Ndipo ulipoishia upeo wako. I respect your opinionsSijawahi kuona kujikomba kwa kiwango hiki cha unafiki na uzandiki kwa hiyo unawashtaki watumishi wa umma kwa wananchi huku ni kujikomba kwa kiwango cha degree ya kwanza!@#@^$*&*!
Well said! Human resources ndo kila kitu hata km wagonjwa wote watalala vitandani lakini daktari hana moyo wa kuwatibu watakufa tu, lakini hata wakilala chini na daktari ana moyo wa kuwaponya watatibiwa na watapona tu
Escapist, mkiambiwa ni wavivu mnakuja juu.daktari akiwa night shift ana pingamizi kujiburudisha mchana? ukiwa ukanda wa pwani mchana kutwa utakuta watu vijiweni wakinywa kahawa na kupiga soga. ukichunguza utagundua kuwa wengi wao kama sio wote wako kazini baharini usiku kucha. usipende kujumuisha katika hoja zako
Hebu weka majina ya hao madaktari tumpatie mkuu wa wilaya ya temeke awasweke rumande maana wana kunywa na kushinda bar muda wa kazi!
Wambie wajiandae kunyooka!
Wakuu, niko Rachel bar Moshibar .- Ukonga. Pembeni yangu kuna watu watano wanapata bia. Katika hali ya kustaajabisha namsikia jamaa mmoja akilaani kitendo cha mh. rais kufuta sherehe za uhuru. Anaelezea jinsi gani rais anavyojijengea chuki na watumishi wa umma. Jamaa anahitimisha kwa kutolea mfano yeye akiwa daktari kwenye sherehe za uhuru hutoka na shilingi laki tatu. Anajiapiza kuwa Magufuli atarogwa kwa sababu hii ya kuwanyima ulaji.
Baada ya kuyasikia haya nasema moyoni mwangu, bado safari ni ndefu sana kufikia mageuzi ya kweli. Juzi nilimsikia mama mmoja akilalamika kuwa mwalimu mkuu (shule hakutaja ) alimwambia wazi wazi kwamba kitendo cha kuondoa michango na tuition mashuleni hakikubaliki. Kwamba walimu hawajafurahi hata kidogo, kisha akamwahidi mama huyo kuwa baada ya miezi sita mtakuja kutupigia magoti mkiomba tuition.
Hivi watanzania tumekuwaje hasa!? Unataka nini? Mbona inavyoonekana "wasomi" ndio wanageuka kikwazo kwa mabadiliko chanya? Kundi la wasomi limegeuka kuwa wapigania maslahi binafsi. Tutafika kweli!!?
Mungu mtie nguvu rais wetu, tuko pamoja naye. Amina
Mkuu Posho za wabunge ziko kisheria sio Hisani hivyo hawezi kuzifuta labda kupunguza.
Dodoma sio eneo la kazi kwa wabunge bali ni kwenye majimbo yao. Huwezi kumtoa mbunge kule mtwara aje Dodoma usimpe pesa ya accomodation pamoja na kujikimu
Posho hii haiko tu kwa wabunge bali kwa wafanyakazi wote wa umma na makampuni binafsi wakiwa nje ya eneo lao la kazi.
......
Baada ya kuyasikia haya nasema moyoni mwangu, bado safari ni ndefu sana kufikia mageuzi ya kweli. Juzi nilimsikia mama mmoja akilalamika kuwa mwalimu mkuu (shule hakutaja ) alimwambia wazi wazi kwamba kitendo cha kuondoa michango na tuition mashuleni hakikubaliki. Kwamba walimu hawajafurahi hata kidogo, kisha akamwahidi mama huyo kuwa baada ya miezi sita mtakuja kutupigia magoti mkiomba tuition....
Wasomi ni kikwazo, ndiyo waliomshabikia hata lowasa