Uchaguzi 2020 Mahera (NEC) na Nyahoza (Naibu Msajili wa Vyama), kwanini hamkujipanga kabla ya kuonesha sinema yenu?

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Wadogo zangu Dr.Mahera na Nyahoza mmeniangusha sana. Nia ya kukisaidia chama chetu cha CCM mnayo. Uwezo mnao. Nguvu mnazo. Kwanini hamna maarifa? Dr. Mahera umejitokeza mbele ya watanzania na kuhabarisha kuwa mgombea wa CHADEMA Tundu Lissu amekiuka Kanuni za Maadili ya Uchaguzi. Ukasema kuwa una nguvu na mamlaka ya kushughulika na hilo. Ukatamba kuwa tayari 'umeshamlima' Lissu barua ajitokeze mbele ya Kamati ya Taifa ya Maadili ya Uchaguzi.

Dr. Mahera ukada wa CCM na 'ushushushu' ukakuumbua. Ukakusukuma kusema visivyotakiwa kusemwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC inayosimamia uchaguzi husika. Ukamwaga sera za CCM na kuzikosoa waziwazi sera za Lissu. Ukakosoa na kuonesha Lissu anakosea bila ushahidi wowote wa maana zaidi ya kufokafoka. Ukashindwa kujizuia kabisa. Ukashindwa kuficha hisia zako dhidi ya Lissu huku ukimuunga mkono Dkt. Magufuli. Umeshindwa kabla ya kuanza!

Ndugu Nyahoza nawe umeningusha. Baada ya mkurugenzi wa Uchaguzi kutangaza kumwandikia barua Lissu, nawe jana ukapeleka barua kwa bodaboda CHADEMA. Ni barua ile ile ya Mkurugenzi au nawe umepandishia barua juu ya barua ili kumtinga Lissu na barua? Nawaambia ukweli, Dr. Mahera na Nyahoza hamkujipanga na kupangika. Muda huu wa kampeni, mbinu zinapaswa kuwa zilizopangika kimyakimya. Si hila za wazi kama zenu.

Hivi, Dkt. Magufuli wa CCM, tangu kuanza kwa kampeni zake, hakuwahi kuvunja Maadili ya Uchaguzi au yale ya vyama vya siasa? Mnatazamwa, mnafikiriwa. Watanzania si wajinga, nao wanaweza kutafakari na kung'amua. Kwa maneno na matendo yenu: Dr. Mahera na Nyahoza, jambo lolote dhidi ya Lissu ni batili kwakuwa mmeshaamua kabla ya kuitisha hivyo vikao vyenu.

Acheni demokrasia ichukue mkondo wake!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Mbeya, Tanzania).
 
Mimi nashauri Lisu aachwe aropoke atakavyo maana ni sehemu ya tiba kwa yaliyomkuta.

Wote tunajua hata shinda. Hivyo aachwe tutamfundisha sisi wananchi kwenye box la kura.

Aachwe aendelee kuropoka kwa ajili ya kujitibu kwa yaliyomsibu.
 
Mimi nashauri Lisu aachwe aropoke atakavyo maana ni sehemu ya tiba kwa yaliyomkuta.

Wote tunajua hata shinda. Hivyo aachwe tutamfundisha sisi wananchi kwenye box la kura.

Aachwe aendelee kuropoka kwa ajili ya kujitibu kwa yaliyomsibu.
Utamfundisha ww. Ww ni nani nchi hii uwasemee wananchi wa tanzania?
Kila mtu kura yake ni siri yake mwenyewe. Usi act kama unajua kura za kila mtu
 
Wadogo zangu Dr.Mahera na Nyahoza mmeniangusha sana. Nia ya kukisaidia chama chetu cha CCM mnayo. Uwezo mnao. Nguvu mnazo. Kwanini hamna maarifa? Dr. Mahera umejitokeza mbele ya watanzania na kuhabarisha kuwa mgombea wa CHADEMA Tundu Lissu amekiuka Kanuni za Maadili ya Uchaguzi. Ukasema kuwa una nguvu na mamlaka ya kushughulika na hilo. Ukatamba kuwa tayari 'umeshamlima' Lissu barua ajitokeze mbele ya Kamati ya Taifa ya Maadili ya Uchaguzi.

Dr. Mahera ukada wa CCM na 'ushushushu' ukakuumbua. Ukakusukuma kusema visivyotakiwa kusemwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC inayosimamia uchaguzi husika. Ukamwaga sera za CCM na kuzikosoa waziwazi sera za Lissu. Ukakosoa na kuonesha Lissu anakosea bila ushahidi wowote wa maana zaidi ya kufokafoka. Ukashindwa kujizuia kabisa. Ukashindwa kuficha hisia zako dhidi ya Lissu huku ukimuunga mkono Dkt. Magufuli. Umeshindwa kabla ya kuanza!

Ndugu Nyahoza nawe umeningusha. Baada ya mkurugenzi wa Uchaguzi kutangaza kumwandikia barua Lissu, nawe jana ukapeleka barua kwa bodaboda CHADEMA. Ni barua ile ile ya Mkurugenzi au nawe umepandishia barua juu ya barua ili kumtinga Lissu na barua? Nawaambia ukweli, Dr. Mahera na Nyahoza hamkujipanga na kupangika. Muda huu wa kampeni, mbinu zinapaswa kuwa zilizopangika kimyakimya. Si hila za wazi kama zenu.

Hivi, Dkt. Magufuli wa CCM, tangu kuanza kwa kampeni zake, hakuwahi kuvunja Maadili ya Uchaguzi au yale ya vyama vya siasa? Mnatazamwa, mnafikiriwa. Watanzania si wajinga, nao wanaweza kutafakari na kung'amua. Kwa maneno na matendo yenu: Dr. Mahera na Nyahoza, jambo lolote dhidi ya Lissu ni batili kwakuwa mmeshaamua kabla ya kuitisha hivyo vikao vyenu.

Acheni demokrasia ichukue mkondo wake!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Mbeya, Tanzania)
Do we need figureheads and unscrupulous leaders in this country
 
Back
Top Bottom