kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,298
- 12,600
Kwa mtu mwenye akili timamu na msafi anajuwa kile alichokifanya Rais Magufuli na atapenda aendelee tena na tena kufanya hivi ili aone tutaelekea wapi.
Kwa miaka mingi sana Tanzania tulikuwa na marafiki wengi sana, mikopo mingi sana, misaada mingi sana na hata vita tumepigana kusaidia wengine tena bure kabisa, lakini hali yetu kimaendeleo ilizidi kudidimia kila uchao kuliko zile nchi tulizozisaidia.
Sasa hivi shida yetu sio majirani wema, misaada wala mikopo, bali shida yetu kubwa ni ndege, meli, reli, afya, umeme, maji, elimu, utalii, chakula na amani. Tusidanganyane, Hata wazungu waliendelea kwanza kabla ya kuja na demokrasia hii tunayoiona sasa kwao. Wazungu wanafahamu kuwa demokrasia sio rafiki kwa uzalishaji na uchumi, na ndiyo maana walituletea demokrasia kwenye nchi ambazo ni changa ili tubaki masikini milele. Kama China ingeanza na demokrasia wangeshindwa kuwalisha watu wao ambao ni robo ya dunia.
China inawasumbua wazungu sasa hivi kiuchumi kwakuwa waliachana na demokrasia kwanza. Hata Magufuli asingeweza kutenda yote hayo kama kila siku angekuwa anasikia sauti za demokrasia za huyooo, yuhoooo, mchinjeeee, mchinjeeee!!!!
Wazungu wamefika pale kiuchumi kwa kupora kwa hila na kwa kutumia majeshi yao. Sisi majeshi yetu sio ya kupora bali ya ulinzi tu wa wananchi, hayazalishi hata kidogo ukilinganisha na majeshi ya nchi tajiri duniani.
Lazima tumshukuru JPM kwa kupambana na majangiri waliokuwa wanaua tembo, faru, twiga wetu, kupunguza rushwa, kujenga kujenga, kununua, kununua, nk, tusimvunje nguvu mtu kama huyu, kwani hata yeye starehe anazitaka, marafiki anawataka, kusafiri nje ya nchi zilizoendelea walizohangaikia marais wenzie anataka lakini anaona aibu. Marais wanaoona aibu sio wengi, hasa katika nchi zetu hizi.
Tunafahamu kuwa wako watu ambao wamekatishwa mipango yao haramu ya kuwinda, kuchimba, kukata magogo, kuiba, ajira, ufisadi na ukuwadi wa nchi mabeberu; obvious, hawa hawatampa kura Mzee Magufuli, hivyo tutashangaa kusikia Rais Magufuli kapata kura zote kabisa. Lakini wale wapiga kura ambao wanapanda ndege, treni, na magari baada ya Magufuli kuwezesha upatikanaji wake hawa watampa kura, na wale ambao wataona Magufuli kasababisha unafuu wa aina fulani katika upatikanaji wa huduma fulani ambayo haikuwepo kabla hawa pia watampa kura ya NDIYO bila ya kupepesa macho.
Hata wale ambao wanafahamu kuwa hawajapandishwa mishahara yao kwakuwa Magufuli alikuwa anatumia hela nyingi kwa kuboresha miundombinu na huduma ambazo zinahitaji hela nyingi ambazo hatuna, pia hawa watampa kura za ndiyo JPM.
NI wahalifu tu ambao watasita kumpa kura ili warejee vitendo vyao
Haki yake tumpe
Kwa miaka mingi sana Tanzania tulikuwa na marafiki wengi sana, mikopo mingi sana, misaada mingi sana na hata vita tumepigana kusaidia wengine tena bure kabisa, lakini hali yetu kimaendeleo ilizidi kudidimia kila uchao kuliko zile nchi tulizozisaidia.
Sasa hivi shida yetu sio majirani wema, misaada wala mikopo, bali shida yetu kubwa ni ndege, meli, reli, afya, umeme, maji, elimu, utalii, chakula na amani. Tusidanganyane, Hata wazungu waliendelea kwanza kabla ya kuja na demokrasia hii tunayoiona sasa kwao. Wazungu wanafahamu kuwa demokrasia sio rafiki kwa uzalishaji na uchumi, na ndiyo maana walituletea demokrasia kwenye nchi ambazo ni changa ili tubaki masikini milele. Kama China ingeanza na demokrasia wangeshindwa kuwalisha watu wao ambao ni robo ya dunia.
China inawasumbua wazungu sasa hivi kiuchumi kwakuwa waliachana na demokrasia kwanza. Hata Magufuli asingeweza kutenda yote hayo kama kila siku angekuwa anasikia sauti za demokrasia za huyooo, yuhoooo, mchinjeeee, mchinjeeee!!!!
Wazungu wamefika pale kiuchumi kwa kupora kwa hila na kwa kutumia majeshi yao. Sisi majeshi yetu sio ya kupora bali ya ulinzi tu wa wananchi, hayazalishi hata kidogo ukilinganisha na majeshi ya nchi tajiri duniani.
Lazima tumshukuru JPM kwa kupambana na majangiri waliokuwa wanaua tembo, faru, twiga wetu, kupunguza rushwa, kujenga kujenga, kununua, kununua, nk, tusimvunje nguvu mtu kama huyu, kwani hata yeye starehe anazitaka, marafiki anawataka, kusafiri nje ya nchi zilizoendelea walizohangaikia marais wenzie anataka lakini anaona aibu. Marais wanaoona aibu sio wengi, hasa katika nchi zetu hizi.
Tunafahamu kuwa wako watu ambao wamekatishwa mipango yao haramu ya kuwinda, kuchimba, kukata magogo, kuiba, ajira, ufisadi na ukuwadi wa nchi mabeberu; obvious, hawa hawatampa kura Mzee Magufuli, hivyo tutashangaa kusikia Rais Magufuli kapata kura zote kabisa. Lakini wale wapiga kura ambao wanapanda ndege, treni, na magari baada ya Magufuli kuwezesha upatikanaji wake hawa watampa kura, na wale ambao wataona Magufuli kasababisha unafuu wa aina fulani katika upatikanaji wa huduma fulani ambayo haikuwepo kabla hawa pia watampa kura ya NDIYO bila ya kupepesa macho.
Hata wale ambao wanafahamu kuwa hawajapandishwa mishahara yao kwakuwa Magufuli alikuwa anatumia hela nyingi kwa kuboresha miundombinu na huduma ambazo zinahitaji hela nyingi ambazo hatuna, pia hawa watampa kura za ndiyo JPM.
NI wahalifu tu ambao watasita kumpa kura ili warejee vitendo vyao
Haki yake tumpe