Magufuli,Ubabe katika shughuli za Serikali umepitwa na wakati!

Uongozi ni kutumia hekima na busara. Sheria peke yake siyo uongozi. Awe Mkapa, Pinda na hata Kikwete wamekuwa wakiokoa wananchi mara kadha kutokana na kadhia ya Magufuli. Inadaiwa ati anapendwa, na nani??? Hapendwi, bali anautumia mfumo uliokufa kujikweza na kuonekana yeye ni mchapa kazi. Ni sawa na Mrema. Mrema alikuta mfumo wa utawala uliokufa, kwa hiyo hali kama hiyo huwafanya baadhi yetu kufikiria kuwapa madaraka watu kama kina Magufuli. Kiongozi huongozwa na mambo mengi, maana hata kauli lazima itolewe kwa hekima. Pamoja na kile kilichoonekana ubabe lakini mara nyingi Mkapa alikuwa makini sana katika kuwasilisha ujumbe wake, vivyo hivyo kwa Kikwete na Pinda. Unaposikia kiongozi anatamka haogopi kufa ujue hilo ni janga. Kama haogopi anamtangazia nani. Hao viongozi na mawaziri wa kulialia, nakufa, natishiwa, siogopi nk, hawafai kabisa. Ni majanga!!!











Wewe unabusara gani kama mhuni tu,sheria lazima zifuatwe unajiganya kwa kuvunja sheria halafu unataka eti busara ni akili za kinalisu hizi za unafiki na umbea.
 
Muache jembe awe mbabe. Wabongo tu wajing wajinga sana. Wewe unaambiwa mfano malori yanaharibu barabara wewe unashabikia yaendelee kuharibu barabara. Halafu zikiharibika wewe huyo huyo utaanza kumtukana Mh. Magufuli kwa matusi kama fisadi au kuitukana CCM ni mafisadi. Tuache ujinga na unafiki, haswa we mleta maada. Muacheni Magufuli afanye kazi. Wenye malori wapunguze uzito, waache kutuharibia barabara.
 
watanzania bhana wanapenda viongozi wazembe ndiyo maana mtu akiwa kwenye wazifa flani akitoka masikini wanaanza kumcheka akifisadi kwao huyo ndiye shujaa wao hivi nina kaliloga hili taifa au lina laana :A S-confused1:

Nakubaliana na wewe. Watanzania ni waaajiinga waaajiinga. Wewe ukitoka kwenye nafasi masikini yaani hata ukiugua useme upitishe bakuri wakuchangie ukatibiwe kama ulikuwa kiongozi wa juu basi watakucheka vibaya mno. Mfano aliyekuwa mwanasheria mkuu marehemu francis nyalali, alistaf maskini na akaja ugua na hakuwa na hela za matibabu mil 10. Watu walimcheka eti alikuwa mwanasheria mkuu atakosaje mil 10. Ndiyo maana chenge hakufanya kosa, kajilipa vizuriiiiii, mpaka watu tena wanamuita fisadi
 
Ukishajua chanzo cha neno "bongoland", wala hutapata shida juu ya hawa wanaomwandama Magufuli. Nchi hii kila kitu watu wanataka kifanywe kisanii-sanii tu. Ukisikia watu wanamchukia polisi, basi ujue ni yule asiyehongeka! Madereva wakimsifu trafiki, ujue huyo trafiki hatoi adhabu kwa wanaovunja sheria za barabarani. Shuleni ukisikia mwalimu anapewa jina la "mnoko", ujue ni yule anayetaka wanafunzi wawe darasani wakati wa vipindi. Tukiendelea na upuuzi huu nchi hii itakuwa tambara bovu! Najua kwa hili Magufuli atashindwa, maana Pinda hatachelewa kumtaka awaache! Kila kitu nchi hii ni uvunjifu wa sheria tu. Hata hiyo katiba mpya inayokuja, kwa mwenendo huu, bure tu!

