MAGUFULI na MWAKYEMBE tubuni dhambi hizi.

MAGUFULI na MWAKYEMBE tubuni dhambi hizi.

YAGHAMBA

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2012
Posts
545
Reaction score
147
Magufuli ulisimamia sera mbovu ya CCM ya kuuza nyumba za umma; Mwakyembe ulificha sehemu muhimu ya ripoti ya Richmond.
 
watanzania tunapenda sana kuangalia nyuma tukiwa tunakimbia,usiangalie umejikwaa wapi kazania kurekebisha ili usijikwae tena, hakuna mwanadamu asiye na madhaifu hata wewe naamini yapo madhaifu yako ,hakuna mkamilifu hata mmoja. hawa mawaziri wawili kwakweli kwa namna moja au nyingine wamejaribu kutimiza dhamana ya uongozi wao licha ya kukwamishwa na watendaji na VIJOGOO wanaotaka vyote kwa faida yao, embu tuangalie ni wizara gani zinajitahidi kutimiza malengo. hebu tujiulize ni miaka mingapi tanzania tunalalmika tatizo la maji na umeme wakati tumezungukwa na mito,maziwa bahari na chemichemi lakini hatuna maji safi.viongozi wanaimba kila siku KILIMO UTI WA MGONGO....AU UTI WA MCHONGO????? manake tunona waziri anatangaza ruzuku zinatolewa kwa wakulima,mara wakulima jiungeni mpewe matrekta hivi mlishawi kusikia mtanzania wa kawaida kafaidika na kilimo kwa kuwezeshwa an serikali.Jamni tuache lawama aliyetenda zuri tumpe sifa yake
 
Nakubaliana na wewe mkuu ila maumivu tunayopata kwa waliyotufanyia ni makubwa ndo maana nasema watubu na watasamehewa.
 
Makubwaaaaa....kweli kila lenye zuri halikosi kasoro.
 
Mwakyembe alificha ripoti kwa maslahi ya chama chake.Kosa hilo limeendelea kuligharimu taifa.Watanzania hatuna rekodi ya ku-apologize

Magufuli alisimamia sera mbovu na pia alikandamiza wavuvi kwa kukamata nyavu zao badala ya kufunga viwanda vinavyotengeneza zana hizo na kizuia zile zinazotoka nje

Kufanya mazuri hakufuti mabaya.Mazuri ndiyo wajibu wake ndiyo maana anatafuta ridhaa ila makosa ya kizembe ndiyo yaliyolifikisha taifa hapa yakifanywa na wasomi waliobobea kwa kulenga narrow interests
 
  • Thanks
Reactions: Ame
wacheni watu wafanye kazi...hata we mtoa mada una mambo mabaya mengi tu unayo kwa hiyo usiangalie ya wenzako..fanyeni kazi watz wacheni ufitna na wivu
 
Mwakyembe alificha ripoti kwa maslahi ya chama chake.Kosa hilo limeendelea kuligharimu taifa.Watanzania hatuna rekodi ya ku-apologize

Magufuli alisimamia sera mbovu na pia alikandamiza wavuvi kwa kukamata nyavu zao badala ya kufunga viwanda vinavyotengeneza zana hizo na kizuia zile zinazotoka nje

Kufanya mazuri hakufuti mabaya.Mazuri ndiyo wajibu wake ndiyo maana anatafuta ridhaa ila makosa ya kizembe ndiyo yaliyolifikisha taifa hapa yakifanywa na wasomi waliobobea kwa kulenga narrow interests

Waziri wa Viwanda na Biashara alikuwa ana kazi gani? Magufuli akiwa waziri mwenye dhamana na uvuvi alizuia kile ambacho allikuwa na madaraka nacho.
 
I can't beleive Tanzaniana are such selfish, always thinikng about themsleves. Hao watu maelfu ambao hata jamii forum hawaijui wamepewa usafiri wa uhakika nyie mwapiga kelele. That what mabadiliko and people want maisha kuwa bora that what mapwepande promised to People that what we need to go. Go ahead good Askari's and God Bless U.
 
Magufuli ulisimamia sera mbovu ya CCM ya kuuza nyumba za umma; Mwakyembe ulificha sehemu muhimu ya ripoti ya Richmond.

Ama kweli Mwakyembe ni Kiboko Yao. Linapokuja suala la mabehewa mabovu ya TRL, Mwakyembe anashutumiwa peke yake bila kumhusisha aliyekuwa Naibu Waziri wake, Tizeba. Linapokuja suala la taarifa ya CAG kuhusu Wizara ya Ujenzi, Magufuli anatuhumiwa pamoja na aliyekuwa Naibu Waziri wake, Mwakyembe! Ama kweli Mwakyembe ni Kiboko Yao! Yote tisa, kumi ni Richmond Bwana, hoja iliyomng'oa PM na Baraza zima la Mawaziri madarakani! Yaghamba anasema Mwakyembe alificha sehemu muhimu ya ripoti ya Richmond. Naendelea kumpongeza sana Mwakyembe kwa weledi wake katika sheria na mbinu aliyotumia kuficha sehemu ya ushahidi ili kumpa Lowassa tumbo joto. Lowassa angediriki kubisha tu, Mwakyembe na timu yake wangemkabili na ushahidi huo wa akiba ambao mbumbumbu wote wa sheria wana-question maana yake. Bravo Mwakyembe! Ripoti yako ya Richmond inatosha kumtunukia mtu stashahada ya sheria!
 
Mwakyembe alificha ripoti kwa maslahi ya chama chake.Kosa hilo limeendelea kuligharimu taifa.Watanzania hatuna rekodi ya ku-apologize

Magufuli alisimamia sera mbovu na pia alikandamiza wavuvi kwa kukamata nyavu zao badala ya kufunga viwanda vinavyotengeneza zana hizo na kizuia zile zinazotoka nje

Kufanya mazuri hakufuti mabaya.Mazuri ndiyo wajibu wake ndiyo maana anatafuta ridhaa ila makosa ya kizembe ndiyo yaliyolifikisha taifa hapa yakifanywa na wasomi waliobobea kwa kulenga narrow interests

Tatizo hapa ni Ben Saanane - hajawahi kuisoma Taarifa ya Richmond! Pili, Ben Saanane si mwanasheria kujua sanaa ya uwasilishaji taarifa. Mimi nimeisoma yote na nimefurahia staili ya uwasilishaji aliyoitumia Mwakyembe - ya kuficha ushahidi nyeti kwa matarajio kuwa Lowassa angeamua kuikataa taarifa na kudai ushahidi! Hapo sasa viporo vyote vya ushahidi vingetolewa! Staili hiyo ilimwogopesha Lowassa, akaamua kujiuzulu bila kujitetea!
 
Back
Top Bottom