DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam imetupilia mbali pingamizi lililowasilishwa na Tundu Lissu kuhusu uhalali wa hati ya mashtaka pamoja na maelezo ya mashahidi ambayo yanadaiwa kuandikwa kinyume cha sheria.
Lissu alidai hati hiyo pamoja na viambatanisho vyake, ikiwemo maelezo ya mashahidi, vimeandikwa kinyume cha sheria na havikidhi matakwa ya kisheria.
Lissu alidai hati hiyo pamoja na viambatanisho vyake, ikiwemo maelezo ya mashahidi, vimeandikwa kinyume cha sheria na havikidhi matakwa ya kisheria.
Katika uamuzi wake, Jaji Nduguru amesema hati ya mashtaka iliyopo Mahakama Kuu ni ileile iliyowasilishwa awali Mahakama ya Kisutu na haijafanyiwa marekebisho yoyote.
Ameeleza kuwa kifungu cha 135 na 138 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA) vinaweka wazi matakwa ya kisheria kuhusu muundo na maelezo ya hati ya mashtaka, na kwamba hati iliyowasilishwa inajitosheleza kisheria.
Kuhusu hoja ya maelezo ya mashahidi kuandikwa kinyume cha sheria, Mahakama imekataa pingamizi hilo kwa maelezo kuwa halikuwasilishwa kwa wakati sahihi, na hivyo halina msingi wa kisheria.
Kwa uamuzi huu, shauri la msingi linaendelea kusikilizwa kwa ushahidi.
Endelea kutufatilia kwa taarifa zaidi
Ameeleza kuwa kifungu cha 135 na 138 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA) vinaweka wazi matakwa ya kisheria kuhusu muundo na maelezo ya hati ya mashtaka, na kwamba hati iliyowasilishwa inajitosheleza kisheria.
Kuhusu hoja ya maelezo ya mashahidi kuandikwa kinyume cha sheria, Mahakama imekataa pingamizi hilo kwa maelezo kuwa halikuwasilishwa kwa wakati sahihi, na hivyo halina msingi wa kisheria.
Kwa uamuzi huu, shauri la msingi linaendelea kusikilizwa kwa ushahidi.
Endelea kutufatilia kwa taarifa zaidi