Mkuu salaam.Hapa sidhani kinachokataliwa na hawa watu ni kufuata sheria!Iyo Allowance ya 5% walipewa kwa utaratibu unaoeleweka sasa unapotaka kuuondoa pia zingatia utaratibu na utoe muda.Mfano malori yaliyokwishapakia yapo barabarani yasihusishwe watoe kama wiki moja ili uanze.Kitu kingine wanacholalamikia kwanini mizani zinapima uzito tofauti tena kwa kiasi kikubwa ivyo?Mizani nisehemu kubwa sana ya kero kwani hazikuandaliwa ktk mazingira rafiki zinasababisha foleni kwa wasiohusika au nikuulize mzee lori la mafuta limepima kibaha on the way to Zambia kila mizani linakopita linatakiwa kupima ..ina maana mafuta yanaongezeka uzito kila liendako kwanini lisipime mara moja tu kama ok its ok why repetition every now and then?
 
Mie ninadhani kuna issues ambazo inabidi ziwekwe wazi ili tupate uhakika.. Kwa mfano kuna madai toka kwa wenye magari kwamba kwanza mizani inasoma tofauti.. Kwamba kama ukipima kibaha na baadae kwenda kupima makambako kwa mfano mizani inasoma tofauti.. Jeee hili dai lina ukweli wowote..? Na pili ni nini mantiki ya kupima mabasi katika mizani..? Badala ya malumbano ni vyema haya yakazungumzwa ili mwisho wa siku tujue usahihi uko wapi..
 
Ukishajua chanzo cha neno "bongoland", wala hutapata shida juu ya hawa wanaomwandama Magufuli. Nchi hii kila kitu watu wanataka kifanywe kisanii-sanii tu. Ukisikia watu wanamchukia polisi, basi ujue ni yule asiyehongeka! Madereva wakimsifu trafiki, ujue huyo trafiki hatoi adhabu kwa wanaovunja sheria za barabarani. Shuleni ukisikia mwalimu anapewa jina la "mnoko", ujue ni yule anayetaka wanafunzi wawe darasani wakati wa vipindi. Tukiendelea na upuuzi huu nchi hii itakuwa tambara bovu! Najua kwa hili Magufuli atashindwa, maana Pinda hatachelewa kumtaka awaache! Kila kitu nchi hii ni uvunjifu wa sheria tu. Hata hiyo katiba mpya inayokuja, kwa mwenendo huu, bure tu!

Umenena Baba..
 
Uongozi ni kutumia hekima na busara. Sheria peke yake siyo uongozi. Awe Mkapa, Pinda na ham. ta Kikwete wamekuwa wakiokoa wananchi marai kadha kutokana na kadhia ya Magufuli. Inadaiwa ati anapendwa, na nani??? Hapendwi, bali anautumia mfumo uliokufa kujikweza na kuonekana yeye ni mchapa kazi. Ni sawa na Mrema. Mrema alikuta mfumo wa utawala uliokufa,


kwa hiyo hali kama hiyo huwafanya baadhi yetu kufikiria kuwapa

madaraka watu kama kina Magufuli. Kiongozi huongozwa na mambo mengi, maana hata kauli lazima itolewe kwa hekima. Pamoja na kile kilichoonekana ubabe lakini mara nyingi Mkapa alikuwa makini sana katika kuwasilisha ujumbe wake, vivyo hivyo kwa Kikwete na Pinda. Unaposikia kiongozi anatamka haogopi kufa ujue hilo ni janga. Kama haogopi anamtangazia nani. Hao viongozi na mawaziri wa kulialia, nakufa, natishiwa, siogopi nk, hawafai kabisa. Ni majanga!!!

