Bintiwangara
JF-Expert Member
- Jun 30, 2013
- 551
- 287
MGOMBEA nafasi ya urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, amesema anazijua shida zote za Watanzania hivyo, atasimama imara katika kuzitatua na kuweka wazi kwamba, kwa muda wa miaka 20 aliyokaa Serikalini hakuwahi kushindwa.
Shida ya kwanza ni Laptop kwa Walimu ambayo atahakikisha kila mwalimu awe primary au secondary lazima awe na Laptop.
Shida zingine zilishatatuliwa na Raisi kikwete na Maraisi wengine waliopita, yeye atakachokifanya ni
Kuendeleza tuu., yaani " Sitawaangusha hawa maraisi waliopita" Alisema Dr. J.P. Magufuri.
Dk. Magufuli aliyasema hayo jana, wakati akizungumza na wazee na wanachama wa CCM wa Mkoa wa Dar es Salaam, baada ya mapokezi yaliyofanyika kwa kurudisha fomu ya urais, huku akibainisha kuwa, atashirikiana na mgombea mwenza wake kuhakikisha wanatatua shida za Watanzania.