Magufuli, Mwakyembe Watunishiana Misuli

Mkuu, kuna Ukweli na upotoshaji fulani ulivyorejesha, alichosema Magufuli ni kuwa kandarasi huyo atakapoanza Kazi barabara itafungwa lakini Kwa sasa huwezi funga Kwa vile hakuna kitu kilichofanyika kama ilivyokuwa inasadikika!

My take: Imekuwaje Mkandarasi huyo kalipwa boll join nane wakati hajazalisha kitu?? Navyojua ukifanya Kazi unaandaa certificate kuomba fedha against progress/production - sasa huyu imekaaje??? Hii ndo bongo land!
 
Mkuu, kuna Ukweli na upotoshaji fulani ulivyorejesha, alichosema Magufuli ni kuwa kandarasi huyo atakapoanza Kazi barabara itafungwa lakini Kwa sasa huwezi funga Kwa vile hakuna kitu kilichofanyika kama ilivyokuwa inasadikika!

My take: Imekuwaje Mkandarasi huyo kalipwa boll join nane wakati hajazalisha kitu?? Navyojua ukifanya Kazi unaandaa certificate kuomba fedha against progress/production - sasa huyu imekaaje??? Hii ndo bongo land!

Nashukuru kwa correction Mkuu. Ila sasa, kwa nini Mwakyembe naye anasema anataka kugombana na Magufuli kwa swala hilo? Naona hawa watu wanatofautiana katika maelezo yao
 
Wanajamii,

Nimeshangazwa na taarifa ya Star TV ikimuonyesha Dk. Magufuli akitoa msimamo wake juu ya amri ya kufungwa kwa barabara inayodaiwa kuzuia ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Mwanza. Kwa maelezo yake Magufuli, uwanja huo si kikwazo kama ilivyoelezwa na mkandarasi, maana hata upembuzi yakinifu wa ujenzi wa uwanja huo, hadi sasa ni asilimia thelathini na tano (35%) tu na imeshachelewa miezi minne zaidi. Magufuli ameiagiza wizara ya Uchukuzi imbane mkandarasi na si kuagiza barabara ifungwe.

Wakati huohuo, siku Waziri wa Uchukuzi alizoipa Wizara ya Ujenzi kuifunga barabara hiyo zimebakia nne tu. Dk. Harrison Mwakyembe ametoa kauli yake kuwa kesho itabidi tu agombane kabisa na Dk. Magufuli kwa ajili ya swala hilo.

Wanajamii, hii serikali inatupeleka wapi ikiwa wizara mbili za serikali moja zinatunishiana misuli na kuoneshana ubabe? Kweli kwa misingi hii tutayapata maendeleo?

Nawasilisha

Acha upotoshaji Ukweli ni huu:
1.Mkandarasi kasaini contract June 2012 (miezi nane tayari) mobilisation zero au suturing or 0%
2.Mhandisi Mshauri kutoka Gambia kakiri mbele ya Waziri Magufuli kuwa Mkandarasi hajafanya kitu tangu apewe mradi!
3.Magufuli kajionea Kwa macho yake pale uwanja Wa ndege Mwanza hata jembe la kupalilia site halipo?
4. Tayari Magufuli keshapata njia mbadala ambayo inatokea Nyakato kupitia Buswelu itakayotumika pindi hii ya airport itakapofungwa ( zote hizi jitihada kumaliza tatitizo)
5. Juzi Tabora Magufuli na Mwakyembe wameonekana wakiwa pamoja na raisi na hawana mgogoro wowote na ikumbukwe wamewahi fanya Kazi Pamoja hivyo wanajua wanachokifanya!
6. Ifike sehemu tuache uchonganishi Wa kihuni, tuwape moyo japo hawa wanaonyesha kufanya Kazi na segment kubwa ya watanzania inawakubali
 
kweli mkuu. mambo mengine humu ni umbeya kwa kwenda mbele. Sometimes mtu anaanzisha tu uzushi ili aonekane naye kapost. huu ni uchonganishi na uhuni humu jf.
 
