Magufuli ajibu shutuma za Zitto

Magufuli ajibu shutuma za Zitto

KadamaKadama

Member
Joined
Oct 9, 2013
Posts
86
Reaction score
65
Katika hali ya kukamiana kwenye mbio za uraisi Zitto Kabwe akiwa Mkoani Lindi alimshambulia dKT.magufuli kuhusu uuzwaji wa nyumba za serikali, lakini kwa nyakati tofautitofauti serikali ilishatolea majibu kuhusu uuzwaji wa nyumba hizo pasipo binafsi yeye Magufuli kujibu. Ikumbukwe yale yalikuwa maamuzi ya baraza la mawaziri kwa maana ya serikali nzima. Angalia Waziri Mkuu Mstaafu Ndugu Sumaye akitolea ufafanuzi:





Nyongeza ya jibu hapo juu:

Hata Nyerere aliuza nyumba za Serikali na aliwahi kuunda tume ktk hili:

Kutokana na idadi ya watumishi Serikalini kuongezeka kadri ukubwa wa Serikali ulivyokuwa unaongezeka, tatizo la uhaba wa makazi ya kudumu kwa watumishi wa Serikali liliongezeka. Kutokana na changamoto hiyo Serikali iliunda tume mbalimbali zilizotoa ushauri wa kitaalamu kuhusunamna bora ya kupunguza tatizo hili.


Baadhi ya tume hizo ni;


  • Tume ya ADU mwaka 1963
  • Tume ya Nsekela ya mwaka 1975
  • Tume ya Mramba mwaka 1984

Tume hizo zote zilipendekeza kuwa Serikali iondokane na gharama kubwaya kumiliki na kukarabati nyumba hivyo, kupendekeza kuanzishwa kwachombo kinachojitegemea kitakachoshughulikia suala la ujenzi wa nyumba za kuishi watumishi.

Kwa kutumia Sheria Na. 30 ya mwaka 1997 ya Wakala za Serikali (ExecutiveAgencies Act No. 30/1997), Serikali ilianzisha Wakala wa Majengo yaSerikali tarehe 17 Mei, 2002.
 
Last edited by a moderator:
Amini amini nakwambia, Watanzania wote kwasasa wanatazamia kupata kiongozi radical,msafi,mchapakazi na mwenye chembechembe za udikteta anayeweza kugeuza muelekeo wa mambo -up-side-down.
Mpaka sasa hakuna mtu anaye-fit hiyo profile kutoa Dr.JP Magufuli.
Ningeweza kumpa kurayangu Rev. Ramadhan lakini anakasoro moja kubwa sana (sio radical na hawezi kugeuza mambo juu chini chini juu).
Tumeshuhudia Dk.Magufuli kila wizara anayoenda ameinyoosha ipasavyo!
Nashindwa kuelewa watu wachache wanaosema kuwa Tanzania haimuhitaji Magufuli
 
Haya pro - Chadema njoo mumsifie tena Magufuli kamjibu Zitto.

Teh teh teh
 
Last edited by a moderator:
Bado hajajibu swali,
Kwanini basi huyo wakala wa majengo asiwe yeye ndio mmiliki wa hizo nyumba za serikali? Yaani kwanini serikali isingeanzisha agency ya kuzisimamia hizi nyumba badala ya kuziuza?

Na ukiuza nyumba aliyokua akikaa labda mkuu wa wilaya, akija mpya atakaa wapi?

Inaingia vipi akilini uuze Nyumba kwa Million 20 (mapato) miaka 15 iliyopita, kisha uanze kuwalipia rent waliokosa Nyumba baada ya hizo kuuzwa labda jumla million 45 (matumizi) kwa kipindi chote hicho??

Unakiri kua idadi ya wafanyakazi wa serikali inaongezeka kila kukicha, kama waliokuwepo serikalini kipindi kile waliuziwa hizo nyumba, vipi walioko serikalini sasa watauziwa zipi? Huoni kama ni ubaguzi?

Nani alipanga bei za kuuzia hizo nyumba? Utauzaje nyumba iliyoko Prime location kama Bongoyo Street, Oyesterbay, Kiwanja Low Density (Sqm 4,000) kwa million 30?? Tena hela ambayo huikusanyi mara moja bali unakata kidogokidogo kwenye mishahara??

