Elections 2015 Magufuli ataja mafisadi CCM

makundubhyali

JF-Expert Member
May 26, 2013
2,389
882
Ameahidi atakapoingia madarakani, atahakikisha kuwa mafisadi wote wanashughulikiwa bila woga.

Mgombea Urais wa CCM, Dk. John Pombe Magufulu akizumgumza katika mkutano wa kampeni
Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, amesema mafisadi wamo hadi ndani ya chama chake na ndiyo maana baada ya kuteuliwa kuwa mgombea urais wengi wao wameanza kuweweseka kutokana na hofu kubwa waliyo nayo dhidi yake.

Akizungumza kwa nyakati tofauti katika mikutano ya kampeni ya chama chake mjini Kisarawe, Pwani na baadaye Ukonga, jijini Dar es Salaam jana, Magufuli alikiri kuwa chama chake kiliwalea walarushwa na mafisadi kwa muda mrefu na ndiyo maana baadhi ya watu walianza kukichukia.

Hata hivyo, alisema tatizo hilo halitakuwapo tena kwani atakapoingia madarakani baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, atahakikisha kuwa mafisadi wote wanashughulikiwa bila woga.

“Ndugu zangu, nasema kweli mafisadi hawako upinzani tu... ni ngumu sana mtu aliye ndani ya CCM kuyasema haya, lakini lazima niseme ukweli maana msemaukweli ni mpenzi wa Mungu. Haya mafisadi ndiyo yametufikisha hapa na (sasa), lazima tuyashughulikie,” alisema Magufuli na kushangiliwa na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wake wa Ukonga.

Magufuli aliwataja kwa sifa za jumla mafisadi waliopo kuwa ni pamoja na baadhi ya viongozi wa serikali, ambao hujihusisha na vitendo vya rushwa na dhuluma dhidi ya wananchi kiasi cha kuifanya serikali ichukiwe na baadhi ya wananchi wake.

Akitolea mfano, Magufuli alisema ni aibu kuona serikali ikikimbizana na mamalishe na wafanyabiashara ndogondogo (Wamachinga) ili kupata kodi wakati kuna baadhi ya nchi ambazo zinaendeshwa kwa mapato ya bandari tu.

Magufuli aliongeza kuwa anatambua wananchi wamekuwa wakinyanyaswa katika maeneo mbalimbali ikiwamo kutozwa kodi zisizosaidia kuinua pato la taifa bali kuwafaidisha baadhi ya viongozi na kwamba, kwa sababu hiyo, haoni sababu ya kuendelea kwa hali hiyo hasa kwa kujua kuwa kuna nchi zinajiendesha kwa mapato ya bandari.

Alisema yote hayo ni baadhi ya mambo anayoamini kuwa ni sababu ya yeye kuchaguliwa kuwa rais ili kudhibiti uonevu kwa wanyonge na pia kupambana na mafisadi serikalini, ambao wamezoea kuishi kwa rushwa na ulaghai.

Kwa mfano, alisema anajua namna ambavyo baadhi ya watumishi bandarini huruhusu makontena kupita bila kulipiwa ushuru na kuikosesha serikali mapato yake ili kuwahudumia wananchi.

“Wapo watu wanaikosesha serikali mapato. Hawa nataka nikapambane nao... na nitapambana nao kweli kweli. Na hawatanikwepa…najua wananiogopa na wameanza kumwaga hela ili nishindwe. Nyinyi hela zao kuleni maana ni kodi zenu, lakini kura ni kwa Magufuli,” alisema.
K/K
Sasa wanaCCM wanaokuwa wanabwabwaja humu kuwa mafisadi wamekimbia CCM hebu tuelezeni ninyi na magufuri nani mwongo
 
Eti mafisadi atawashughulikia ebu tujiulize
1. Aliyeuza nyumba za serikali ni nani?
2. Aliyeiba billion 262 wizara ya Ujenzi ni nani?
3. Aliyekamata meri ya samaki kipumbavu na serikali kulipa billion 3.6 ni nani?

Eti Leo hii apambane na mafisadi huu in ujinga, upumbavu na upuuzi mtupu mkadanganye walevi.
 
Eti mafisadi atawashughulikia ebu tujiulize
1. Aliyeuza nyumba za serikali ni nani?
2. Aliyeiba billion 262 wizara ya Ujenzi ni nani?
3. Aliyekamata meri ya samaki kipumbavu na serikali kulipa billion 3.6 ni nani?

Eti Leo hii apambane na mafisadi huu in ujinga, upumbavu na upuuzi mtupu mkadanganye walevi.

neenda kumuulize sumaye atakujibu vizuri madai yako.
 
Ameahidi atakapoingia madarakani, atahakikisha kuwa mafisadi wote wanashughulikiwa bila woga.

