Polepole leo amesema kuwa wakati wa utawala wa Magufuli, yeye alikuwa akitumika kama mtu wa kati, baina ya Magufuli na Warioba, na kati ya Magufuli na Mkapa.
Akaeleza kuwa kila mara Warioba alimkumbusha juu ya katiba mpya, naye aliupeleka ujumbe huo kwa Magufuli. Magufuli alimwambia kuwa ni vigumu kwenye huo mhula wake wa kwanza kukamilisha mchakato wa katiba, kwa sababu wanamtandao hawataki katiba mpya, na kwamba yeye Magufuli kwa muda huo, ndani ya CCM, ni sawa na mtu ambaye yupo mtoni anaoga, lakini nguo zake zimeshikiliwa na hao wanamtandao. Akiwaudhi, wakiondoka na nguo zake, yeye atatoka vipi huko mtoni anakooga?
Hivyo akaomba upatikanaji wa katiba mpya ufanyike kwenye muhula wake wa pili. Bahati mbaya, mwanzoni tu mwa muhula wake wa pili, Mungu akampenda.
Leo ndiyo tumejua kuwa kumbe kizingiti cha kupatikana kwa katiba mpya ni Kikwete.
Akaeleza kuwa kila mara Warioba alimkumbusha juu ya katiba mpya, naye aliupeleka ujumbe huo kwa Magufuli. Magufuli alimwambia kuwa ni vigumu kwenye huo mhula wake wa kwanza kukamilisha mchakato wa katiba, kwa sababu wanamtandao hawataki katiba mpya, na kwamba yeye Magufuli kwa muda huo, ndani ya CCM, ni sawa na mtu ambaye yupo mtoni anaoga, lakini nguo zake zimeshikiliwa na hao wanamtandao. Akiwaudhi, wakiondoka na nguo zake, yeye atatoka vipi huko mtoni anakooga?
Hivyo akaomba upatikanaji wa katiba mpya ufanyike kwenye muhula wake wa pili. Bahati mbaya, mwanzoni tu mwa muhula wake wa pili, Mungu akampenda.
Leo ndiyo tumejua kuwa kumbe kizingiti cha kupatikana kwa katiba mpya ni Kikwete.