Umenena mkuu fikra pevu. Tatizo sisi watz tumelogwa tukishampenda mtu basi hata kama ananuka inya tutasema ni pafyumu mpya!!!!!
 
halafu hayo malori yakiwa hayapo barabarani hizo reli ziingie mpaka ndani kuchukua mazao vijijini?halafu nani kakuambia wenye malori wanataka kuzidizisha mizigo?
Huyo makufuli fisadi tu hana lolote wanatafuna pesa za ujenzi kinyama barabara zinajengwa chini ya kiwango baada ya miezi sita zimebomoka sasa analeta kizogo cha kusingizia wasafirishaji sasa kama mizigo ipo na pesa ipo si barabara zijengwe kukidhi mahitaji au hayo magari yenye tani zisizotakiwa yalipitia bandari gani na nani aliyapa leseni huyo makufuli apewe urais na nani si atapigwa kiberiti mitaani na watu wenye hasira kama kibaka
 
Ombi,,mwenye uelewa na upimaji wa magari katika mizani,,naona anifahamishe tafadhali au mwenye link yoyote kuhusu mizani anitumie ili namimi nifanane na ulimwengu wa leo,,,,vile vile kuhusu hii 5% anifafanulie inakuaje
 
Uongozi ni kutumia hekima na busara. Sheria peke yake siyo uongozi. Awe Mkapa, Pinda na hata Kikwete wamekuwa wakiokoa wananchi mara kadha kutokana na kadhia ya Magufuli. Inadaiwa ati anapendwa, na nani??? Hapendwi, bali anautumia mfumo uliokufa kujikweza na kuonekana yeye ni mchapa kazi. Ni sawa na Mrema. Mrema alikuta mfumo wa utawala uliokufa, kwa hiyo hali kama hiyo huwafanya baadhi yetu kufikiria kuwapa madaraka watu kama kina Magufuli. Kiongozi huongozwa na mambo mengi, maana hata kauli lazima itolewe kwa hekima. Pamoja na kile kilichoonekana ubabe lakini mara nyingi Mkapa alikuwa makini sana katika kuwasilisha ujumbe wake, vivyo hivyo kwa Kikwete na Pinda. Unaposikia kiongozi anatamka haogopi kufa ujue hilo ni janga. Kama haogopi anamtangazia nani. Hao viongozi na mawaziri wa kulialia, nakufa, natishiwa, siogopi nk, hawafai kabisa. Ni majanga!!!

Big up sana mkuu.
 
Ninawapenda viongozi wanaosimamia sheria, lakini ukiwa mkweli lazima usimamie sheria zote. Nimwulize waziri amechukua hatua gani kwa wale waliojenga barabara kati ya Chalinze na Ruvu. Barabara ya hovyo ina mawimbi haina kiwango na inaharibu magari, je wajenzi na wasimamizi wa barabara ile kama kweli anasimamia sheria na haki amewachukulia hatua gani. Barabara haijawekwa lami bali imetiwa tope la lami (kama lipo). Kama kweli serikali iliwapa msamaha mpaka asilimia tano basi ilikuwa na sababu za kufanya hivyo haikupashwa basi kufuta msamaha huo kwa ubabe tena magazetini, alipashwa kuwaita viongozi wa wenye malori ili jambo hilo lizungumzwe kabla ya utekelezaji wake.

Waziri alipashwa kuiga mfano wa Rais ambaye pamoja na kuwa mswaada wa rasimu ya katiba mpya kupitia sehemu zote kisheria bado busara ilimwongoza kuwasihi viongozi wa upinzani wakae mezani wajadiliane ili kuepusha shari. Rais kwa uwezo aliopewa kikatiba alikuwa anaweza kutia saini sheria ile na asingekuwa na kosa kisheria na kikatiba, lakini busara za kawaida hazikumwongoza kufanya hivyo japo sheria ilimruhusu. Tulitegemea waziri naye angekuwa hivyo, angeongozwa na busara zaidi kuliko sheria, angekaa na viongozi wa wenye malori na kujadiliana nao, nina hakika wangefikia muafaka bila hata sisi wengine kujua kilichotokea. Lakini hii njia isiyokuwa ya busara aliyoamua kuichukua hakika itawadhuru waliokuwemo na wasiokuwemo, mfano leo mabasi yamechelewa kuondoka Ubungo. Kama vile kidonda kukitia chumvi waziri bila hekima anasema wenye malori wakitaka kugoma wakae majumbani mwao, anasahau kwamba si kila lori linaenda nje ya nchi, kitendo chake hiki kitasababisha upungufu mkubwa wa bidhaa mikoani ha hivyo kusababisha mfumuko wa bei.