Mgombea Urais wa CCM, Dk. John Pombe Magufulu akizumgumza katika mkutano wa kampeni
Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, amesema mafisadi wamo hadi ndani ya chama chake na ndiyo maana baada ya kuteuliwa kuwa mgombea urais wengi wao wameanza kuweweseka kutokana na hofu kubwa waliyo nayo dhidi yake.

Akizungumza kwa nyakati tofauti katika mikutano ya kampeni ya chama chake mjini Kisarawe, Pwani na baadaye Ukonga, jijini Dar es Salaam jana, Magufuli alikiri kuwa chama chake kiliwalea walarushwa na mafisadi kwa muda mrefu na ndiyo maana baadhi ya watu walianza kukichukia.

Hata hivyo, alisema tatizo hilo halitakuwapo tena kwani atakapoingia madarakani baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, atahakikisha kuwa mafisadi wote wanashughulikiwa bila woga.

"Ndugu zangu, nasema kweli mafisadi hawako upinzani tu... ni ngumu sana mtu aliye ndani ya CCM kuyasema haya, lakini lazima niseme ukweli maana msemaukweli ni mpenzi wa Mungu. Haya mafisadi ndiyo yametufikisha hapa na (sasa), lazima tuyashughulikie," alisema Magufuli na kushangiliwa na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wake wa Ukonga.

Magufuli aliwataja kwa sifa za jumla mafisadi waliopo kuwa ni pamoja na baadhi ya viongozi wa serikali, ambao hujihusisha na vitendo vya rushwa na dhuluma dhidi ya wananchi kiasi cha kuifanya serikali ichukiwe na baadhi ya wananchi wake.

Akitolea mfano, Magufuli alisema ni aibu kuona serikali ikikimbizana na mamalishe na wafanyabiashara ndogondogo (Wamachinga) ili kupata kodi wakati kuna baadhi ya nchi ambazo zinaendeshwa kwa mapato ya bandari tu.

Magufuli aliongeza kuwa anatambua wananchi wamekuwa wakinyanyaswa katika maeneo mbalimbali ikiwamo kutozwa kodi zisizosaidia kuinua pato la taifa bali kuwafaidisha baadhi ya viongozi na kwamba, kwa sababu hiyo, haoni sababu ya kuendelea kwa hali hiyo hasa kwa kujua kuwa kuna nchi zinajiendesha kwa mapato ya bandari.

Alisema yote hayo ni baadhi ya mambo anayoamini kuwa ni sababu ya yeye kuchaguliwa kuwa rais ili kudhibiti uonevu kwa wanyonge na pia kupambana na mafisadi serikalini, ambao wamezoea kuishi kwa rushwa na ulaghai.

Kwa mfano, alisema anajua namna ambavyo baadhi ya watumishi bandarini huruhusu makontena kupita bila kulipiwa ushuru na kuikosesha serikali mapato yake ili kuwahudumia wananchi.

"Wapo watu wanaikosesha serikali mapato. Hawa nataka nikapambane nao... na nitapambana nao kweli kweli. Na hawatanikwepa…najua wananiogopa na wameanza kumwaga hela ili nishindwe. Nyinyi hela zao kuleni maana ni kodi zenu, lakini kura ni kwa Magufuli," alisema.
K/K
Sasa wanaCCM wanaokuwa wanabwabwaja humu kuwa mafisadi wamekimbia CCM hebu tuelezeni ninyi na magufuri nani mwongo

Mi nilidhani amewataja mafisadi kwa majina... KUMBE KALITAJA NENO FISADI
 
Eti mafisadi atawashughulikia ebu tujiulize
1. Aliyeuza nyumba za serikali ni nani?
2. Aliyeiba billion 262 wizara ya Ujenzi ni nani?
3. Aliyekamata meri ya samaki kipumbavu na serikali kulipa billion 3.6 ni nani?

Eti Leo hii apambane na mafisadi huu in ujinga, upumbavu na upuuzi mtupu mkadanganye walevi.


Na walevi nao wameshituka, hawadanganyiki safari hii... Labda ajidanganye mwenyewe
 
acha kumpigia promo...

sijaona jina hata moja la fisadi.

poor thread
Nilidhani ni miimi pekee ambaye sijaona jina la fisadi hata mmoja, kumbe mleta mada ndio mwenye makengeza
 
Mbona hawataji?huyu kilaza anafikiri nchi ni kama barara he!yeye mwenyewe ni fisadi mkubwa kauza nyumba za serekali,amejenga magorofa makubwa kwa mshaharagani?joka mkubwa huyu.
 
Ameahidi atakapoingia madarakani, atahakikisha kuwa mafisadi wote wanashughulikiwa bila woga.

