IFAHAMU KWA UNDANI GARI AINA YA TOYOTA RAUM
Toyota Raum ni gari dogo lililotengenezwa na kampuni ya Toyota na kuuzwa kwenye soko la ndani la Japan (JDM) kuanzia mwaka 1997 mpaka mwaka 2011 ambapo uzalishaji wake ulisitishwa rasmi. Gari hili liko kwenye kundi la magari madogo kwa ajili ya matumizi mbali mbali yajulikanayo kitaalamu kama Mini Multi-Purpose Vehicle (Mini MPV).
Vitu vinavyokuja katika gari hii ni
Umbo ni Hatchback
Extras:Spoiler
Safety Features:ABS, Curtain Airbags, EBD, SRS
Airbags, TRC, VSC
Exterior Features:Alloy Rims(optional), Fog
Lights(optional)
Interior Features:A/C, CD/Radio player
Muundo wa gari hili ulijipatia umaarufu saana kwenye soko la Japan kutokana na kuwa na nafasi ya kubwa ndani huku nje likiwa na muonekano mdogo ambau unarahisisha uendeshaji hasa kwenye mjini ya Japan yenye msongamano mkubwa wa magari.
Kwenye uzi huu tutajikita zaidi kwenye generation ya pili (2nd Gen) ya gari hili ambayo ilianza kuzalishwa mwaka 2003 mpaka mwaka wa mwisho wa uzalishaji wake.
Matoleo ya 2nd Gen Raum
2nd Gen Raum ina matoleo makubwa mawili. Front-Wheel-Drive na All-Wheel-Drive (hizo AWD ni chache sana kwenye used market). Kimuonekano Raum haijabadilika saana tangu ilipotoka. Japo mwaka 2006 kulikuwa na mabadiliko kidogo kwenye design (facelif) hasa fog lights za mbele na ile taa kubwa ya nyuma. Kuna toleo moja lilitengenezwa maalumu kwa ajili ya kusaidia kubeba watu wenye ulemavu ambapo siti ya mbele au ya nyuma ya abiria huweza kutoka nje na kuwarahisishia kupanda au kushuka kwenye gari.
Engine na Gearbox
2nd Gen Raum inatumia moja kati ya engines maarufu kwa magari madogo ya Toyota kipindi hicho aina ya 1NZ-FE. Engine hii cylinder 4, ina cc 1496 (1.5l) na ina mfumo wa VVTi ili kuifanya itumie mafuta vizuri. Kama utakumbuka, engine hii imetumika pia kwenye magari kama Sienta, Premio, Allion, Probox, Ractis, Porte, Belta, Platz, Vitz n.k. So ni very common. Kwa upande wa gearbox, Raum ina gearbox ya automatic yenye gia nne (4 speed automatic) ambayo pamoja na engine
MATUMIZI YA MAFUTA
Utumiaji wa mafuta wa Raum kufikia wastani wa 10-12km kwa lita 1 mjini na 15-17km kwa lita 1ukiwa highway kutegemeana na uendeshaji wako.
GROUND CLEARENCE
Kutokana na umbo la gari hii ,uvungu wake ni 6.0 inch sawa na 165 mm …..mm naona kabisa gari hii inafaa sana kwa wana chato haiko complicated kivile ,haichagui njia unaweza kuwa kijijini au mjini bado ikakufaa kwa sasa hii ggari inapendwa sana na vijana
The goods
* Raum very reliable kiasi kwamba Toyota waliamua kulitengeneza kwa miaka karibu 10 bila mabadiliko yoyote makubwa. Maana jamaa wanasema, if it ain’t broke, don’t fix it. So unaweza litumia kwa mjini na hata safari za mbali bila mawazo kabisa.
* Nafasi ya kutosha ndani kulinganisha na magari mengi madogo. Watu watano wanaweza kukaa vizuri kwa safari ndefu. It is comfortable enough for its size and price. Pia dereva anaweza kutoka kwenye siti yake ya mbele mpaka siti ya nyuma kwa urahisi bila kushuka kwenye gari.
