Magufuli - Mbunge Machemuri muongo

MAFILILI

JF-Expert Member
Apr 28, 2011
2,377
1,194
WAZIRI wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, amemtaka Mbunge wa Ukerewe, Salvatory Machemuri (Chadema) kuacha tabia ya kudanganya wananchi wa jimbo lake kwamba mradi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami unaotekelezwa wilayani humo ni wake.

Amesema mbunge huyo anapaswa kuwaambia ukweli wananchi kwamba huo ni mradi wa Serikali inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Dk. Magufuli aliyasema hayo juzi wilayani hapa kwenye uzinduzi wa kivuko kipya cha mv Ujenzi, uliofanyika Kijiji cha Kisorya, ambapo pia Machemuri alikuwa ni kati ya wabunge waliohudhuria uzinduzi huo.

Wabunge wengine walikuwa ni Mbunge wa Viti Maalumu, Rosemary Kirigini (CCM), Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugora (CCM) na Mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (Chadema).

Dk. Magufuli alisema mbunge huyo wa Ukerewe amekuwa akipotosha wananchi wa jimbo hilo kwamba mradi huo ameuleta yeye na kwamba ni wake, hivyo kumtaka aache mara moja tabia hiyo, kwani si mradi wake, bali ni wa Serikali inayoongozwa na CCM, chini ya Rais Jakaya Kikwete.

Alisema atapanga ziara ya kwenda wilayani Ukerewe ili awaambie ukweli wananchi kwamba mradi huo unatekelezwa na Serikali na si mali ya mtu ye yote, bali ni mpango wa Serikali na hivyo wasikubali kupotoshwa na mbunge wao anayetaka umaarufu wa haraka kupitia mradi huo.

“Serikali ya Rais Jakaya Kikwete inatekeleza mradi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami katika Wilaya ya Ukerewe, lakini ninasikia mheshimiwa Machemuri, anasema mradi huo ni wake ndiye aliyeuleta.

Nitapanga niende huko Ukerewe niwaambie wananchi kwamba si mradi wake, bali ni wa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi,” alisisitiza Dk. Magufuli.

Aliwataka viongozi wa vyama vya upinzani kuwaambia ukweli wananchi wao kuwa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao ni sera ya CCM, kwani iko ndani ya Ilani ya Uchaguzi ya chama hicho.

Alisema ujenzi wa barabara ya Nyamuswa, Bunda, Kisorya hadi Ukerewe mkoani Mwanza, kwa kiwango cha lami, tayari umeanza kutekelezwa katika hatua ya kwanza ambayo ni ya upimaji na kwamba kabla ya mwaka 2015 wananchi wataona mkandarasi anajenga barabara hiyo.

Source: gazeti la Habari Leo, December 19, 2011.

BIG UP MHESHIMIWA Magufuli kwa kuwapa ukweli watanzania kukusu utekelezaji wa sera za CCM
 
Unashangaa hilo mbona ccm hakuna mkweli wala mwaminifu hata kwenye ndoa zao nadhani wako hivyo hivyo
 
ni mradi wa cdm (machemuri).....serikali imeajiriwa tu na cdm. majimbo yote ambayo kuna vyama vya upinzani kumechangamka na kuna maendeleo coz of upinzani. kama huamini njoo tanga ucheki mambo yalivyoovyo coz of ccm.

kwani hakuna hata jimbo moja la upinzani. matokeo yake viwanda vingi vimekufa, na cha kusikitisha zaidi ni kiwanda cha unga cha pembe ambacho watu wengi walipata ajira.

pale lakini kimizengwezengwe kimefungwa.....kwa nini? hatuna serikali inayojali maisha ya wananchi wake.
 
Maskini Ukerewe! kumbe mradi wenyewe mpaka 2015? tumeliwa! hapo tuhesabu maumivu tu.
 
Ah! na kuchelewesha mishahara ya watumishi ili waendelee kuadhirika nazo ni sera nzuri! wabongo wake up and perish this nonsense sentences. huo ukweli anaoenda kusema huko ukerewe ni upi! sio kodi zetu hizo hizo zinazojenga barabara ndio posho za huyo hayawani! aache unafiki wake pesa za barabara , hizo wanazogombea kama posho si za CCM ni zetu watz. Nawe mleta huu uzi kichwa chako kipo masaburi masaburi tu
 
Toka Magufuli aanze kujiingiza kwenye siasa za kijinga na uongo akiwa Igunga naona sasa anapoteza mwelekeo
 
ni wa mbunge cdm kwa kuwa unafanyika katika himaya yake, yeye ndo msimamizi wa kuhakikisha unafanikiwa. kutoa mpesa ni suala moja, lakini utekelezaji ni suala lingine.

hata hivyo, pesa zote ni za wananchi, c za ccm wala cdm, lakini ccm wameziiba kwa mda mrefu huku wakitutuliza kwa utekelezaji wa miradi midogomidogo
 
Kwako Magufuli:-
Kama huo ni mradi wa ccm. mbona kuporomoka kwa uchumi husemi kuwa kumesababishwa na ccm?
 