Nashukuru kwa correction Mkuu. Ila sasa, kwa nini Mwakyembe naye anasema anataka kugombana na Magufuli kwa swala hilo? Naona hawa watu wanatofautiana katika maelezo yao

Mkuu Lubua kwanza nashukuru unakubali Ukweli pengine naomba nikupe nyongeza:
1. Waziri Wa Ujenzi ( Dr. Magufuli) kupitia sheria namba 13 ya mwaka 2007 kifungu namba 11(1) Pamoja na kifungu namba 12 na 13 vya sheria hiyo hiyo vimempa mamlaka ya kufunga barabara na Kwa bahati nzuri amevitaja kwenye mkutano jana (nashangaa Kwa nini vyombo vya habari waliskip hiyo)
2. Katika mkutano huo Dr. Magufuli aliambatana na Katibu Mkuu Wizara ya uchukuzi akiwa na wakurugenzi wake,Mkuu Wa Mkoa Wa Mwanza Mh .Eng Evaristi Ndikilo, wakuu Wa Wilaya Za Nyamagana na Ilemela,Mama Ngimbwa(Mwenyekiti Bodi ya usajili Makandarasi),Professor Ninatubu Lema(Mwenyekiti Wa Bodi ya Usajili Wa Wahandisi),Eng. Mfugale ( Chief Executive TANROADS), Eng. Nyamuhanga ( Mkurugenzi Wa Barabara, Wizara ya Ujenzi),Kamati ya Ulinzi ya Mkoa Wa Mwanza, Meya Wa jiji la Mwanza, Eng.Magesa (Chief Executive Wa TEMESA)na Dr.Ambwene Mwakyusa (Architects and Quantity Surveyors Registration Board, AQSRB)
3.Hao wote nilowataja ni mashahidi Wa tukio zima la kutembelea uwanja huo, nakuhakikishia hata jembe halijakutwa/halipo site
4. Magufuli kaziagiza Bodi zote zinahusiana na civil works kumbana Mkandarasi huyo ili kuhakikisha thamani ya fedha unapatikana (Value for Money)
5. Mkandarasi alipewa nafasi kujiekeza na kama kawaida visingizio ooh vifaa bado vipo Zanzibar , imagine 8 months since contract isainiwe vifaa bado vipo Zanzibar, haingii akilini hata kidogo
6.Lakini pia ili kudhibiti uzushi na uongo humu JF siku mbili zijazo nitatoa clips ili kutujuza umma yaliyojiri ktk mkutano huo Wa Waziri wa Ujenzi
7.Naomba Kwa mara nyingine ieleweke Magufuli na Mwakyembe hawa ni marafiki, kumbuka Bajeti ya kwanza ya Mwakyembe bungeni mwaka jana alikili kufundishwa Kazi na Magufuli nanukuu maneno yake" Magufuli alinifundisha kuwa zege huwa halilali..."
8.Namsihi Mwakyembe akutumie sana Magufuli kama Mwalimu wake ktk Kazi kwa vile bado ana mwendo mrefu wa kujifunza na kasi aliyonayo ni matunda ya Magufuli . Aachane na wachonganishi!

Nakupenda Tanzania wangu!
 
Nashukuru kwa correction Mkuu. Ila sasa, kwa nini Mwakyembe naye anasema anataka kugombana na Magufuli kwa swala hilo? Naona hawa watu wanatofautiana katika maelezo yao

Haujachanganya taarifa hapo mkuu?
Suala la kesho kugombana na magufuli lilisemwa na Mwakyembe katika ujenzi wa reli itakayowezesha usafirishaji wa madini ya nikotin kutoka Burundi ambapo alisema

kutokana na uzito wa mizigo hiyo haiwezi kusafirishwa kwa barabara vinginevyo itakapoanza kusafirishwa KESHO yake tu tutagombana na Magufuli
 