* Mfumo wake wa rear sliding doors kwa upande wa abiria na dereva unawezesha abiria wa size tofauti kuingia na kutoka kirahisi kwenye gari. Siti ya mbele ya abiria inaweza kukunjwa kwa mbele na kuacha nafasi kubwa zaidi kwa abiria na mizigo.
* Low maintenance cost, vile utumiaji wake wa mafuta naoweza sema kuwa ni relatively good kwa aina ya gari hili. Pia engine yake imetumika kwa magari mengi saana, so spare zinapatikana kirahisi. Vile vile Raum inashare parts nyingi na magari mengi madogo ya Toyota.
* Muonekano wake ni wa kisasa, linafaa kwa matumizi binafsi na biashara pia. Linapendwa na jinsia zote, japo kina dada wanalipenda zaidi, sijui kwa nini? Wenda ni vile wanapenda kusafiri na kundi la watu.
MATUNZO YA GARI HII
JITAHIDI USOME MANUAL BOOK YA GARI TU MM HAPA SIANDIKI CHOCHOTE
The bads
* Power sliding door mechanism ya upande wa abiria huwa inaharibika mapema, hasa pale jamaa wanapotumia nguvu kufungua badala ya kuacha mlango ufunguke wenyewe…..
Kuna changamoto ya sensor kwenye milango hasa ile ya kuslide ni vyema kabisa ukajipanga kuiweka manual badala ya automatic kama unapenda idumu kwa muda mrefu ...
* Only room for 5, wakati Spacio ambayo iko kwenye class moja na Raum inaweza kubeba watu 7. ....hapo ndio naona kuna shida kidogo
* Kwa kweli, zaidi ya tank dogo la mafuta, na muungurumo wa 1NZ, hakuna mengi ya kulalamika kuhusu gari hili.....engine hii naipemda muungurumonwake hasa kwa wazee wa kuweka xxx... Nadhani mnajua inavyokuwa inaunghuruma kibabe sana plus mziki wa wastani na taa za miguuninza rangi flani hivi ya bluuu
Cha kuzingatia unaponunua gari hili
Tafuta Lenye options nyingi hasa la kuanzia mwaka 2006, utalifaidi zaidi. Liwe na fog lighs, alloy wheels, ukipata ile yenye siti ya abiria ya umeme ni bora zaidi. Suspension system yake iko vizuri kwa kiasi kikubwa, shock absorber ni soft, japo mara nyingi bushes zinakuwa na zimekwish vile ni gari la siku nyingi. Hakikisha power sliding door mechanism inafanya kazi, otherwise utajikuta unakuwa konda wa daladala.
Maoni yangu
Kama unapenda mwonekano wake wa nje wa Raumu ,chaguo lako litakuwa sahihi sana kwa mizunguko hata safari , hunatatizo na gearlever iliyokaa kwenye dashboard, na instrument cluster (speed-o-meter) ya katikati ambayo inaruhusu abiria wote kuona taa ikiwaka pindi umeishiwa mafuta,na rahic kupitisha mchango chap wakachangia kama ni watumishi wenzako ,au majirani sio lift tu kila siku wakati hawataki kuchangia then 2nd Gen Toyota Raum ni gari zuri saana. Hasa wa matumizi ya familia kwenye mizunguko ya mjini. Go for it.
Raumu ni gari nzuri huwezi kuilinganisha na spansio japo zimechangia Engine moja lakini ...bado consuption ya mafuta ni nzuri sana, hata balance handle ni nzuri compare to spansio , Raumu ni gari inayofaa hata kwa wamama wale wenye matumbo makubwa ambao wawawezi kuinhia kwenye IST toyota kwa gari hii wanaingia bila shida na vitambi vyao karibu timu Raum, lakini pia ni gari isiyobagua hata watu wenye mahitaji maalumu bado ina miundo mbinu rafiki
Mwaka ndio tumeuanza jaribu kuifikiria hiii gari ....hautakuja kujutia hata kwa kula vichwa bado inavumilia sana
BEI YAKE NI YA KAWAIDA SANA KUANZIA MILION 8.5 mpka 12m kwa chases no UNAPATA
KWA MAKALA UFAFANUZI WA KITAALAMU USISITE KUNI WHATSAP KWA NAMBA 0623953036 GHARAMA NI SH 15000/-