Ukweli ni kwamba hiyo ni hongo ya CCM kupitia kodi zetu ili Wakerewe 2015 wamurudishe mbunge wa CCM.
BTW, hivi ahadi ya JK ilikuwa moja tu Ukerewe? Machemuri ndaa orodha ya ahadi zote alizozitoa JK UK
halafu amukabidhi Magufuri azisome mbele ya wakerewe akishindwa wewe fanya hivyo.
 
WAZIRI wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, amemtaka Mbunge wa Ukerewe, Salvatory Machemuri (Chadema) kuacha tabia ya kudanganya wananchi wa jimbo lake kwamba mradi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami unaotekelezwa wilayani humo ni wake.

Amesema mbunge huyo anapaswa kuwaambia ukweli wananchi kwamba huo ni mradi wa Serikali inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Dk. Magufuli aliyasema hayo juzi wilayani hapa kwenye uzinduzi wa kivuko kipya cha mv Ujenzi, uliofanyika Kijiji cha Kisorya, ambapo pia Machemuri alikuwa ni kati ya wabunge waliohudhuria uzinduzi huo.

Wabunge wengine walikuwa ni Mbunge wa Viti Maalumu, Rosemary Kirigini (CCM), Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugora (CCM) na Mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (Chadema).

Dk. Magufuli alisema mbunge huyo wa Ukerewe amekuwa akipotosha wananchi wa jimbo hilo kwamba mradi huo ameuleta yeye na kwamba ni wake, hivyo kumtaka aache mara moja tabia hiyo, kwani si mradi wake, bali ni wa Serikali inayoongozwa na CCM, chini ya Rais Jakaya Kikwete.

Alisema atapanga ziara ya kwenda wilayani Ukerewe ili awaambie ukweli wananchi kwamba mradi huo unatekelezwa na Serikali na si mali ya mtu ye yote, bali ni mpango wa Serikali na hivyo wasikubali kupotoshwa na mbunge wao anayetaka umaarufu wa haraka kupitia mradi huo.

"Serikali ya Rais Jakaya Kikwete inatekeleza mradi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami katika Wilaya ya Ukerewe, lakini ninasikia mheshimiwa Machemuri, anasema mradi huo ni wake ndiye aliyeuleta.

Nitapanga niende huko Ukerewe niwaambie wananchi kwamba si mradi wake, bali ni wa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi," alisisitiza Dk. Magufuli.

Aliwataka viongozi wa vyama vya upinzani kuwaambia ukweli wananchi wao kuwa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao ni sera ya CCM, kwani iko ndani ya Ilani ya Uchaguzi ya chama hicho.

Alisema ujenzi wa barabara ya Nyamuswa, Bunda, Kisorya hadi Ukerewe mkoani Mwanza, kwa kiwango cha lami, tayari umeanza kutekelezwa katika hatua ya kwanza ambayo ni ya upimaji na kwamba kabla ya mwaka 2015 wananchi wataona mkandarasi anajenga barabara hiyo.

Source: gazeti la Habari Leo, December 19, 2011.

BIG UP MHESHIMIWA Magufuli kwa kuwapa ukweli watanzania kukusu utekelezaji wa sera za CCM
Mbunge ana nafasi kubwa katika jimbo lake kumbe ni mradi wake huo wala hakuna ubishi ila kauleta nani ni jambo lingine maana huduma muhimu kwa jamii hazibebi chama bali kodi yetu wananchi wote na hata Serikali iliyopo ni yetu wote, ni lazima watofautishe Chama na Serikali ingawa wanasema Serikali ya Chama cha Mpainduzi, si kweli ni Serikali ya Tanzania.
 
