Bartazar
JF-Expert Member
- Oct 4, 2011
- 1,043
- 565
Hii kitu imenitokea live, demu wng anayesoma UDSM mwaka wa mwisho, na tukiwa tumepanga mikakati mingi ya maisha ghafla akawa hapokei simu. Mwanzo nilidhani simu yake kaiacha mbali hasa ukizingatia mazingira ya kupanga nje ya hostels za vyuo husika, nikahisi kuwa huenda kaiacha simu room. Hivyo nikasitisha kwanza zoezi la kupiga simu, kwa lengo la kumpigia usiku, nikiamini kuwa muda huo pilika pilika zitakuwa zimeisha. Na kama atakuwa aliitelekeza simu yake, muda huo lazima atakuwa nayo, pamoja na imani yangu kuwa kuziona tu missed calls angepiga tu. Ajabu ni kwamba hakupiga, na nilipompigia bado hakupokea. Nikamtumia ujumbe bado haukujibiwa. Siku ya tatu alinitumia meseji, baada ya mimi kupiga sana na kumtumia ujumbe kuwa 'yupo bize' na maandalizi ya mitihani! Toka hapo mawasiliano yamekatika, hakuna simu wala meseji. Hivi naona ni viroja. Hivi waungwana ninyi mmesoma vyuoni wengi wenu! Katika hali ya kawaida mchumba wako au mpenzi wako akikupigia simu unaweza kubehave namna hiyo hata kama upo bize? Je, ni komedy gani hiyo ninayochezewa wanajukwaa?