Nakubaliana na wazo lako kwa 100%
SABABU NI HIZI
1, Historia inaonyesha kuwa karne ya 5 dini na serikali/siasa zilipochanganywa mamilioni ya watu waliuawa
2. Maandiko yanasema ya Kaisari mpeni Kaisari na ya MUNGU mpeni MUNGU
3. Viongozi wa dini ndio neutral ground ambapo watu wote watapata kimbilio
Hii haina maana ya kuwa serikali iko sahihi laa, na pia viongozi wa dini wana nafasi ya kuita kiongozi wa serikali na kumpa ushauri na mtazamo mwema .
Sasa hivi kiongozi wa dini ni mwana siasa na anasema uongo. mfano mwanasiasa alisema kuwa akiwa mbunge atawapeleka watu nje ya nchi kujifunza na hajapeleka mtu wala aliyosema hajafanya. Hii inamuondoa kama kiongozi wa kiroho wa watu