Idd Azzan aomba radhi CCM
MBUNGE wa Kinondoni, mkoani Dar es Salaam, Idd Azzan, ameomba radhi mbele ya kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Dar es Salaam, kwa kitendo cha kukiuka maadili ya chama na kuwatuhumu viongozi wenzake katika vyombo vya habari.
Hayo yamesemwa jana Dar es Salaam na Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Mkoa, Juma Simba wakati akizungumza na waandishi wa habari na kuitaka Kamati ya Siasa ya Mkoa kutazama upya adhabu dhidi ya Mbunge huyo ya karipio kwa lengo la kumuondolea.
Azzan alifungiwa kwa miezi 18 kutogombea nafasi yoyote ndani ya chama pamoja na kupewa onyo kali kwa kosa la kutumia vibaya madaraka yake na kuzichafua mamlaka za CCM Mkoa wa Dar es Salaam.
Adhabu hiyo ilitolewa baada ya Azzan kuwatuhumu wajumbe wa Kamati ya Siasa na Sekretarieti ya Mkoa kuwa ni mafisadi na wala rushwa na kuwataka wajivue gamba.
Kwa mujibu wa Simba, Azzan aliomba radhi katika kikao cha kawaida cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa kilichofanyika juzi.
Katika kikao hicho kilichofanyika Kinondoni pamoja na mambo mengine, kilitoa maagizo hayo kwa Kamati ya Siasa baada ya mhusika kuomba radhi, alisema Simba.
Simba alisema kutokana na uamuzi huo wa Halmashauri ya Mkoa, Kamati ya Siasa itakutana na kuzingatia kanuni katika kutekeleza agizo hilo.
Katika hatua nyingine Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Dar es Salaam imekubali maombi ya Khamis Kizenga ya kurejeshewa uanachama wa CCM baada ya kutumikia adhabu ya kuvuliwa uanachama kwa zaidi ya mwaka mmoja na nusu.
source: HabariLeo | Idd Azzan aomba radhi CCM
MBUNGE wa Kinondoni, mkoani Dar es Salaam, Idd Azzan, ameomba radhi mbele ya kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Dar es Salaam, kwa kitendo cha kukiuka maadili ya chama na kuwatuhumu viongozi wenzake katika vyombo vya habari.
Hayo yamesemwa jana Dar es Salaam na Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Mkoa, Juma Simba wakati akizungumza na waandishi wa habari na kuitaka Kamati ya Siasa ya Mkoa kutazama upya adhabu dhidi ya Mbunge huyo ya karipio kwa lengo la kumuondolea.
Azzan alifungiwa kwa miezi 18 kutogombea nafasi yoyote ndani ya chama pamoja na kupewa onyo kali kwa kosa la kutumia vibaya madaraka yake na kuzichafua mamlaka za CCM Mkoa wa Dar es Salaam.
Adhabu hiyo ilitolewa baada ya Azzan kuwatuhumu wajumbe wa Kamati ya Siasa na Sekretarieti ya Mkoa kuwa ni mafisadi na wala rushwa na kuwataka wajivue gamba.
Kwa mujibu wa Simba, Azzan aliomba radhi katika kikao cha kawaida cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa kilichofanyika juzi.
Katika kikao hicho kilichofanyika Kinondoni pamoja na mambo mengine, kilitoa maagizo hayo kwa Kamati ya Siasa baada ya mhusika kuomba radhi, alisema Simba.
Simba alisema kutokana na uamuzi huo wa Halmashauri ya Mkoa, Kamati ya Siasa itakutana na kuzingatia kanuni katika kutekeleza agizo hilo.
Katika hatua nyingine Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Dar es Salaam imekubali maombi ya Khamis Kizenga ya kurejeshewa uanachama wa CCM baada ya kutumikia adhabu ya kuvuliwa uanachama kwa zaidi ya mwaka mmoja na nusu.
source: HabariLeo | Idd Azzan aomba radhi CCM