Mgombea Urais wa CCM, Dk. John Pombe Magufulu akizumgumza katika mkutano wa kampeni
Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, amesema mafisadi wamo hadi ndani ya chama chake na ndiyo maana baada ya kuteuliwa kuwa mgombea urais wengi wao wameanza kuweweseka kutokana na hofu kubwa waliyo nayo dhidi yake.

Akizungumza kwa nyakati tofauti katika mikutano ya kampeni ya chama chake mjini Kisarawe, Pwani na baadaye Ukonga, jijini Dar es Salaam jana, Magufuli alikiri kuwa chama chake kiliwalea walarushwa na mafisadi kwa muda mrefu na ndiyo maana baadhi ya watu walianza kukichukia.

Hata hivyo, alisema tatizo hilo halitakuwapo tena kwani atakapoingia madarakani baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, atahakikisha kuwa mafisadi wote wanashughulikiwa bila woga.

“Ndugu zangu, nasema kweli mafisadi hawako upinzani tu... ni ngumu sana mtu aliye ndani ya CCM kuyasema haya, lakini lazima niseme ukweli maana msemaukweli ni mpenzi wa Mungu. Haya mafisadi ndiyo yametufikisha hapa na (sasa), lazima tuyashughulikie,” alisema Magufuli na kushangiliwa na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wake wa Ukonga.

Magufuli aliwataja kwa sifa za jumla mafisadi waliopo kuwa ni pamoja na baadhi ya viongozi wa serikali, ambao hujihusisha na vitendo vya rushwa na dhuluma dhidi ya wananchi kiasi cha kuifanya serikali ichukiwe na baadhi ya wananchi wake.

Akitolea mfano, Magufuli alisema ni aibu kuona serikali ikikimbizana na mamalishe na wafanyabiashara ndogondogo (Wamachinga) ili kupata kodi wakati kuna baadhi ya nchi ambazo zinaendeshwa kwa mapato ya bandari tu.

Magufuli aliongeza kuwa anatambua wananchi wamekuwa wakinyanyaswa katika maeneo mbalimbali ikiwamo kutozwa kodi zisizosaidia kuinua pato la taifa bali kuwafaidisha baadhi ya viongozi na kwamba, kwa sababu hiyo, haoni sababu ya kuendelea kwa hali hiyo hasa kwa kujua kuwa kuna nchi zinajiendesha kwa mapato ya bandari.

Alisema yote hayo ni baadhi ya mambo anayoamini kuwa ni sababu ya yeye kuchaguliwa kuwa rais ili kudhibiti uonevu kwa wanyonge na pia kupambana na mafisadi serikalini, ambao wamezoea kuishi kwa rushwa na ulaghai.

Kwa mfano, alisema anajua namna ambavyo baadhi ya watumishi bandarini huruhusu makontena kupita bila kulipiwa ushuru na kuikosesha serikali mapato yake ili kuwahudumia wananchi.

“Wapo watu wanaikosesha serikali mapato. Hawa nataka nikapambane nao... na nitapambana nao kweli kweli. Na hawatanikwepa…najua wananiogopa na wameanza kumwaga hela ili nishindwe. Nyinyi hela zao kuleni maana ni kodi zenu, lakini kura ni kwa Magufuli,” alisema.
K/K
Sasa wanaCCM wanaokuwa wanabwabwaja humu kuwa mafisadi wamekimbia CCM hebu tuelezeni ninyi na magufuri nani mwongo

Sijaona chochote ulichoandika,hayo majina yako wapi?hizi porojo peleka kwenu
 
neenda kumuulize sumaye atakujibu vizuri madai yako.

