Mahari...

Mahari...

stata mzuka

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2012
Posts
4,834
Reaction score
1,765
Wakuu habari Zenu, twende kwenye mada moja kwa moja.

Hivi Mahari ni muhimu kulipwa? Mantiki ya mahari ni nini? Hivi hatuoni kuwa ni sababu ya w/wake kunyanyaswa? M/ume analipia Mahari kwa maana ya zawadi au kununua? Tunaonaje Mila nyingine zikafutwa ni pamoja na kuoa kwa kulipa mahari.

Nawasilisha wakuu.
 
Kaa chini mwenyewe ufikirie kidogo mke ukimuoa labda kwa mahari ya sh 1ml unakaa na mke labda miaka 20 au mpaka kifo ni mangangapi amekufanyia na uliyomfanyia au kazaa watt 4 unadhani kila mtt anaweza kuwa sh ngapi kwa iyo milion yako kwa hiyo mahari ni proses tu ya kiheshima badala ya kuishi kihuni na sio umemnunua mke wenye uelewa watafafanua zaidi.
 
Mahari ni utamaduni wetu,pia ni heshima kwa wazazi na kwa mtaa unaoishiii tena ikianzia m.2 au tatu hivi lol
Kuna rafiki ni mwarabu katolewa milion 5 lol
 
Watu wana njaa jamani, hata mahari imekuwa mzigo?

Mwanamke kunyanyaswa sio function ya mahari peke yake, wote waliolipiwa mahari wananyanyaswa? AU je, wanawake waliowekwa kinyumba tu bila kufuata utaratibu wa mahari hakuna wanaonyanyaswa?

Au wanamme wanaopigwa na wake zao wamelipiwa mahari?
 
Mahari ni zawadi kutoka kwa mume kwamke wake na sio ya family, wengine sijui wanataka mkaja kilemba, sijui mshaka gani mengine,lakini kwa ufupi nizawadi ya mke kutoka kwa mumewee,na haina limit kua mpe mil1 au 100 mpe elfu 10 au 50, hata pete ya silver pia anaweza kukupa zawadi,muhimu maelewano...
 
bride price is the spirit of humanity and pride.. nenda bure uone!

kunyanyasika ni mengineyo... otherwise na yenyewe yangekuwa yanatolewa mahari!

sie kwetu bila ming'ombe kama hii 20, hujabeba mke..!

ng%27ombe2.jpg
 
Mahar ni utamaduni wetu waafrica.c kununua mke bali huonyesha heshima na shukran kwa wazaz wa mke kwakuwa nin make mndiye anaewaacha wazaz wake na ndugu zaje na kumfuata mume na ukoo wake.kimsingi kisheria kutokulipa mahari hakuwez kuibatilisha ndoa ambayo imefuata taratibu zote za msingi.unyanyaswaji wa wanawake nin kit kingne kabsa na gains uhusiani kabsa na mahar
 
mi ninachoelewa kwa kutoa mahari sio kwa kununua ni kama kushukuru fulani na ndio maana haimalizwagi yote hapo hapo, ila kuna watu hawajui maana ya mahari
 
Kaa chini mwenyewe ufikirie kidogo mke ukimuoa labda kwa mahari ya sh 1ml unakaa na mke labda miaka 20 au mpaka kifo ni mangangapi amekufanyia na uliyomfanyia au kazaa watt 4 unadhani kila mtt anaweza kuwa sh ngapi kwa iyo milion yako kwa hiyo mahari ni proses tu ya kiheshima badala ya kuishi kihuni na sio umemnunua mke wenye uelewa watafafanua zaidi.


I beg to differ with you hapo kwenye red. Yule siyo asset kuwa anakuja kuzalisha, wala watoto siyo mali ya mume pekee. Mahari ni utamaduni tu ambao huonesha shukrani kwa familia ya mke/mume. Mbona wahindi wanaume ndo wanatolewa mahari?
 
Mahari ni utamaduni wetu,pia ni heshima kwa wazazi na kwa mtaa unaoishiii tena ikianzia m.2 au tatu hivi lol
Kuna rafiki ni mwarabu katolewa milion 5 lol
hata mimi kwa mwaarab natoa m.5 c najua kabaang kama kawaida.
 
Its just a formality inayohusiana na udumisho was mila zetu... Haimaanishi umemnunua mkeo
 
Heshima Ndio imelala hapo vinginevyo hamna ndoa....
 
vya kwetu ni mali,vya kigeni ni magarasha.mwafrika atabaki kuwa mwafrika na mzungu ni mzungu tu kwa hiyo si kila kitu ni cha kuiga.linda heshima yako kwa kutunza uaslia wako,mmeelewa jamni?
 
Wazaz wengine ndio wamefanya pa kutokea kimaisha kwenye mahari sasa mtu unataka Mil.5 au Ng'ombe 20 unaenda kufungua zizi au?
 
Back
Top Bottom