Mafuta ya Taa yaadimika Nchini, Bei yapanda

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,360
8,094
Bei ya mafuta ya taa imeongezeka kwa wastani wa Sh39 kwa mikoa mitatu ya Dar es Salaam, Mtwara na Tanga mwezi Machi ikilinganishwa na Februari 2023, huku uhaba wa bidhaa hiyo ukitawala.

Katika taarifa ya bei mpya za mafuta iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), Dk James Mwainyekule imeonyesha kuisha kwa bidhaa hiyo katika matanki yaliyopo Tanga.

"Kutokana na kuisha kwa mafuta ya taa kwenye matanki ya kuhifadhia yaliyopo Tanga, waendeshaji wa vituo vya mafuta kwenye mikoa ya Kaskazini wanashauriwa kuchukua mafuta ya taa kutoka katika Bandari ya Dar es Salaam," imesema taarifa hiyo.

Taarifa hiyo pia imeonyesha katika bandari tatu za Dar es Salaam, Mtwara na Tanga zinazopokea mafuta ni mbili pekee (Tanga na Dar es Salaam) ndio zenye matanki ya kuhifadhia mafuta ya taa.

Kutokana na kuisha kwa mafuta ya Tanga katika Bandari ya Tanga, hivyo nchi nzima kwa sasa inategemea mafuta ya taa kutoka Bandari ya Dar es Salaam huku athari ya kuongezeka kwa bei ya mafuta hayo imeongezeka.

"Bei ya mafuta ya taa mkoani Tanga imeongezeka kutoka Sh3,107 Februari Hadi Sh3,144 Machi, huku Mtwara ikiongezeka kutoka Sh3,134 hadi Sh3,170 mwezi huu," imesema taarifa hiyo.

Wakati mafuta ya taa yakipatikana katika bandari moja pekee, takwimu za ripoti ya mwisho wa mwaka ya Ewura inaonyesha kupungua kwa uagizaji wa mafuta ya taa kwa asilimia 28 mwaka 2020/2021 ikilinganishwa na mwaka 2019/2020.

"Mwaka 2019/2020 lita 38.47 milioni yaliingia nchini kabla ya kupungua Hadi lita 27.86 milioni mwaka 2020/2021," ripoti ya Ewura ya Mwaka 2021 imeonyesha.

EWURA MACH 2023
 
Nashangaa wanaosema watu hawatumii mafuta ya taa. Hata mimi nina majilo mengi ukitak hata video natuma

1. Jiko la mchina - Hili hutumika sana kupikia vitu vya mda mrefu kwa sababu nina familia ndogo vinaiva fasta mfano uji wa ulezi, nyama, maharage, kande nk
Huwa nanunua dumu kita 20

2. Jiko la Gas - Hili huwa linatumika sana kuunga mboga za majani, kupika mayai, chai, kukaanga nyama nk
Nanunua mtungi oryx kg 15

3. Jiko la Mkaa - Huwa nalitumia kupika wali na pilau endapo umeme hakuna. Huwa nanunua mkaa gunia

4. Rice cooker - Natumia rice cooker kupika wali na pilau tu
Linatumia umeme

5. Pressure cooker- Mara nyingi hili linatumiwa kwa kupika sana sana supu na viazi roast
Linatumia umeme

6. Jagi za kuchemsha maji - Haya yapo mawili moja la kuchemsha maji ya kuogea. Sikutaka kuweka heater nyumba ina vifaa vingi vya umeme very dangerous. Yapo matatu ila moja ndio la lita 25 kwa ajili ya kuchemsha maji ya kunywa


7. Jiko koa - Hili huwa linatumika nadra sana kupikia lipo lipo tu

8. Convention oven - Kazi yake ni kuchoma nyama, viazi, mihogo na ndizi
Hutumia umeme

9. Slow cooker - Hii inatumika kupashia chakula moto na kuipa mboga taste aisee ukiweka mchuzi humu kwenye slow cooker nyama zinalaika vizuri na zinataste vizuri

Sina: Oven + microwave + induction cooker, planning to buy in the future

Kufupisha jiko la mchina ndio jiko linalotumika sana tena hususani vyakula vya kukaanga kaanga kama ndizi za mzuzu, nyama za kukaanga nk. Kwa hiyo kusema kuwa hayatumiki ni nyinyi ambao hamtumii ila kwa sisi huwa tunayatumia bado. .

La ziada: Gharama huwa nafuu sana ukiwa na majiko tofauti kwa mapishi tofauti tofauti. .
 
Nashangaa wanaosema watu hawatumii mafuta ya taa. Hata mimi nina majilo mengi ukitak hata video natuma

1. Jiko la mchina - Hili hutumika sana kupikia vitu vya mda mrefu kwa sababu nina familia ndogo vinaiva fasta mfano uji wa ulezi, nyama, maharage, kande nk
Huwa nanunua dumu kita 20

2. Jiko la Gas - Hili huwa linatumika sana kuunga mboga za majani, kupika mayai, chai, kukaanga nyama nk
Nanunua mtungi oryx kg 15

3. Jiko la Mkaa - Huwa nalitumia kupika wali na pilau endapo umeme hakuna. Huwa nanunua mkaa gunia

4. Rice cooker - Natumia rice cooker kupika wali na pilau tu
Linatumia umeme

5. Pressure cooker- Mara nyingi hili linatumiwa kwa kupika sana sana supu na viazi roast
Linatumia umeme

6. Jagi za kuchemsha maji - Haya yapo mawili moja la kuchemsha maji ya kuogea. Sikutaka kuweka heater nyumba ina vifaa vingi vya umeme very dangerous. Yapo matatu ila moja ndio la lita 25 kwa ajili ya kuchemsha maji ya kunywa


7. Jiko koa - Hili huwa linatumika nadra sana kupikia lipo lipo tu

8. Convention oven - Kazi yake ni kuchoma nyama, viazi, mihogo na ndizi
Hutumia umeme

9. Slow cooker - Hii inatumika kupashia chakula moto na kuipa mboga taste aisee ukiweka mchuzi humu kwenye slow cooker nyama zinalaika vizuri na zinataste vizuri

Sina: Oven + microwave + induction cooker, planning to buy in the future

Kufupisha jiko la mchina ndio jiko linalotumika sana tena hususani vyakula vya kukaanga kaanga kama ndizi za mzuzu, nyama za kukaanga nk. Kwa hiyo kusema kuwa hayatumiki ni nyinyi ambao hamtumii ila kwa sisi huwa tunayatumia bado. .

La ziada: Gharama huwa nafuu sana ukiwa na majiko tofauti kwa mapishi tofauti tofauti. .
Umenirusha roho, nilikuwa na majiko ya mchina nimeyatupa daah.
 
Umenirusha roho, nilikuwa na majiko ya mchina nimeyatupa daah.
Kwa nini utupe?

Mda mwingine yanasaidia sana. Nakupa kazi nunua nyama kilo na chemsha nyama nusu kwenye gas na nusu kwenye mchina halafu uje uniqmbie ipi ni tamu zaidi 😃
 
Back
Top Bottom