Mahari yaniachisha na mke wangu

Mahari yaniachisha na mke wangu

Mkami Lum

JF-Expert Member
Joined
Feb 23, 2013
Posts
414
Reaction score
96
Niaje wana MMU

Yamenikuta mwenzenu, mwezi uliopita nilipeleka mahari sehemu fulani ili niweke huduma karibu. Sasa yamenikuta, wamenipangia Sh Mil 6.2.

Ukilinganisha na uwezo wangu nashindwa kuilipa hiyo, nimeamua kumuacha coz na yeye anasema hataki kuja bila wazazi kuridhia na anamimba tayari ya miezi mitano na wazazi wake hawajui.

Mie nimeamua kuachana nae kama anakua na msimamo huo na nitakomboa mtoto.

WE UNAONAJE?
 
Niaje wana MMU!
Yamenikuta mwenzenu,,, mwezi uliopita nilipeleka mahari sehemu fulani ili niweke huduma karibu. Sasa yamenikuta,,, wamenipangia Sh Mil 6.2. Ukilinganisha na uwezo wangu nashindwa kuilipa hiyo,,, nimeamua kumuacha coz na yeye anasema hataki kuja bila wazazi kuridhia na anamimba tayari ya miezi mitano na wazazi wake hawajui... Mie nimeamua kuachana nae kama anakua na msimamo huo na nitakomboa mtotto, WE UNAONAJE???????

Hili tatizo sana kwa baadhi ya wazazi, subiri lijulikane hilo kuwa binti ana mimba yako, then itunze, mambo mengine baadae.
 
haimalizwi sawa but kumbukakwa kiwango hicho itakuwa sh ngap itayofaa kupeleka?
 
Hiyo hela ni ndogo kulinganisha na huduma utakazopewa...

Money mongers utawajua kwa miandiko yao. Kijana alipe mahari ya 6m? Ana mda gani kazini? Ana kipato gani? Amewekeza wapi ili apate 6m ya mahari? Watu wenye attitude hii huwa naona hamnazo..!
 
we peleka 1m wambie nyingine utamaliza wakishakupa mkeo.....kuna rafiki yangu alipigwa 2m akawapa laki na nusu tuu ...nilikuwepo kwenye hicho kikao walinuna haoo lakini binti keshapigwa mimba watafanyaje wakampa mke na hajamaliza hadi leooo....kitu kikubwa na kizuri ulichofanya ni kumpa mimba huyo binti we jipange na 1m lazima wakubali hawana njia nyingine
 
6m kwa kipi hasa? Ridiculous kabisa!!
 
Money mongers utawajua kwa miandiko yao. Kijana alipe mahari ya 6m? Ana mda gani kazini? Ana kipato gani? Amewekeza wapi ili apate 6m ya mahari? Watu wenye attitude hii huwa naona hamnazo..!

Mpk kijana afikie kuoa ina maana kajiaandaa,,,,,,,,
Bora niwe hamnazo nipate kuliko kuwa nazo afu nikose
 
Mpk kijana afikie kuoa ina maana kajiaandaa,,,,,,,,
Bora niwe hamnazo nipate kuliko kuwa nazo afu nikose
Unamuongelea mtanzania wa kipato gani we mwanamke? Tatizo itakuwa unahitaji "ready-made" wewe!
Kwa maisha ya kawaida ya mtz wa haki ya kawaida hawezi mudu gharama hizo+sherehe then aanze maisha akiwa vizuri.
Mwanamke mwenyewe yupi wa kumlipia mahari kubwa hivyo, hawa waliotembea na kujaza fuso ndo wakuwalipia 6m? You must be kidding
 
Mmmh...ebu tafuta mwanamke mwingine uoe huyo wazazi wake hawajataka aolewe au hawajapenda aolewe na wewe,au labda majina yako huenda yanashabihana na akina Ruge,Tiba au Chenge wazazi wakadhani mgao wa escrow umetia maguu home..!
 
Kusoma hujui hata kuangalia picha huwezi?

HUTAKIWI, na inawezekana huyo mwanamke hakutaki tena amewaambia wakupandishie mahali ili aachana na wewe! chapa lapaaaaaaaa
 
Unamuongelea mtanzania wa kipato gani we mwanamke? Tatizo itakuwa unahitaji "ready-made" wewe!
Kwa maisha ya kawaida ya mtz wa haki ya kawaida hawezi mudu gharama hizo+sherehe then aanze maisha akiwa vizuri.
Mwanamke mwenyewe yupi wa kumlipia mahari kubwa hivyo, hawa waliotembea na kujaza fuso ndo wakuwalipia 6m? You must be kidding

Naongelea wtz hawa hawa,,,,, labda tu awe hana hio hela!!!!!!! nina mfano hai wa mtu kalipiwa mahari ya tshs m5 last w'end......
Hao unaooita wametembea na kujaza fuso ndio wapya kwa wenzio.
 
Huduma gani? kwani unauziwa? yeye atakazo kuja kupata atalipia? au yeye hakuna huduma anazopata?

Huduma ziko nyng like kufua,, kupika,,, usafi
achia yote kubwa ni mimba na kuzaa na kulea wakati huo ww uko baa na mchepuko unafikiri hiyo m6 inafit?????????
 
Back
Top Bottom