Amemtaja Jinga Kubwa?..Hiyo ni mbinu tu kama hizi zifuatazo!! Hakika mwaka huu ni wa "Mabadiliko" maana CCM wametumia na bado watatumia mbinu nyiingi bila Kufanikiwa kuyazuia Mabadiliko!!Mfano;
1. Wamenunua vyombo vya habari kama Magazeti,Vituo vya Redio na Runinga na Blogs lakini wapi!!
2. Wamenunua Viongozi Waandamizi wa vyama vya Upinzani kudhoofisha Mabadiliko lakini wapi!!
3. Wamenunua Wasanii wa Maigizo,Wanamichezo na Wanamuziki wa Kizazi Kipya kuwavuta vijana lakini wapi!!
4. Wametoa vitisho kwa watu wanaopenda mabadiliko vijana na wakina mama lakini wapi!!
5. Wamepenyeza watu kudhoofisha upinzani katika vyama na kwa Wanaharakati lakini hollaa!!
6. Wamejaribu kuzusha tuhuma mbalimbali kwa Viongozi wa "Mabadiliko" lakini wapiii!!
7. Wametumia vyombo vya dola kuzima "Mabadiliko" kwa kuwakamata na kuwasweka ndani na kuwafungulia kesi zisizokuwa na kichwa wala miguu wana Mabadiliko lakini wapiiiii!!
8. Wameunda Kamati ya watu 32 maalumu kwa ajili ya kuporomosha matusi na kuzusha tuhuma za ufisadi kwa Lowassa na wana "Mabadiliko" Lakini wapiiii!!
9. Waliapa kutokutumia Helkopta katika Uchaguzi wa Mwaka huu kwa kusingizio wanataka kupita kila kata kwa wapiga kura lakini wapiiii!!
10. Wameandaa tafiti feki za Twawezwa na Ipsos kuwalaghai wana "Mabadiliko" lakini wapi!!
11. Wametumia Mamilioni kuwalaghai watumishi wa Umma kama Polisi waliowatelekeza siku nyingi kwa kuwapa posho nono na ahadi lukuki lakini wapiiii!!
12. Wamejaribu kuwalaghai walimu ambao waliwasahau miaka nenda rudi na sasa wameahidi kuwalipa baadhi ya madai yao lakini wapiii!!
13. Wamejaribu kutoa kuwaondoa baadhi ya Watumishi wa idara Muhimu zinazohusika na uchaguzi ili kujenga hofu na kuandaa mipango miovu lakini wapi!!
14. Wamejaribu kuwatumia Vingozi wastaafu kuomba Huruma kwa Wananchi waliowaacha katika Umaskini mkubwa,maradhi na ujinga huku wakiwakejeli lakini wapiiii!!
15. Wamejaribu kuwazuia Wapinzani kutumia Viwanja vyao na Sehemu mbalimbali kwa ajili ya Kampeni lakini wapiiii!!
16. Wamejaribu kutumia ulaghai wa kuwavalisha wafuasi wao mavazi ya Upinzani ili wawakatate Viongozi wa Upinzani eti kuonesha kumeguka kwa Upinzani lakini wapi!!
17. Wamejaribu kupanga njama za kuwadhuru Viongozi wa Upinzani kwa namna mbalimbali lakini wapiii?
18. Wamejaribu kutumia Matamasha,Makongamano,Mikutano,Semina,Maandamano,Mikusanyiko,Matamko,na Warsha mbalimbali kubadili hisia za Wananchi dhidi ya Mabadiliko lakini wapiiiiiiiiiiiiiii!!!
19. Wamejaribu kupanga Mapinduzi hewa ya Kuwapindua Viongozi wa Upinzani kuonesha kumeguka kwa Umoja wa UKAWA lakini wapiii!!
20. Wamejaribu kupiga push ups,kuongea lugha za makabila mbalimbali,kucheza rhumba,kuandaa fiesta na Kufunga milango watu wasiondoke Viwanjani baada ya Fiesa lakini waaapi!!
21. Wamejaribu kusomba watu kwa malori,pikipiki,bajaji,Mabasi kutoka Mkutano mmoja hadi mwingie kujaza mikutano kuwahadaa wana "Mabadiliko"Lakini waaapi!!!
22. Kuzuia post za Ki "Mabadiliko" katika Mitandao ya Kijamiii kama JF,FB,Twitter, na Kuwa Block wanao post Mabadiliko ..Lakini wapiiii!!
23. Wamejaribu kuwashinikiza waajiri kuwafukuza Wafanyakazi wao wanaopenda Mabadiliko ili kuwatisha wengineo Lakini waapiii!!
24. Wamejaribu kurusha ndege za Kivita ili kuwatisha wananchi dhidi ya Mabadiliko pamoja na kuonesha Picha za Machafuko katika nchi mbalimbali na kufananisha Mabadiliko na Kuwait NA Iraq lakini waaapiiii!!!!
25. Wanajaribu kutengeneza "Goli la Mkono" kwa takwimu za wapiga kura na kuzuia Wapinzani kuhakiki taarifa sahihi za Vifaa na Daftari kwa wakati lakini wapiiiiii!!
26. Wamejaribu kuzindua Miradi iliyokwisha zinduliwa zamani pamoja na Miradi hewa ama ambayo hata haijaanza kuwarubuni wananchi lakini wapi!!!!
27. Na bado ndani ya siku zilizobakia watakuja na mbinu mbalimbali tena huenda zikawa ni mbaya zaidi na zenye dalili ya uvunjifu wa AMANI na UTULIVU wa Nchi ili mradi wazuie "Mabadiliko" ninaamini kwa Msaada wa MUNGU watashindwa na kulegea!!!!
Mimi nitampigia kura yangu ya thamani "EDWARD NGOYAI LOWASSA" pamoja na "Diwani na "Mbunge" wa UKAWA!!..Kwa maisha bora ya kwako nay a Kizazi chako Ondoa CCM,kwani imeishiwa pumzi!!!! "ALUTA Continua, Victoria Ascerta".... "The Struggle Continues, Victory is Certain"; ...Mapambano yanaendelea, Ushindi unakuja!!
 
Back
Top Bottom