Magufuli amewaumiza watumishi wa umma!

Magufuli amewaumiza watumishi wa umma!

Nyenyere

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2010
Posts
14,842
Reaction score
10,765
Wakuu, niko Rachel bar Moshibar .- Ukonga. Pembeni yangu kuna watu watano wanapata bia. Katika hali ya kustaajabisha namsikia jamaa mmoja akilaani kitendo cha mh. rais kufuta sherehe za uhuru. Anaelezea jinsi gani rais anavyojijengea chuki na watumishi wa umma. Jamaa anahitimisha kwa kutolea mfano yeye akiwa daktari kwenye sherehe za uhuru hutoka na shilingi laki tatu. Anajiapiza kuwa Magufuli atarogwa kwa sababu hii ya kuwanyima ulaji.

Baada ya kuyasikia haya nasema moyoni mwangu, bado safari ni ndefu sana kufikia mageuzi ya kweli. Juzi nilimsikia mama mmoja akilalamika kuwa mwalimu mkuu (shule hakutaja ) alimwambia wazi wazi kwamba kitendo cha kuondoa michango na tuition mashuleni hakikubaliki. Kwamba walimu hawajafurahi hata kidogo, kisha akamwahidi mama huyo kuwa baada ya miezi sita mtakuja kutupigia magoti mkiomba tuition.

Hivi watanzania tumekuwaje hasa!? Unataka nini? Mbona inavyoonekana "wasomi" ndio wanageuka kikwazo kwa mabadiliko chanya? Kundi la wasomi limegeuka kuwa wapigania maslahi binafsi. Tutafika kweli!!?

Mungu mtie nguvu rais wetu, tuko pamoja naye. Amina
 
Hao ni watu wa kunyongwa tu.

Umeposti saa tisa na nusu hivyo hao watu wanakunywa wakati wa kazi!

Huo ndo mfano wa watu wanaojifanya wanafanya kazi kumbe ni mizigo.
 
Hao ndio wezi waliotufikisha hapa tulipo. Kama angesema wafanyakazi wanamchukia Dk. Magufuli kwa kuwanyima au kupunguza mishahara yao ningemuelewa. Akafie mbele hukoooooo kama vipi aache kazi apate kazi kutafuta kazi.
 
Huu utawala kuna malofa waliojaa serikali watachezea sana mvua kizembe. Kuna wajinga walikuwa wanaimba mabadiliko na kumpinga magufuli kwa nguvu zote eti ni wale wale kumbe walijua hatma yao inakuja. Msiwe na wasiwasi magufuli hajawai kushindwa hao malofa watanyooshwa tu.
 
so huyo mlevi mmoja ndio kwako ametosha kuwakilisha watumishi wa umma wa Tanzania??
 
Afute kwanza posho za wabunge, inakuwaje anakomalia wafanyakazi tu?
 
We unadhani hata sitting allowance ikifutwa wabunge watafurahi?

Magufuli ana kazi sana@huo ndo uhalisia wa mambo,mwanadamu anaangalia kwanza interest zake rais anataka kubadili mambo ili watu kwa ujumla wanufaike ni kaazi sana
 
Wakuu, niko Rachel bar Moshibar .- Ukonga. Pembeni yangu kuna watu watano wanapata bia. Katika hali ya kustaajabisha namsikia jamaa mmoja akilaani kitendo cha mh. rais kufuta sherehe za uhuru. Anaelezea jinsi gani rais anavyojijengea chuki na watumishi wa umma. Jamaa anahitimisha kwa kutolea mfano yeye akiwa daktari kwenye sherehe za uhuru hutoka na shilingi laki tatu. Anajiapiza kuwa Magufuli atarogwa kwa sababu hii ya kuwanyima ulaji.

Baada ya kuyasikia haya nasema moyoni mwangu, bado safari ni ndefu sana kufikia mageuzi ya kweli. Juzi nilimsikia mama mmoja akilalamika kuwa mwalimu mkuu (shule hakutaja ) alimwambia wazi wazi kwamba kitendo cha kuondoa michango na tuition mashuleni hakikubaliki. Kwamba walimu hawajafurahi hata kidogo, kisha akamwahidi mama huyo kuwa baada ya miezi sita mtakuja kutupigia magoti mkiomba tuition.

Hivi watanzania tumekuwaje hasa!? Unataka nini? Mbona inavyoonekana "wasomi" ndio wanageuka kikwazo kwa mabadiliko chanya? Kundi la wasomi limegeuka kuwa wapigania maslahi binafsi. Tutafika kweli!!?

Mungu mtie nguvu rais wetu, tuko pamoja naye. Amina
Ndiyo maana mara nyingi Magufuli amesikika mara kwa mara akiwasihi watanzania wamwombee kwa Mungu kutokana na 'mapambano' aliyoyaanzisha na vigogo.
Kwa kuwa ni ukweli usiopingika kuwa katika utawala huu wa Magufuli, watakaopata pigo sana ni wale watumishi wa Umma, ambao waligeuza job description zao walizopewa za utumishi wa Umma na kugeuza job description hizo na kuwa ni utumishi kwa ajili ya maslahi yao binafsi na ya familia zao peke yake.
 
Hao ni watu wa kunyongwa tu.

Umeposti saa tisa na nusu hivyo hao watu wanakunywa wakati wa kazi!

