Magufuli anapotoshwa au vinginevyo?Kisa cha Hon. Justice Dr. Eliezer Mbuki Feleshi

Tunkamanini

JF-Expert Member
Jul 18, 2014
377
93
2bf98b9e86c66899288ce53f8c66ece5.jpg

Binafsi sina tatizo sana na utendaji wa Mhe. Rais, naiona dhamira yake ya dhati kabisa katika kulipeleka Taifa mbele, bado ninaimani kubwa sana na JPM kiutendaji.

Yako mengi Mhe. Rais anayofanya na kutufanya wengine tubaki midomo wazi na hivyo kushindwa kuelewa whether ni yeye au wasaidizi wake wanampotosha.

Binafsi mpaka leo huwa najiuliza nikikumbuka siku Mhe. Rais alipomnanga DPP Feleshi siku akiongea na waendesha mashitaka pamoja na wapelelezi kisa kesi ya wale samaki wa Magufuli, nilijiuliza maswali mengi sana, kwa sisi tunavyoielewa tasnia ya sheria nchini ilivyo, ukambedha mtu kama mhe. Feleshi utafanya kazi na nani? yule gwiji wa sheria za jinai, kaongoza kitengo kile nyeti kwa miaka mingi kuliko DPP yeyote yule katika historia ya nchi tena akiwa kijana, uadilifu wa Feleshi uliliza mastate attorneys siku JPM alivyozungumza yale maneno.

Kila napohusanisha hili swala na haya yanayoendelea mitandaoni najiuliza, je ni kweli JPM anakuwa hajui hivyo ANAPOTOSHWA na wasaidizi wake au ni vinginevyo?
 
Mimi nikishaona mtu anamuadress mwenzake kwa neno Mheshimiwa wakati ni cheo cha kitaaluma tayari naona walakini. Eti Mh DPP, Mh AG...etc

Tuwaachie hao wanaojua kusoma na kuandika tu huo uHeshimiwa

Hata hivyo nadhani katika MaDPP waliopwaya kuliko wote Feleshi ni mmojawapo. Nadhani alichaguliwa wakati mbaya tu ambapo ule msigano wa Polisi(Prosecuters) na ofisi ya AG ulikua umefika kileleni.
 
Feleshi aliweka wazi kesi ike hawatashinda ila Magu kwa ubishi wake wa kuzaliwa nao na kiburi alilazimisha ndio akapata alichostahili...serikali ililipa 3b kwa kukamata meli ya watu na kupoka vibua na tasi wa watu nila mpango
 
Uliona mbali mkuu, leo hii ndiye kiongozi wa mahakama kuu (Jaji Kiongozi), na kwa umri wake bila shaka ndiye Jaji Mkuu ajaye, kweli Jiwe alikurupuka.
 
Uliona mbali mkuu, leo hii ndiye kiongozi wa mahakama kuu (Jaji Kiongozi), na kwa umri wake bila shaka ndiye Jaji Mkuu ajaye, kweli Jiwe alikurupuka.
Anazidi kuongeza CV, sasa ni wazi kweli huyo ndiye CJ ajaye.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom