MAFILILI
JF-Expert Member
- Apr 28, 2011
- 2,377
- 1,194
WAZIRI wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, amemtaka Mbunge wa Ukerewe, Salvatory Machemuri (Chadema) kuacha tabia ya kudanganya wananchi wa jimbo lake kwamba mradi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami unaotekelezwa wilayani humo ni wake.
Amesema mbunge huyo anapaswa kuwaambia ukweli wananchi kwamba huo ni mradi wa Serikali inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Dk. Magufuli aliyasema hayo juzi wilayani hapa kwenye uzinduzi wa kivuko kipya cha mv Ujenzi, uliofanyika Kijiji cha Kisorya, ambapo pia Machemuri alikuwa ni kati ya wabunge waliohudhuria uzinduzi huo.
Wabunge wengine walikuwa ni Mbunge wa Viti Maalumu, Rosemary Kirigini (CCM), Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugora (CCM) na Mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (Chadema).
Dk. Magufuli alisema mbunge huyo wa Ukerewe amekuwa akipotosha wananchi wa jimbo hilo kwamba mradi huo ameuleta yeye na kwamba ni wake, hivyo kumtaka aache mara moja tabia hiyo, kwani si mradi wake, bali ni wa Serikali inayoongozwa na CCM, chini ya Rais Jakaya Kikwete.
Alisema atapanga ziara ya kwenda wilayani Ukerewe ili awaambie ukweli wananchi kwamba mradi huo unatekelezwa na Serikali na si mali ya mtu ye yote, bali ni mpango wa Serikali na hivyo wasikubali kupotoshwa na mbunge wao anayetaka umaarufu wa haraka kupitia mradi huo.
Serikali ya Rais Jakaya Kikwete inatekeleza mradi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami katika Wilaya ya Ukerewe, lakini ninasikia mheshimiwa Machemuri, anasema mradi huo ni wake ndiye aliyeuleta.
Nitapanga niende huko Ukerewe niwaambie wananchi kwamba si mradi wake, bali ni wa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi, alisisitiza Dk. Magufuli.
Aliwataka viongozi wa vyama vya upinzani kuwaambia ukweli wananchi wao kuwa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao ni sera ya CCM, kwani iko ndani ya Ilani ya Uchaguzi ya chama hicho.
Alisema ujenzi wa barabara ya Nyamuswa, Bunda, Kisorya hadi Ukerewe mkoani Mwanza, kwa kiwango cha lami, tayari umeanza kutekelezwa katika hatua ya kwanza ambayo ni ya upimaji na kwamba kabla ya mwaka 2015 wananchi wataona mkandarasi anajenga barabara hiyo.
Source: gazeti la Habari Leo, December 19, 2011.
BIG UP MHESHIMIWA Magufuli kwa kuwapa ukweli watanzania kukusu utekelezaji wa sera za CCM
Amesema mbunge huyo anapaswa kuwaambia ukweli wananchi kwamba huo ni mradi wa Serikali inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Dk. Magufuli aliyasema hayo juzi wilayani hapa kwenye uzinduzi wa kivuko kipya cha mv Ujenzi, uliofanyika Kijiji cha Kisorya, ambapo pia Machemuri alikuwa ni kati ya wabunge waliohudhuria uzinduzi huo.
Wabunge wengine walikuwa ni Mbunge wa Viti Maalumu, Rosemary Kirigini (CCM), Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugora (CCM) na Mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (Chadema).
Dk. Magufuli alisema mbunge huyo wa Ukerewe amekuwa akipotosha wananchi wa jimbo hilo kwamba mradi huo ameuleta yeye na kwamba ni wake, hivyo kumtaka aache mara moja tabia hiyo, kwani si mradi wake, bali ni wa Serikali inayoongozwa na CCM, chini ya Rais Jakaya Kikwete.
Alisema atapanga ziara ya kwenda wilayani Ukerewe ili awaambie ukweli wananchi kwamba mradi huo unatekelezwa na Serikali na si mali ya mtu ye yote, bali ni mpango wa Serikali na hivyo wasikubali kupotoshwa na mbunge wao anayetaka umaarufu wa haraka kupitia mradi huo.
Serikali ya Rais Jakaya Kikwete inatekeleza mradi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami katika Wilaya ya Ukerewe, lakini ninasikia mheshimiwa Machemuri, anasema mradi huo ni wake ndiye aliyeuleta.
Nitapanga niende huko Ukerewe niwaambie wananchi kwamba si mradi wake, bali ni wa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi, alisisitiza Dk. Magufuli.
Aliwataka viongozi wa vyama vya upinzani kuwaambia ukweli wananchi wao kuwa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao ni sera ya CCM, kwani iko ndani ya Ilani ya Uchaguzi ya chama hicho.
Alisema ujenzi wa barabara ya Nyamuswa, Bunda, Kisorya hadi Ukerewe mkoani Mwanza, kwa kiwango cha lami, tayari umeanza kutekelezwa katika hatua ya kwanza ambayo ni ya upimaji na kwamba kabla ya mwaka 2015 wananchi wataona mkandarasi anajenga barabara hiyo.
Source: gazeti la Habari Leo, December 19, 2011.
BIG UP MHESHIMIWA Magufuli kwa kuwapa ukweli watanzania kukusu utekelezaji wa sera za CCM