Huo ndo mfano wa watu wanaojifanya wanafanya kazi kumbe ni mizigo.

Hiyo saa tisa si afadhali, kuna hao wanao piga bia wakienda kupata supu ya breakfast halafu wanarudi maofisini
 
Sherehe za uhuru walioathilika zaidi ni makada wa ccm. Walikuwa wanapewa per diem kwenda dar kushiriki. Wafanyakazi wataathirika kama mei mosi zikifutwa, kitu ambacho hakiwezekani kwani sio sherehe za kiserikali
 
Afute kwanza posho za wabunge, inakuwaje anakomalia wafanyakazi tu?

Kuna mzungu aliwahi kunitania akisema Tanzania kwa posho ni kiboko. kuna:

Sitting allowance,
Sleeping allowance
Standing allowance
Running allowance
Walking allowance
Travelling allowance
Meeting allowance
 
so huyo mlevi mmoja ndio kwako ametosha kuwakilisha watumishi wa umma wa Tanzania??

Ndugu yangu huyu jamaa katoa mfano wa kwanza na nina uhakika wako wengi tu aina hiyo. Wewe jiweke mwenyewe kwenye nafasi za hawa watumishi, ungejisikiaje? Cha muhimu tuwe pammoja kupambana na tatizo hili sugu.
 
Kuna mzungu aliwahi kunitania akisema Tanzania kwa posho ni kiboko. kuna:

Sitting allowance,
Sleeping allowance
Standing allowance
Running allowance
Walking allowance
Travelling allowance
Meeting allowance


Hahaaaaaaa ila kweli tunaongoza kwa posho aisee, tena waheshimiwa wabunge ndo wanaongoza
 
Mungu ni mwema,, atamsaidia Rais wetu katika mapambano haya dhidi ya miungu watu walojaa ofisini bila kuwajibika,
Tumuombee kwa Mungu ili afanikishe malengo yake ya kutetea wanyonge
 
Wakuu, niko Rachel bar Moshibar .- Ukonga. Pembeni yangu kuna watu watano wanapata bia. Katika hali ya kustaajabisha namsikia jamaa mmoja akilaani kitendo cha mh. rais kufuta sherehe za uhuru. Anaelezea jinsi gani rais anavyojijengea chuki na watumishi wa umma. Jamaa anahitimisha kwa kutolea mfano yeye akiwa daktari kwenye sherehe za uhuru hutoka na shilingi laki tatu. Anajiapiza kuwa Magufuli atarogwa kwa sababu hii ya kuwanyima ulaji.

Baada ya kuyasikia haya nasema moyoni mwangu, bado safari ni ndefu sana kufikia mageuzi ya kweli. Juzi nilimsikia mama mmoja akilalamika kuwa mwalimu mkuu (shule hakutaja ) alimwambia wazi wazi kwamba kitendo cha kuondoa michango na tuition mashuleni hakikubaliki. Kwamba walimu hawajafurahi hata kidogo, kisha akamwahidi mama huyo kuwa baada ya miezi sita mtakuja kutupigia magoti mkiomba tuition.

Hivi watanzania tumekuwaje hasa!? Unataka nini? Mbona inavyoonekana "wasomi" ndio wanageuka kikwazo kwa mabadiliko chanya? Kundi la wasomi limegeuka kuwa wapigania maslahi binafsi. Tutafika kweli!!?

Mungu mtie nguvu rais wetu, tuko pamoja naye. Amina
Hebu weka majina ya hao madaktari tumpatie mkuu wa wilaya ya temeke awasweke rumande maana wana kunywa na kushinda bar muda wa kazi!
Wambie wajiandae kunyooka!
 
Wakuu, niko Rachel bar Moshibar .- Ukonga. Pembeni yangu kuna watu watano wanapata bia. Katika hali ya kustaajabisha namsikia jamaa mmoja akilaani kitendo cha mh. rais kufuta sherehe za uhuru. Anaelezea jinsi gani rais anavyojijengea chuki na watumishi wa umma. Jamaa anahitimisha kwa kutolea mfano yeye akiwa daktari kwenye sherehe za uhuru hutoka na shilingi laki tatu. Anajiapiza kuwa Magufuli atarogwa kwa sababu hii ya kuwanyima ulaji.

Baada ya kuyasikia haya nasema moyoni mwangu, bado safari ni ndefu sana kufikia mageuzi ya kweli. Juzi nilimsikia mama mmoja akilalamika kuwa mwalimu mkuu (shule hakutaja ) alimwambia wazi wazi kwamba kitendo cha kuondoa michango na tuition mashuleni hakikubaliki. Kwamba walimu hawajafurahi hata kidogo, kisha akamwahidi mama huyo kuwa baada ya miezi sita mtakuja kutupigia magoti mkiomba tuition.

Hivi watanzania tumekuwaje hasa!? Unataka nini? Mbona inavyoonekana "wasomi" ndio wanageuka kikwazo kwa mabadiliko chanya? Kundi la wasomi limegeuka kuwa wapigania maslahi binafsi. Tutafika kweli!!?

Mungu mtie nguvu rais wetu, tuko pamoja naye. Amina
Unambana mwalimu huku analipa kodi na kupata net salary ya laki mbili halafu na mtu kama wewe unasupport ujinga wakati gas na mikataba mingine ya wakubwa haizungumzi. Ni upuuzi
 
Back
Top Bottom