- Source #1
- View Source #1
- Tunachokijua
- Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi la Kenya (National Police Service) iliyotolewa Machi 23 2026, Jiji la Nairobi ni eneo lililoathirika zaidi na mafuriko kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nchini humo, kukiwa na vifo 37 vilivyoripotiwa katika jiji hilo huku vifo vya jumla vikifikia 81 na uharibifu mkubwa ukitokea katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo.
Madai
Kumekuwapo na video inayosambazwa mtandaoni ikionesha hali ya mafuriko huku magari yakisombwa na kudaiwa kuwa ni tukio lililotokea Nairobi nchini Kenya.
Je, ni upi uhalisia wa Video hiyo?
Ufuatiliaji wa JamiiCheck kupitia Google Reverse Image Search umebaini eneo halisi linaloonesha jengo la Odeon linalopatikana katika makutano ya Barabara ya Latema na Mtaa wa Tom Mboya jijini Nairobi.
Aidha kupitia Google Earth ambayo inaonesha mazingira halisi ya eneo hilo ambapo hayafanani na video inayodai kuonesha mafuriko katika eneo hilo. Mfano saa, mabango na kadhalika havionekani katika video hiyo.
Aidha kupitia nyenzo za kubaini maudhui yaliyotengenezwa kwa akili unde zinabainisha kuwa video hiyo imetengenezwa kwa teknolojia hiyo.