NI KATIKA KAKAO CHA UVCCM DAR ES SALAAM JANA
Dk Magufuli alisema baadhi ya wapinzani ni waigizaji wakubwa ambao wamesomea uigizaji na wataufanya Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu kutawaliwa na mbwembwe na maigizo mengi.
Alisema kazi kubwa ya CCM ni kukabiliana na mbwembwe na maigizo hayo ili kuyashinda.
Magufuli alisema CCM siyo watu wa matumaini, bali ni watu wa maendeleo na safari ya uhakika.
Alisema wapinzani wa CCM sasa wameanza kunukuu kila kitu hasa nyimbo za chama.
Aliwaambia vijana hao: Katika mchakato huu na katika uchaguzi wa mwaka huu kuna mbwembwe nyingi, kuna mbinu nyingi na kuna maigizo mengi hasa kwa sababu wako wengine walisomea maagizo. Kwa hiyo tuna wajibu wa pamoja kuyashinda haya maigizo.
source (mwananchi 17 .08. 2015)