubwani kwa njia ya mtandao tuna siku ya pili leo tunashindwa kupata masomo kutoka kwa walimu wetu. Chonde chonde msituharibie elimu yetu ya lala salama😭
Yaani kama siyo wewe, vile!!!Ha ha haaa!
====
MB unazimalizia kwa kuwaambia lugha za kuudhi watanzania halafu lawama unazibwaga kusiko husika!
 
Kuna watu lazima wajiaandae sasa kiakili.hasa Kagera na koote kulikokuwa na vidomo domo.
Wafanyakazi kwa nyanja zote mjiaandae zaidi kifrika.

Wale mliomba ajira zile mkaae vyema kiakili.Simama funga mkanda.
 
Kuna watu lazima wajiaandae sasa kiakili.hasa Kagera na koote kulikokuwa na vidomo domo.
Wafanyakazi kwa nyanja zote mjiaandae zaidi kifrika.

Wale mliomba ajira zile mkaae vyema kiakili.Simama funga mkanda.
Maisha lazima yaendelee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…