Blackafrica
Senior Member
- Jun 26, 2021
- 140
- 401
Hata siku moja huwezi kupendwa na watu wote, hii ndio hulka ya wanadamu, inasikitisha sana kuona sasa Magufuli amekosa kabisa watetezi, wale waliokuwa hawampendi na kumchukia, kwa sasa wanajiachia watakavyo kumsema vibaya watakavyo hata mazuri aliyofanya hayaonekani bali ni kumkebehi kumtukana na kumsema vibaya.
Nina Hakika hata angekuwa hai leo, wasingekosekana wa kumsema na kumshtumu vibaya, tofauti ya sasa ambapo huyu mtu hatupo naye kimwili tena ni kwamba hata wale watetezi wake waliokuwa Wanamkubali wamegawanyika wengine wamekaa kimya hawamtetei wala kuwa upande wake, wengine Wanahuzunika na hawaamini kama kweli jembe hayupo na mambo mengi wakitizama hayaendi au yamekwama, lakini hawana sauti ya kupaza labda ni uoga au maslahi wanayokuwa nayo katika ukimya wao, binadamu ni wanafiki sana naamini angekuwepo Magufuli hai, angepata watetezi wengi sana tena watetezi wa hoja zenye nguvu.
Lakini tukubaliane kuwa watanzania wengi wamekata tamaa haswa watanzania wale wa kipato cha kati na cha chini, ukipita kila mkoa utakutana na maneno angekuwepo Magufuli huu mradi ungeisha au hii Barabara ingekuwa imejengwa tayari au hii hospital ingekuwa imefunguliwa tayari au tungekuwa tumepiga maendeleo makubwa sana, kwahiyo tusizibeze hizi sauti zinazolalamika chini chini na hakika hizi sauti zikifika mahali zikaamua ziseme sauti ya juu ili zisikike, ndio utakuwa mwisho wa watawala kutudanganya, uongo una mwisho wake uongo una ukomo wake.
Tusimbeze sana Magufuli bali tuendeleze mazuri yake aliyoacha, mkiendelea kumbeza, mfahamu kuwa watetezi wake wapo tele na siku wakiamua kutetea haki zao na nchi yao mtatafuta mlango wa kutokea.
Nina Hakika hata angekuwa hai leo, wasingekosekana wa kumsema na kumshtumu vibaya, tofauti ya sasa ambapo huyu mtu hatupo naye kimwili tena ni kwamba hata wale watetezi wake waliokuwa Wanamkubali wamegawanyika wengine wamekaa kimya hawamtetei wala kuwa upande wake, wengine Wanahuzunika na hawaamini kama kweli jembe hayupo na mambo mengi wakitizama hayaendi au yamekwama, lakini hawana sauti ya kupaza labda ni uoga au maslahi wanayokuwa nayo katika ukimya wao, binadamu ni wanafiki sana naamini angekuwepo Magufuli hai, angepata watetezi wengi sana tena watetezi wa hoja zenye nguvu.
Lakini tukubaliane kuwa watanzania wengi wamekata tamaa haswa watanzania wale wa kipato cha kati na cha chini, ukipita kila mkoa utakutana na maneno angekuwepo Magufuli huu mradi ungeisha au hii Barabara ingekuwa imejengwa tayari au hii hospital ingekuwa imefunguliwa tayari au tungekuwa tumepiga maendeleo makubwa sana, kwahiyo tusizibeze hizi sauti zinazolalamika chini chini na hakika hizi sauti zikifika mahali zikaamua ziseme sauti ya juu ili zisikike, ndio utakuwa mwisho wa watawala kutudanganya, uongo una mwisho wake uongo una ukomo wake.
Tusimbeze sana Magufuli bali tuendeleze mazuri yake aliyoacha, mkiendelea kumbeza, mfahamu kuwa watetezi wake wapo tele na siku wakiamua kutetea haki zao na nchi yao mtatafuta mlango wa kutokea.
