Magufuli asema Sheria haina CCM, CHADEMA wala CUF

Magufuli asema Sheria haina CCM, CHADEMA wala CUF

sokoinei

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2012
Posts
1,832
Reaction score
566
Waziri wa ujenzi Dr John Pombe Magufuli amesema kuwa bomoa bomoa inayoendelea sasa kati ya barabara itakayo Mbeya kwenda Chunya yenye urefu wa Klm 76 ni katika kutekeleza sheria kwa wale wote waliojenga ktk hifadhi ya barabara!

Alisema kwamba wale wote waliojenga ktk eneo la akiba ya barabara wataendelea kuwa Masikini kwani serikali haitawalipa fidia na kwamba hawatajali kuwa ni nani anabomolewa nyumba hata km ni Viongozi kwani sheria haijui CDM,CCM wala CUF hata km ni mkuu wa mkoa sheria ni msumeno!!

Source ITV HABARI SAA 2 USIKU.

Je ni kweli kauli ya Magufuli ni sahihi au ni kwa vile tu nyingi ya nyumba zinazobomolewa ni za watu wadogo na wasiojua haki na sheria zinazowalinda?
 
Hapo mwisho umehitimisha vizuri sana Comrade, Magufuli ni janga jingine kama ni hivyo mbona tanesco ubungo aliiacha?? Magufuli ni mnafiki na mpenda sifa anapenda kuonea maskini na watu wasio na majina kwa sababu anaona hawawezi kumtisha.
 
Jana sikuaminia alichosema ,eti kwa nini mapato ya faini ya malori yanayozidisha uzito mizani mkoani iringa ni hafifu?na kutaka uchunguzi ufanyike,INA MAANA MIZANI NI MRADI WA SERIKALI KUWAKOMOA WANANCHI?BADALA ASHUKURU KUWA WENYE MALORI HAWAZIDISHI UZITO YEYE ANATAKA MAPATO
 
Yaani alikuwa anatafuta sababu tu ya kutamka neno CHADEMA.
Magamba Bwana...
 
mbona alitulizwa na pinda huyo...........akae kimya tu afanye kazi tutaziona kazi zake hata asipo ropoka
 
Kwa kitendo chake cha kutoheshimu muda wa kwisha wa kampeni katika mkutano wake wa hadhara jana ambayo kisheria ilitakiwa kwisha saa 12.00 jioni na kujiongezea muda mpaka sasa 12.35 jioni ktk uwanja wa jangwani hakika pasipo na shaka magufuli pasipo na shaka ametuonyesha kuwa yeye haheshimu sheria na hii sio mara yake ya kwanza kutoheshimu sheria.

Katika uchaguzi wa marudio mwaka 2011 Igunga magufuli aliwataka wana igunga wasimchague mgombea wa chadema bwana Kashindiye kwa sababu hawata pewa mahindi ya msaada.Kesi ilipoenda mahakamani alidharau wito wa kuitwa mahakamani kutoa ushahidi.

Lakini pia sote tunakumbuka samaki wa magufuli ambapo kwa pupa aliwakamata wachina waliokuwa wanavua kwa halali samaki baharini kisha wachina kushinda kesi na serikali kutakiwa kulipa fidia ya mamilioni ya fedha...

Kuna visa kibao ambayo inaonyesha bwana huyu hajui utawala wa sheria....

Hoja imetolewa changieni




 
Hats tatizo no nape, UNC hauwezi analazimisha tu, UNC was magufuli bora wamtafute taji liundi au masanja mkandamizaji kuliko nape,
 
hUYU JAMAA NI MBABE ALIYEJIFICHA.bOMOA BOMOA YOTE YEYE NDIE CHANZO.

 
Last edited by a moderator:
Ni wanavijiji wangapi hadi leo wanamadai ya nyumba zao kupigiwa X na wangapi wamebomolewa nyumba zao na hawajalipwa na hakuna dalili za kulipwa Magukufuli alifuata sheria ipi kikatiba kuvunja nyumba za wanavijiji hao ambayo imo kwenye Katiba bila ya kuwalipa ? Na bado mtu huyu anahadithi za kujenga barabara mpya ,wakati hizo alizojenga kibabe ni za kiwango cha chini kabisa zenye kusababisha ajali kila siku ,kwa maana barabara za Tanzania baada ya UHURU miaka 60 iliyopita ,ilikuwa iwe na dual carriageway zinazokwenda na kurudi na ndani ya miji mikuu kila upande wa njia kuu ulihitaji uwe na njia nne
 
Watanzani ni viumbe wa ajabu rais Kikwete mnamuita dhaifu mnasema hana maamuzi magumu Dr.Magufuli kafanya maamuzi magumu mnasema mbabe na dictator...daah!!
 
Watanzani ni viumbe wa ajabu rais Kikwete mnamuita dhaifu mnasema hana maamuzi magumu Dr.Magufuli kafanya maamuzi magumu mnasema mbabe na dictator...daah!!

Kwa sasa tunahitaji rais dictator. Watu wengi wanapuuza sheria na miongozo makusudi. Nidhamu na uadilifu kwa watumishi wa umma ni zero. Tingatinga anza kazi mara moja!!!
 
Huyu Magufuli ni mbabe na hana huruma hata kidogo anachopita akikieleza ni kilio cha mamba ,UKAWA wanaondoa X zote na Magufuli atatoa hela mfukoni mwake kuwalipa wale aliowavunjia nyumba na hakuwapa hata liwazo.
 
Huyu Magufuli ni mbabe na hana huruma hata kidogo anachopita akikieleza ni kilio cha mamba ,UKAWA wanaondoa X zote na Magufuli atatoa hela mfukoni mwake kuwalipa wale aliowavunjia nyumba na hakuwapa hata liwazo.
Kwa hiyo Ukawa wakichukua nchi wananchi ruksa kujenga nyumba kwenye hifadhi za barabara.
 
Kwa hiyo Ukawa wakichukua nchi wananchi ruksa kujenga nyumba kwenye hifadhi za barabara.

Sio UKAWA wakichukua nchi,shee wangu UKAWA wameshachukua nchi wanasubiri kuapishwa tu ,ila Kikwete haonekani kwenye ili kukabidhi madaraka.

Back on the topic--- Haki inatakiwa itendeke kwa kuifuata KATIBA ya nchi na si vinginevyo ,kwa kuwa wewe ni waziri wa miundombinu unakuwa hushirikishi wengine ,hufuati KATIBA unatunga sheria zako ,alimuradu uonekane ni mchapa kazi ,vilio kila anapopitisha barabara au China wanafanya hivyo ?
 
Kwa sasa tunahitaji rais dictator. Watu wengi wanapuuza sheria na miongozo makusudi. Nidhamu na uadilifu kwa watumishi wa umma ni zero. Tingatinga anza kazi mara moja!!!

Dikteta aanzie huko huko kwa wakubwa wanaofanya nchi ikaenda mrama na sio kwa walalahoi,
 
Back
Top Bottom