Magufuli, kama wabunge wanaopanda Bombadier hawakuelewi,wananchi wanaoziona angani ndio watakuelewa?

Salary Slip

Platinum Member
Apr 3, 2012
49,312
152,112
Raisi Magufuli,kama utaendelea kutoa kipaumbele katika mambo yanayohusu miundombinu tu na kusahau mambo mengine yanayogusa moja kwamoja uchumi na maisha ya watu wako,hakika 2020 unaweza kuja kusema labda watanzania hawa hawana shukrani kwani umwajengea miundombinu na kununa ndege lakini bado wamekukataa.

Kitendo cha waheshimiwa wabunge jana kumshangilia JK ambae hakununua Bombardier lakini ameonekana ni bora zaidi ni ishara tosha kuwa japo wanasafiri na hizo Bombadier, hizo Bombadier kwao si issue muhimu kuliko uchumi wao na wa wananchi wanaowawakilisha.

Pengine swali muhimu unalopaswa kujiuliza ni ikiwa hawa wabunge wanaopanda hizi ndege kwao wanaziona sio issue.Je,wananchi wa kawaida wanaoziona ndege hizi zinapita tu huko hewani na wala hawaoti kuzipanda, 2020 ndio watakuelewa?

Kama wabunge wameonyesha picha hiyo,unadhani hali itakuwaje kwa watumishi wa umma wenye maslahi duni kuliko hayo ya wabunge?

Mfanyabiashara na mkulima je?

Hiyo ya bombardier nimetoa kama mfano tu lakini endelea na miradi mingi ya aina hiyo ukasahau mambo mengine au miradi mingine inayogusa moja kwa moja maisha ya watu na matokeo yake yatajidhihirisha wakati ukifika.
 
Ulichoandika ni uchafu wa Kwenye safina enzi za Nuhu.
Kifupi, kilichofanyika jana bungeni ni unafiki uliokithiri wa baadhi ya watanzania.

Tukio la Jana haliwezi mtikisa Rais Magufuli hata kidogo.
Ni Rais anaejiamini, anatenda kwa weledi na si kwa mihemuko yenu wazandiki.

Hata Kikwete anatambua hilo.
Endelea kujisiliba mavi Yako mwenyewe.
 
Nimwpenda apo Jk alivyojibu waandishi wa hbar kuwa yeye si mbunge hawezi ongea bungeni . Lakini angekuwa yule msukuma mwenzangu mpenda sifa na majifuno angebwabwaja zaidi ya nusu saa. Yan Sijui mlMungu wasukuma alituumba siku gani!!!
 
Ulichoandika ni uchafu wa Kwenye safina enzi za Nuhu.
Kifupi, kilichofanyika jana bungeni ni unafiki uliokithiri wa baadhi ya watanzania.

Tukio la Jana haliwezi mtikisa Rais Magufuli hata kidogo.
Ni Rais anaejiamini, anatenda kwa weledi na si kwa mihemuko yenu wazandiki.

Hata Kikwete anatambua hilo.
Endelea kujisiliba mavi Yako mwenyewe.
Ni wazi umeelewa japo hutaki kukiri ukweli huu.

Endeleeni hivyo hivyo but time will tell.
 
Kazi kwelikweli
hizi mada zingine!!
Hivi lengo nini!!
kupata kick au!!
 
Nimwpenda apo Jk alivyojibu waandishi wa hbar kuwa yeye si mbunge hawezi ongea bungeni . Lakini angekuwa yule msukuma mwenzangu mpenda sifa na majifuno angebwabwaja zaidi ya nusu saa. Yan Sijui mlMungu wasukuma alituumba siku gani!!!
Ulivyo kuwa huna akili
Huyo Ulie mtaja si mbunge!!?
kweli Nchi imejaa vilaza
 
Nimwpenda apo Jk alivyojibu waandishi wa hbar kuwa yeye si mbunge hawezi ongea bungeni . Lakini angekuwa yule msukuma mwenzangu mpenda sifa na majifuno angebwabwaja zaidi ya nusu saa. Yan Sijui mlMungu wasukuma alituumba siku gani!!!
JK aliona mbali na hakutaka iwe tabu hivyo akaamua kupotezea tu.
 
Mkuu huyu Ni Rais MWANAUME anayejiamini.

Uchaguzi kwake sio issue, Tume Ni yake
ref; Mkurugenzi tu(Ni)nakupa gari (VX-V8), nyumba, matibabu(bima) na posho za kutosha achilia mbali mshahara halafu unatangaza mpinzani kashinda", (maneno mengine Ni yangu).. Kwa kauli kama hiyo WHAT DO YOU EXPECT?

Na msipokua Makini atatawala mpaka Mungu atakapomchukua.
 
  • Thanks
Reactions: Mj1
Kila siku mnapewa ushauri, msiandike mambo msiyoelewa mkajidai nyie ni watalaam. Huwezi kujenga uchumi imara kama hakuna miundo mbinu inayokuunganisha wewe (kama nchi) na dunia. Tanzania sio kijiji, inahitaji kufikia nchi nyingine kwa masoko, mitaji na hata watalii. Mambo ya kupigiana vigelegele kama kitchen party hayajengi uchumi na ni upuuzi kuleta hoja kama hizo hapa jukwaani. Halafu sio ndio watu hao hao walikuwa wanaimba 'Dhaifu'?
 
Kila siku mnapewa ushauri, msiandike mambo msiyoelewa mkajidai nyie ni watalaam. Huwezi kujenga uchumi imara kama hakuna miundo mbinu inayokuunganisha wewe (kama nchi) na dunia. Tanzania sio kijiji, inahitaji kufikia nchi nyingine kwa masoko, mitaji na hata watalii. Mambo ya kupigiana vigelegele kama kitchen party hayajengi uchumi na ni upuuzi kuleta hoja kama hizo hapa jukwaani. Halafu sio ndio watu hao hao walikuwa wanaimba 'Dhaifu'?
Lazima u-balancea maana wananchi waliopigiga kiuchumi hiyo miundo mbinu haiwezi kuwasaidia.

Sekta ya benki inatakiwa imaarike ili iweze kutoa mikopo kwa wananchi ili nao sasa waweze kutumia hiyo miundombinu kibiashara kuboresha maisha yao na kukuza uchumi wa Taifa.

Wananchi wanaopoteza ajira za kila siku watatumia vipi miundombinu hiyo kujiletea maendeleo ili hali hawana kipato na wala hawakopesheki tena?

Watumishi wenye mishahara duni huku wengine wakikabiliwa na makato ya asilimia 15 ya mishahara hiyo hata ukiwajengea miundombinu mizuri watakopesheka na benki gani?

Wakishindwa kukopesheka, miundombinu hiyo itawasaidiaje?

Bei ya mazo ya mkulima ikiporomoka, miundombinu ya barabara itakuwa na faida gani kwake?

Haya mambo ni lazima yaende pamoja kwasababu yanategemeana.

Just use common sense.
 
Ulichoandika ni uchafu wa Kwenye safina enzi za Nuhu.
Kifupi, kilichofanyika jana bungeni ni unafiki uliokithiri wa baadhi ya watanzania.

Tukio la Jana haliwezi mtikisa Rais Magufuli hata kidogo.
Ni Rais anaejiamini, anatenda kwa weledi na si kwa mihemuko yenu wazandiki.

Hata Kikwete anatambua hilo.
Endelea kujisiliba mavi Yako mwenyewe.
mkuu umepaniki kunywa maji kidogo utakaa sawa. maana oxgen aipandi kichwani kwako
 
Back
Top Bottom