Category ya kuwachagua wafanyakazi wa kuzinunua ilikua ni nini? Wapo watu ambao waliuziwa kwanza Nyumba kabla ya kupata ajira serikalini. Magazeti ya Habari Corporation yakiwa chini ya Jenerali Twaha Ulimwengu yaliandika sana hii story, tena file la transfer of ownership alikua akilibeba Magufuli mwenyewe kulipitisha Department mbalimbali na ole wako ucheleweshe, huu ni ufisadi huu, hauwezi kufutika kwa sifa ya mtu tu kukariri idadi ya madaraja na kilomita za barabara, bado anabaki fisadi tu.

Hapa bana watu waliamua kujiuzia hizo nyumba kifisadi, na hata kama ni uamuzi wa baraza la mawaziri basi walihakikisha kila mmoja anapata nyumba kwake au kwa ndugu yake

Kwa hili naungana na Zitto, yeyote alieshiriki huu ufisadi akiwemo Fredrick Tuluway Sumaye hatufai, na sio ws kuombea apitishwe hiyo tarehe 12-July
 
Last edited by a moderator:
yani uamuzi wa baraza la mawaziri hata wa kijambazi ndio uutekeleze,si angejiuzulu!!!halafu huyu kilaza alituambia wakazi masikini wa kigamboni tupige mbizi.
 
yani uamuzi wa baraza la mawaziri hata wa kijambazi ndio uutekeleze,si angejiuzulu!!!halafu huyu kilaza alituambia wakazi masikini wa kigamboni tupige mbizi.

Utamuaona tu mtu asiyerizika, tupo na nyumba anaswitch kupiga mbizi! haya kazi twende!
 
majibu ya magufuli ni blah blah tupu. hayana jipya. ndo maana tunasema tatizo ni mfumo wa hovyo uliojengwa na ccm. kwa sasahakuna rais bora ndani ya ccmkamwe.
 
Haya pro - Chadema njoo mumsifie tena Magufuli kamjibu Zitto.

Teh teh teh

Kile kile nilichokuambia jana..Wewe uko na hao Chadema hata kama mada haihusiani kabisa. Issue hapa NI..Tuhuma alizopewa JPM na Zitto, je ni za kweli au si kweli.
 
Last edited by a moderator:
Shakir

Mtoa mada hakueleza pia kuwa katika mamno ambayo Rais wa awamu ya Tatu, Mh Benjamin Mkapa anajutia ni kuuza nyumba za serikali. Ilikuwa makosa na wote waliohusika wanapaswa kuomba radhi.

Kama ilikuwa sahihi kudingekuwa na haja ya kuanzisha huo Wakala, maana serikali haikutakiwa kuwa na nyumba...na kama suala lilikuwa la gharama za matengenezo, hii haikuwa sababu ya msingi kwani kila kijengwacho kitahitaji matengenezo! Mbaya zaidi waliofanya maamuzi haya ndiyo walikuwa wafaidika wa kuuziana nyumba.
 
Last edited by a moderator:
Maghufuli ni vigumu sana kumchafua, watu wanaomzunguka wanaoweza kumtetea ni wengi mno. Tumuache tu nyota yake iko juu jamani.
 
Mtoa mada hakueleza pia kuwa katika mamno ambayo Rais wa awamu ya Tatu, Mh Benjamin Mkapa anajutia ni kuuza nyumba za serikali. Ilikuwa makosa na wote waliohusika wanapaswa kuomba radhi. Kama ilikuwa sahihi kudingekuwa na haja ya kuanzisha huo Wakala, maana serikali haikutakiwa kuwa na nyumba...na kama suala lilikuwa la gharama za matengenezo, hii haikuwa sababu ya msingi kwani kila kijengwacho kitahitaji matengenezo! Mbaya zaidi waliofanya maamuzi haya ndiyo walikuwa wafaidika wa kuuziana nyumba.
Hoja inabaki palepale, kosa la Maghufuli ni lipi kama siyo kumchafua?
 
Kile kile nilichokuambia jana..Wewe uko na hao Chadema hata kama mada haihusiani kabisa. Issue hapa NI..Tuhuma alizopewa JPM na Zitto, je ni za kweli au si kweli.
Wengi sana walishalirolea ufafanuzi, nadhani Sumaye kapigilia msumari, yeye kama Waziri Mkuu wa wakati huo, Maghufu sasa safi kabisa aendelee na harakati zake kwa roho nyeupe kabisa.
 