Hayo ndiyo matatizo yetu wakati waziri mmoja anapigana kuhakikisha bidhaa zinasambazwa nchini kwa urahisi ili kudhibiti mfumko wa bei waziri mwingine kutoka serikali ile ile anaweka vikwazo potelea mbali hata kama mfumuko wa bei utapanda. Ni matumaini yetu kwamba kama kawaida yake Rais ataongozwa na busara na hekima kuliangalia hili kwa mapana yake ili kuweka mambo sawa bila kuathiri upande wowote. Nchi hii ni yetu sote watawala na watawaliwa hakuna sababu ya UBABE.

Hiyo road section kati yaRuvu na Chalinze ni mbaya, ila kwa kumbukumbu zabgu haikujengwa wakati wa Hon. Magufuli. Wakati huu wa Magufuli waliweka tabaka tu juu ya lami ambayo imeshashindwa kuhimili vehicular traffic loads, na kimsingi inaonyesha pale ni design failure hasa kutatua aina ya udongo na uwepo wa maji, ambapo nadhani tuta la sub base na base course( kwa pamoja huunda road foundation kimantiki) liliwekwa dogo kuliko hali ya udongo korofi wa eneo husika. Kwa hiyo nadhani hapa Hon. Magufuli huwez kumlaumu
 
Mh.Magufuli anatakiwa kujua kwamba Watanzania wa sasa sio wale wa zamani ambao mtu angeweza kuwaburuza atakavyo.Sasa hivi Serikali inaendeshwa kwa misingi ya Utawala Bora.Inashangaza kuona Mh. huyu akitoa majigambo na kumdharau Waziri aliyekuwa ametoa waraka kuruhusu magari yatumiayo barabara zetu kupewa msamaha wa uzito unaofikia asilimia tano ya uzito uliowekwa kisheria.Jambo la kujiuliza ni je,Mh Magufuli kauona lini Waraka huo?Mbona upo tangu mwaka 2006 na yeye amekuwa Waziri wa Wizara hiyo tangu lini?Unafiki wa namna hii ni hatari kwa maendeleo ya nchi hasa pale Serikali inapokuwa na viongozi wa aina ya Mh. Magufuli.Kama kulikuwa na nia nzuri ya kuchukua hatua ya kuufuta huo Waraka Mh. Magufuli alishindwa nini kutoa muda kwa wasafirishaji ili wajue kuwa kuanzia tarehe fulani unafuu uliokuwepo utaondolewa.Viongozi wapenda sifa na wenye majigambo wanawaumiza wananchi kwa maamuzi yao ya kipuuzi na yasiyozingatia busara.Kwamba msafirishaji ambaye gari lake tayari liko njiani atarekebisha vipi mzigo alioubeba kabla ya kufika mizani?Hapo kuna utawala bora?Sasa hivi tayari wananchi wameanza kupata adha ya usafiri kutokana na ubabe wa kiongozi asiye na msimamizi!Mtu huyu anasemekana kuwa anautaka uraisi akiupata nchi hii si itaangamia?
Hafai kupewa kabisa
 
Mh.Magufuli anatakiwa kujua kwamba Watanzania wa sasa sio wale wa zamani ambao mtu angeweza kuwaburuza atakavyo.Sasa hivi Serikali inaendeshwa kwa misingi ya Utawala Bora.Inashangaza kuona Mh. huyu akitoa majigambo na kumdharau Waziri aliyekuwa ametoa waraka kuruhusu magari yatumiayo barabara zetu kupewa msamaha wa uzito unaofikia asilimia tano ya uzito uliowekwa kisheria.Jambo la kujiuliza ni je,Mh Magufuli kauona lini Waraka huo?Mbona upo tangu mwaka 2006 na yeye amekuwa Waziri wa Wizara hiyo tangu lini?Unafiki wa namna hii ni hatari kwa maendeleo ya nchi hasa pale Serikali inapokuwa na viongozi wa aina ya Mh. Magufuli.Kama kulikuwa na nia nzuri ya kuchukua hatua ya kuufuta huo Waraka Mh. Magufuli alishindwa nini kutoa muda kwa wasafirishaji ili wajue kuwa kuanzia tarehe fulani unafuu uliokuwepo utaondolewa.Viongozi wapenda sifa na wenye majigambo wanawaumiza wananchi kwa maamuzi yao ya kipuuzi na yasiyozingatia busara.Kwamba msafirishaji ambaye gari lake tayari liko njiani atarekebisha vipi mzigo alioubeba kabla ya kufika mizani?Hapo kuna utawala bora?Sasa hivi tayari wananchi wameanza kupata adha ya usafiri kutokana na ubabe wa kiongozi asiye na msimamizi!Mtu huyu anasemekana kuwa anautaka uraisi akiupata nchi hii si itaangamia?