Acha upotoshaji Ukweli ni huu:
1.Mkandarasi kasaini contract June 2012 (miezi nane tayari) mobilisation zero au suturing or 0%
2.Mhandisi Mshauri kutoka Gambia kakiri mbele ya Waziri Magufuli kuwa Mkandarasi hajafanya kitu tangu apewe mradi!
3.Magufuli kajionea Kwa macho yake pale uwanja Wa ndege Mwanza hata jembe la kupalilia site halipo?
4. Tayari Magufuli keshapata njia mbadala ambayo inatokea Nyakato kupitia Buswelu itakayotumika pindi hii ya airport itakapofungwa ( zote hizi jitihada kumaliza tatitizo)
5. Juzi Tabora Magufuli na Mwakyembe wameonekana wakiwa pamoja na raisi na hawana mgogoro wowote na ikumbukwe wamewahi fanya Kazi Pamoja hivyo wanajua wanachokifanya!
6. Ifike sehemu tuache uchonganishi Wa kihuni, tuwape moyo japo hawa wanaonyesha kufanya Kazi na segment kubwa ya watanzania inawakubali

Mkuu,

Naona unapambana na ukuta.

Kuna watu hapa hawapendi hata kile kidogo kinachofanywa na viongozi ambao wako kwa mkono wa CCM. usikae ukafikili kama hii kasi nzuri ya utendaji wa hawa mawaziri inafurahisha kila mmoja.

Katika Tanzania maneno Utaifa na Uzalendo yameanza kuwa ni msamiati. Neno Ubinafsi ndilo linashika kasi katika jamii.

Like it or not. Hii ndiyo hali halisi.
 
Acha upotoshaji Ukweli ni huu:
1.Mkandarasi kasaini contract June 2012 (miezi nane tayari) mobilisation zero au suturing or 0%
2.Mhandisi Mshauri kutoka Gambia kakiri mbele ya Waziri Magufuli kuwa Mkandarasi hajafanya kitu tangu apewe mradi!
3.Magufuli kajionea Kwa macho yake pale uwanja Wa ndege Mwanza hata jembe la kupalilia site halipo?
4. Tayari Magufuli keshapata njia mbadala ambayo inatokea Nyakato kupitia Buswelu itakayotumika pindi hii ya airport itakapofungwa ( zote hizi jitihada kumaliza tatitizo)
5. Juzi Tabora Magufuli na Mwakyembe wameonekana wakiwa pamoja na raisi na hawana mgogoro wowote na ikumbukwe wamewahi fanya Kazi Pamoja hivyo wanajua wanachokifanya!
6. Ifike sehemu tuache uchonganishi Wa kihuni, tuwape moyo japo hawa wanaonyesha kufanya Kazi na segment kubwa ya watanzania inawakubal
i
Asante mkuu kwa uchambuzi makini.

Inaelekea mtoa mada si mchonganishi tu, bali ni kati ya watu wasioitakia nchi hii mema.
Katika kila jambo wao wanaingiza roho mbaya na FITINA.
Roho hizo zitawaumiza wenyewe kwa msaada wa Mungu.
 
A word to a wise person,is enough-naamini mtoa hoja utakuwa umejifunza ,siku nyingine,hata kama unataka kuweka uwongo wako hapa,au kupandikiza chuki zako kwa watu,jipange vizuri-shame on you!!!
 
Hii nimeipenda, JF ingekuwa hivi siku zote haa ingekuwa poa. Kuna watu wamefanya JF sehemu ya majungu, kuchonganisha watu, mfano ni huyu mwanzisha mada. Mmwanachama au kiongozi toka ccm akifanya vizuri anastahili kupongezwa na kutiwa moyo na sio kumletea majungu kisa yupo ccm,na mwanachama au kiongozi wa chadema akikosea anastahili kukosolewa ili siku nyingine asirudie!
 
Back
Top Bottom