Gagurito
JF-Expert Member
- Feb 11, 2011
- 5,600
- 803
Ukistaajabu ya Mussa...ya firauni! Ni uhusiano mbovu ulioleta jambo la ajabu kutokea bt ndio ukweli wenyewe huo na imetokea Iringa, mpaka niandikapo thread hii nipo iringa na hili ndio gumzo la mtaani.. Mume, mwalimu wa shule ya msingi moja ya hapa iringa mjini amezuiwa kuzika, mwili/maiti ya mkewe ikafukuliwa na ndugu za mkewe wakiongezwa baba mkwe wake na kusababisha marehemu kuzikwa usiku kwa kutumia taa za chemli, karabai, tochi na mishumaa kisa mwalimu (mume wa marehemu) hakumalizia kulipa mahali. Hali hii ikasababisha wananchi waombolezaji kuchangia pesa kumlipa baba mkwe ili mwili wa marehemu uzikwe, baba mkwe kapokea na akaonekana akinywa pombe kwa furaha na rafiki zake. Kwa maoni ya mume (mwalimu) anasema mahali alilipa yote toka miaka ya 90 na ameishi ya marehemu kwa takriban miaka 20 pasipo matatizo yoyote ukweni! WanaJF hii stori niyakweli na imetokea hv karibuni hapa iringa.. Sijui unalichukuliaje swala hili? TUNAOTAKA OA TUJIANDAE, KWA MWENDO HUU TEMBO CARD MASTER CARD MUHIMU. Hebutujadili..