Hoja inabaki palepale, kosa la Maghufuli ni lipi kama siyo kumchafua?
Kuhusika na Kutekeleza maamuzi ya hivyo yaliyoiingiza serikali na nchi hasara kubwa. Kuwa sehemu ya uvunjaji huu wa kimaadili
 
majibu ya magufuli ni blah blah tupu. hayana jipya. ndo maana tunasema tatizo ni mfumo wa hovyo uliojengwa na ccm. kwa sasahakuna rais bora ndani ya ccmkamwe.
Wewe unasumbuliwa na Ushabiki wa kisiasa tu, hivi hata hayo aliyoyasema Waziri Mkuu aliyesimamia zoezi hilo bado unasema ni Maghufuli. Unakimbia kusema ni mfumo hata haujui mfumo ni nini, au unataka kutuambia Maghufuli ndiyo mfumo wenyewe. Acha na wewe comments blah blah.
 
Shakir

Unakurupuka kujibu bila kuangalia Sumaye alisema nini au uvivu wa kuchunguza mambo? Kipindi fulani Magufuli aliondolewa katika Wizara ya Ujenzi (2005-2010) ili wachunguze kama kulikuwa na wrongdoing mwisho wa siku wakaambulia patupu ikiwemo kumrudishia wizara anayoimudu - leo kila mtanzania asiye mnafiki anakiri mafanikio ya barabara ikiwemo ujenzi wa nyumba mpya za serikali.

Habari ya watu ndugu zake waliuziwa nyumba unazidi kupotea kabisa mambo haya yalichunguzwa vilivyo kipindi Magufuli kaondolewa wizarani, njooni na vitu vingine hili la nyumba mnapoteza muda wenu badala ya kuufanyia kazi zenye tija.
 
Last edited by a moderator:
Hoja si pro-chadema , bali hoja hiyo haijajibiwa mpka leo .Kimsingi hakuna hoja ya mashiko bali ni baraza la mawaziri kuamua kujiuzia nyumba kwa visingizio visvyo na mashiko.Mwaka uleule wameuza wakaenda kujenga nyumba kijitonyama na usalama wa taifa kwa ghrama kubwa na pia hazina hadhi ya kiuwaziri.Pia tuliona wengine wanapewa nyumba mbweni mabazo hazina hadhi.ona leo sasa hata bei waluyuzia hata siku moja hutapata kiwanja osterbay au masaki kwa shs.20mil
Huu ni usisadi wa ajoabu.unauz nyumba ya polisi kituoni , bila kujua polisi wana kaa baracks , baada ya kuuza inauzwa kwa rai , polisi anayetakiwa kukaa baracks hakai bali raia aliyeinunua .leo tunaona nyumba zili waliuziwa maofisa wa serikali ili wapate makazi , je leo ni makazi ya maofisa wa serikali au mahekalu ya matajiri kwa mgogo wa uzwaji huo
 
Amini amini nakwambia, Watanzania wote kwasasa wanatazamia kupata kiongozi radical,msafi,mchapakazi na mwenye chembechembe za udikteta anayeweza kugeuza muelekeo wa mambo -up-side-down.
Mpaka sasa hakuna mtu anaye-fit hiyo profile kutoa Dr.JP Magufuli.
Ningeweza kumpa kurayangu Rev. Ramadhan lakini anakasoro moja kubwa sana (sio radical na hawezi kugeuza mambo juu chini chini juu).
Tumeshuhudia Dk.Magufuli kila wizara anayoenda ameinyoosha ipasavyo!
Nashindwa kuelewa watu wachache wanaosema kuwa Tanzania haimuhitaji Magufuli
Ndiyo maana nasema, 2015 ni Maghufuli, hizo kelele ni za chura tu hazitamzuia Ng'ombe kunywa maji.
 
Bado hajajibu swali,
Kwanini basi huyo wakala wa majengo asiwe yeye ndio mmiliki wa hizo nyumba za serikali? Yaani kwanini serikali isingeanzisha agency ya kuzisimamia hizi nyumba badala ya kuziuza?

