Mahari ya harusi ikatwe kodi ya TRA

Mahari ya harusi ikatwe kodi ya TRA

Kule Simiyu, SHinyanga, Mwanza, Mara na mikoa ya jirani itabidi wajenge mazizi ya ng'ombe wafungue na mabucha ya kutunzia nyama.

Mahari ngombe 100, TRA wanapewa ng'ombe 18. Kama mahari ng'ombe mmoja, wanapewa mat.ako ya ng'ombe, raha kweli.

We Kongosho acha vituko japo una point. Kuna sehemu mahari wanatoa nafaka labda TRA waanzishe na maghala kabisa.
 
Moja ya sheria muhimu ya nchi ni PAYE (Pay As You Earn).

Naona nchi yetu inapoteza pesa ambazo zingetumika kununua madawati na kulipa mishahara kwa walimu.

Kuingiza pesa bila kulipa kodi huko ni kuhujum uchumi wa nchi, nadhani mnafaham adhabu ya kuhujum uchumi ipoje nchini kwetu.

Mimi kama MCHUNGUZI HURU napendekeza TRA ianzishe utaratibu ambapo kila familia itakayopokea mahari kwaajili ya harusi wakatwe asilimia 18 ya pesa hizo.

ASANTENI
MCHUNGUZI HURU

Makabila mengi ndoa ikivunjika mahari hurudishwa. Sasa kama TRA watakuwa wamelamba hiyo asilimia 18 hapo utashauri nini wakati wa kurudisha mahari?
 
Ulikuwa hujui? Basi ulikimbia hesabu za uwiano.


Umri wa Maria ni mara 3 ya umri wa Jose, baada ya miaka 7, maria atakuwa na miaka 38. Ukichukua umri wa sasa wa maria jumlisha na jose ni miaka 19. Tafuta umri wa Jose.

Hahaahahah kwa hyo mat.ako ya ng'ombe ni asilimia 18 ya ng'ombe mzima? Hahahahahhahaa
 
Nafikiri mleta mada una matatizo ya lugha ya kiswahili. Hivi hiki unachokiita "mahari ya Harusi" ni kitu gani hicho. Hivi kweli kwenye tamaduni zetu tuna kitu kinaitwa hivyo? Ninavyofahamu mimi mahari ni kitu kinachojitegemea na Harusi ni kitu kingine. Mahari ni mali inayotolewa kwa wazazi wa binti (kwa utamaduni wa Waafrika) ili watoe idhini kwa binti yao kuolewa. Na Harusi ni kitendo cha Bwana kukabidhiwa mke rasmi. Kumbuka unaweza kukabidhiwa mke bila kutoa mahali. Inawezekana nakosea lakini wajuzi wa kiswahili watusaidie hapa.

Tiba
 
kunahaja ya kuomba resiti unapopeleka mahari iwapo utadaiwa kodi una resiti ya kuonesha umelipa kiasi gani
Tusisahau na wale wadada poa nao watowe resiti pia kwa huduma wanayotowa na kwenye kulipia kodi utowe na gharama za kazi pia
 
Back
Top Bottom