ulimwengu huu wa sasa sio kama ule wa zamani. kwasasaivi wazungu wanatuhitaji sana na tumeingiliana kibiashara kiasi kwamba nao wanaweza kuadhibiwa vilevile. and due to the rise of china, wana hofu sana, ndio maana rais wa china alipotembelea tu tanzania, marais wa marekani walikuja watatu (obama, bush, clinton) kwasababu wanajua kuwa tukiamua kuwatupa watakosa kitu fulani toka kwetu na ukanda huu. kwa miaka ya siku hizi, adhabu pekee watakayoweza kuifanya ni kutugombanisha sisi wa sisi wawapatie waasi silaha ili tupigane, ila mambo mengine hawawezi nakuapia.
migodini wanajibembeleza toka kwetu, gas tuliyogundua wanajibembeleza toka kwetu, na ukiwa na rais ambaye ni msafi na mchapa kazi, wanakosa hata sababu ya kukushughulikia. enzi za nyerere sio enzi hizi za kwetu. funguka.
hakuna mtu anayeweza kuamuru wafanyabiashara washushe mzigo mombasa badala ya dsm kwa bidhaa kadhaa. ujue bidhaa nyingi zinatoka bara asia kama china, singapore, japan etc, hivyo kama wamagaribi watapiga marufuku meli zao kutua dsm, basi kwa bidhaa za burundi, congo, zambia, malawi na tz yenyewe wachina wataingiza meli zao za biashara, wa singapore na wengine na tutaishi tu, na wao watapata hasara kwa kuwa na wateja wachache kwenye hizo meli zao. usiwe na hofo na kutokujiamini kiasi hicho.