VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,800
Iwe ameshinda au ameshindwa uchaguzi mkuu wa mwaka huu, mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM Dkt. John P. Magufuli lazima abadilike. Lazima awe mpya. Hawezi tena na kamwe kubaki alivyo. Anapaswa kujirudi; kujitathmini; kujiangalia na kuwaangalia watanzania wake na kujiuliza bila kujiliza: nimekosea wapi na nijirekebisheje? Lazima abadilike. Lazima afanye mambo na aseme maneno kwa namna mpya.
Runinga ya Watanzania imewashwa wakati huu wa kampeni. Inaonesha mambo ya kuogofya: watu wameumizwa na kuguswa na maneno na matendo ya Dkt. Magufuli. Wamevunjiwa nyumba zao; wamedhulumiwa korosho zao; wamevurugiwa uchumi wao; wameporwa ardhi zao; wamevurugiwa mipango yao; wamesimamishiwa maendeleo yao; wameshindwa kutimiza mahitaji yao; wamedhalilishwa kwenye kazi zao; wamedhulumiwa mishahara na marupurupu yao na kadhalika.
Watanzania, kupitia runinga yao ya kwenye kampeni na kwa wingi wao, wameumia na hawatarajii wafanyiwe tena hivyo. Watanzania wanatarajia haki, wajibu na maendeleo kutamalaki kwenye awamu itakayoanza baada ya uchaguzi mkuu huu. Watanzania wanahitaji mabadiliko. Lazima, Dkt. Magufuli abadilike kuendana nao. Lazima utendaji uendane na kusababisha furaha badala ya hasira; utulivu badala ya maumivu; mendeleo badala ya upendeleo.
Watanzania wameshatuma ujumbe wao kwa Dkt. Magufuli. Umemfikia. Wanamsubiria Oktoba 28!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Mbeya, Tanzania)
Runinga ya Watanzania imewashwa wakati huu wa kampeni. Inaonesha mambo ya kuogofya: watu wameumizwa na kuguswa na maneno na matendo ya Dkt. Magufuli. Wamevunjiwa nyumba zao; wamedhulumiwa korosho zao; wamevurugiwa uchumi wao; wameporwa ardhi zao; wamevurugiwa mipango yao; wamesimamishiwa maendeleo yao; wameshindwa kutimiza mahitaji yao; wamedhalilishwa kwenye kazi zao; wamedhulumiwa mishahara na marupurupu yao na kadhalika.
Watanzania, kupitia runinga yao ya kwenye kampeni na kwa wingi wao, wameumia na hawatarajii wafanyiwe tena hivyo. Watanzania wanatarajia haki, wajibu na maendeleo kutamalaki kwenye awamu itakayoanza baada ya uchaguzi mkuu huu. Watanzania wanahitaji mabadiliko. Lazima, Dkt. Magufuli abadilike kuendana nao. Lazima utendaji uendane na kusababisha furaha badala ya hasira; utulivu badala ya maumivu; mendeleo badala ya upendeleo.
Watanzania wameshatuma ujumbe wao kwa Dkt. Magufuli. Umemfikia. Wanamsubiria Oktoba 28!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Mbeya, Tanzania)