Na ukiuza nyumba aliyokua akikaa labda mkuu wa wilaya, akija mpya atakaa wapi?

Inaingia vipi akilini uuze Nyumba kwa Million 20 (mapato) miaka 15 iliyopita, kisha uanze kuwalipia rent waliokosa Nyumba baada ya hizo kuuzwa labda jumla million 45 (matumizi) kwa kipindi chote hicho??

Unakiri kua idadi ya wafanyakazi wa serikali inaongezeka kila kukicha, kama waliokuwepo serikalini kipindi kile waliuziwa hizo nyumba, vipi walioko serikalini sasa watauziwa zipi? Huoni kama ni ubaguzi?

Nani alipanga bei za kuuzia hizo nyumba? Utauzaje nyumba iliyoko Prime location kama Bongoyo Street, Oyesterbay, Kiwanja Low Density (Sqm 4,000) kwa million 30?? Tena hela ambayo huikusanyi mara moja bali unakata kidogokidogo kwenye mishahara??

Category ya kuwachagua wafanyakazi wa kuzinunua ilikua ni nini? Wapo watu ambao waliuziwa kwanza Nyumba kabla ya kupata ajira serikalini. Magazeti ya Habari Corporation yakiwa chini ya Jenerali Twaha Ulimwengu yaliandika sana hii story, tena file la transfer of ownership alikua akilibeba Magufuli mwenyewe kulipitisha Department mbalimbali na ole wako ucheleweshe, huu ni ufisadi huu, hauwezi kufutika kwa sifa ya mtu tu kukariri idadi ya madaraja na kilomita za barabara, bado anabaki fisadi tu.

Hapa bana watu waliamua kujiuzia hizo nyumba kifisadi, na hata kama ni uamuzi wa baraza la mawaziri basi walihakikisha kila mmoja anapata nyumba kwake au kwa ndugu yake

Kwa hili naungana na Zitto, yeyote alieshiriki huu ufisadi akiwemo Fredrick Tuluway Sumaye hatufai, na sio ws kuombea apitishwe hiyo tarehe 12-July

Unakurupuka kujibu bila fuatilia clip ya video ya Sumaye (Umecomment hivi kwenye thread fulani) alisema nini au uvivu wa kuchunguza mambo? Kipindi fulani Magufuli aliondolewa katika Wizara ya Ujenzi (2005-2010) ili wachunguze kama kulikuwa na wrongdoing mwisho wa siku wakaambulia patupu ikiwemo kumrudishia wizara anayoimudu - leo kila mtanzania asiye mnafiki anakiri mafanikio ya barabara ikiwemo ujenzi wa nyumba mpya za serikali.

Habari ya watu ndugu zake waliuziwa nyumba unazidi kupotea kabisa mambo haya yalichunguzwa vilivyo kipindi Magufuli kaondolewa wizarani, njooni na vitu vingine hili la nyumba mnapoteza muda wenu badala ya kuufanyia kazi zenye tija.
 
Hoja si pro-chadema , bali hoja hiyo haijajibiwa mpka leo .Kimsingi hakuna hoja ya mashiko bali ni baraza la mawaziri kuamua kujiuzia nyumba kwa visingizio visvyo na mashiko.Mwaka uleule wameuza wakaenda kujenga nyumba kijitonyama na usalama wa taifa kwa ghrama kubwa na pia hazina hadhi ya kiuwaziri.Pia tuliona wengine wanapewa nyumba mbweni mabazo hazina hadhi.ona leo sasa hata bei waluyuzia hata siku moja hutapata kiwanja osterbay au masaki kwa shs.20mil
Huu ni usisadi wa ajoabu.unauz nyumba ya polisi kituoni , bila kujua polisi wana kaa baracks , baada ya kuuza inauzwa kwa rai , polisi anayetakiwa kukaa baracks hakai bali raia aliyeinunua .leo tunaona nyumba zili waliuziwa maofisa wa serikali ili wapate makazi , je leo ni makazi ya maofisa wa serikali au mahekalu ya matajiri kwa mgogo wa uzwaji huo
Hata huweleweki unachosema, Maghufuli atakapoingia ikulu na kuwanyoosha ndo mtajua ni jembe la hatari sana.
 
Back
Top Bottom