Ama kweli wewe ni pepopunda. Kanuni iko wazi kuwa ili usipate pepopunda pata chanjo basi hutapata pepopunda. Ukireta malidhiano utaambiwa chanjo ya pepopunda inapunguza nguvu ya kiume then hutachanjwa.

Taz inahitaji sheria ndio iongoze nchi na si uwezo wa mtu kuwa maarufu kwa maridhiano ya kuvunja sheria. Lowasa alijua kbs Wamasai hakutakiwa kulima ndani ya Ngorongoro CA ila akawaruhusu wamasai walime eti tamko la PM sheria ikapuuzwa. Leo utamwambia nini mwananchi wa mikumi, Serengeti na hifadhi zingine wasilime? Ingekuwa JPM ndo waziri wa Maliasili asingekubali upumbavu ule.

Juzi wananchi wa jimbo la Busega wamemtupa kwenye maoni mh. Kamani (waziri wa mifugo na uvuvi) kwa kushindwa kuwaruhusu wananchi kuchungia hifadhi y Serengeti
 
Magufuli kasimamia sheria tu,tatizo liko wapi,mbona wabongo tunapenda vitu vya njia za mkato tu, huu ni utaratibu usiokubalika kabisaaa......lazima tusimamie utawala wa sheria tulizoweka wenyewe ili nchi iweze kusonga mbele,watu wasiopenda maendeleo ndio wanapotosha umma
 
Magufuli kasimamia sheria tu,tatizo liko wapi,mbona wabongo tunapenda vitu vya njia za mkato tu, huu ni utaratibu usiokubalika kabisaaa......lazima tusimamie utawala wa sheria tulizoweka wenyewe ili nchi iweze kusonga mbele,watu wasiopenda maendeleo ndio wanapotosha umma
 
Kama unaharibu acha sheria ikutafune, kimsingi majina haya ..bongo, dili, papaa, vibopa, wakubwa, vigogo n.k ni majina yaliyotokana na makundi ya baadhi ya watu kuamua kuishi kwa short cuts bila kufata taratiibu, waliamua kuanzisha mfumo wao ambao sheria zilipigwa vita, zilivunjwa na kunyofolewa ili waendelee kulinda himaya zao ..sasa kupitia kwa Magufuri tunasema huu mtindo sasa basi, na wao washalijua na ndo maana wanahaha kuokoa mali zao, sheria zipo na zitafuatwa ili watanzania wanyonge tupumue na kuishi kwa amani
 
Mimi ningeshauri kama John atapita arejeshe kodi ya KICHWA.Watanzania ni wavivu,wambea,wapenda majungu na walalamishı.Jitu linapangiwa kazı Kigoma au Kagera lakini linagoma eti mbali,allah tandika haya.Wachna wapo hapa,kwanı n jiranı na kwao?Magufuli akiweza awe hata dikteta kwa miaka mitano,ondo ujinga ujinga wa ovyo.Mıjitu imesomea taaluma hata hawajazifanyia kazi,inakimbilia ubunge,allah!
 
UBABE WA NINI? UONGOZI BORA UNAHITAJI BUSARA NA AKILI,mambo ya kibaabe mara kupiga push up yanini? LOWASSA ndiye tutakayempigia kura.
 
Back
Top Bottom