Huyu Magufuli sijui ana matatizo gani! au nadhani kile kikombe cha babu lioliondo kilimu overdose...
Hajui kutofautisha shughuli za kiserikali na shughuli za kichama...ndio maana ataiponza CCM igunga...kwani
CDM wanaweza kushinda kesi kutokana na kidomo domo cha Magufuli katika kampeni Igunga kuhusisha shughuli za kiserikali na mambo ya kichama

Vile vile huo mradi...ni wake machemli...kwani kazi yake ni kuusimamia na aliwaahidi wapiga kura wake wa ukerewe...,bila yeye pesa zinaweza kuliwa na watendaji..
Kwahiyo ni haki yake kujidai ni mradi ni wake..

Namshauri tu magufuli..naona ana tamani sana kupambana na CHADEMA..namshauri ajivue gamba agombee tena ubunge ili apambane na chadema! naona anapenda sana mapambano nao
 
Hivi kumbe hii miradi inaendelea kwa feadha za walipa kodi ina ownership ya vyama au mtu binafsi?. Mi nilidhani ni miradi inayofanywa kwa ajili ya watanzania ikisimamiwa na serikali ya watanzania regardless chama gani kinaongoza serikali hiyo. Kwa style hii ya mawazo kama ya kina maghfuli sasa nimeamini kwa nini Tanzania tunasuasua. Yaani kila kitu siasa mbele. Hakuna mbunge wala waziri yeyote anyeweza kujilimikisha mradi isipokuwa tu kupata credit kwa ushawishi na utekelezaji wa mradi. Maghufuli jenga barabara mambo yakiwa sawa wananchi wenye wataamua katika sanduku la kura.
 
.

Amesema mbunge huyo anapaswa kuwaambia ukweli wananchi kwamba huo ni mradi wa Serikali inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Dk. Magufuli aliyasema hayo juzi wilayani hapa kwenye uzinduzi wa kivuko kipya cha mv Ujenzi, uliofanyika Kijiji cha Kisorya, ambapo pia Machemuri alikuwa ni kati ya wabunge waliohudhuria uzinduzi huo.

Wabunge wengine walikuwa ni Mbunge wa Viti Maalumu, Rosemary Kirigini (CCM), Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugora (CCM) na Mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (Chadema).

Dk. Magufuli alisema mbunge huyo wa Ukerewe amekuwa akipotosha wananchi wa jimbo hilo kwamba mradi huo ameuleta yeye na kwamba ni wake, hivyo kumtaka aache mara moja tabia hiyo, kwani si mradi wake, bali ni wa Serikali inayoongozwa na CCM, chini ya Rais Jakaya Kikwete.

Alisema atapanga ziara ya kwenda wilayani Ukerewe ili awaambie ukweli wananchi kwamba mradi huo unatekelezwa na Serikali na si mali ya mtu ye yote, bali ni mpango wa Serikali na hivyo wasikubali kupotoshwa na mbunge wao anayetaka umaarufu wa haraka kupitia mradi huo.

“Serikali ya Rais Jakaya Kikwete inatekeleza mradi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami katika Wilaya ya Ukerewe, lakini ninasikia mheshimiwa Machemuri, anasema mradi huo ni wake ndiye aliyeuleta.

Nitapanga niende huko Ukerewe niwaambie wananchi kwamba si mradi wake, bali ni wa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi,” alisisitiza Dk. Magufuli.

Aliwataka viongozi wa vyama vya upinzani kuwaambia ukweli wananchi



Mbona yeye si Mkweli hadi kwa Mkewe
Mbona yeye si Mkweli kwa watanzania , alimptatia hawara wake Nyumba tena akiwa mwanafunzi wa chuo kikuu na hajawahi kufanya kazi serikalini hata kidogo. Yaani Magufuli na uzeee wake wote anatembea na Sundi ambaye anafaa kuwa mwanae wa kumzaa kabisa
 
Na kuhusu ile Ilani ya CCM ya kutujengea barabara za juu huku Dar ameuzungumzia au ile ilikuwa ni Ilani ya Chadema?
 
mwambieni maku lock aache ujinga mradi ni wetu wote tunalipa kodi....msimamizi mwakilishi wa wananchi ni mbunge ,,,labda kipara kinapunguza uwezo wa kufikiri nawe ulieleta hii weka picha yako labda na wewe una bold
 
Maskini Ukerewe! kumbe mradi wenyewe mpaka 2015? tumeliwa! hapo tuhesabu maumivu tu.


Nilijua tu hili jina ni la kule. BTW kwani chama tawala kinajenga barabara kwa kutmia hela za chama au wanachi wote??? kwa hiyo hao wananchi hawana hata uhuru wa kusema barabara hii ni ya kwetu bali wanatakiwa kusema ni ya ccm siyo. Shame on you magufuli.
 
Back
Top Bottom