Mafuta ya taa kwenye chakula mashuleni

Mafuta ya taa kwenye chakula mashuleni

Full charge

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2018
Posts
1,712
Reaction score
1,661
Wadau wa jf hivi nisahihi chakula anachokula binadamu kutiwa mafuta ya taa? Kama hamna je wanaotufanyia hivyo mashuleni kwetu kwa lengo la kutupunguza mihemuko wanapata wapi kibali hicho(uongozi mzima wa shule)je mafuta hayo yamethibitishwa na wataalam na kugundua kuwa hayana athari kwa binadamu? Je serikali inalitambua hilo? Kama ndiyo, inachukua hatua gani kwa wahusika? Naombeni mawazo yenu ndugu zanguni wa jf.
 
Nasikia hiyo inawapunguzia hamu ya kujamiiana wanafunzi
 
Mkuu wewe binafsi umewahi kushudia wanaweka hayo mafuta kwenye chakula.

R.I.P Father wa Minaki.
 
mkuu wa shule niliyopitia popote ulipo nakupongeza sana, wewe ulipinga huo upuuzi na ulituletea disco vumbi tena la usiku na baada ya nusu saa walibaki walimu peke yao pale chini ya mti wa Tambiko......baada ya wiki mbili mimba 40
 
Kiukwel nimeshudia pia kinachofanyika ni kwamba chakula chenyewe kinakuwa na mafuta hayo
 
Wadau wa jf hivi nisahihi chakula anachokula binadamu kutiwa mafuta ya taa? Kama hamna je wanaotufanyia hivyo mashuleni kwetu kwa lengo la kutupunguza mihemuko wanapata wapi kibali hicho(uongozi mzima wa shule)je mafuta hayo yamethibitishwa na wataalam na kugundua kuwa hayana athari kwa binadamu? Je serikali inalitambua hilo? Kama ndiyo, inachukua hatua gani kwa wahusika? Naombeni mawazo yenu ndugu zanguni wa jf.
kama yamekusaidia kuondoa mihemko yako shida iko wapi?, sio kila sumu ni mbaya kwako, itategemea na ukubwa wa dozi/kiwango, afya ya mtumiaji, umri wa mtumiaji, na frequency ya utumiaaji. Hata sumu ya nyoka ikiwa kidogo mwilini ni kinga ya mwili, hata baadhi ya chanjo unazoziona ni zinatengenezwa na wadudu wa maradhi husika, usijali mdogo wangu, kuwa na amani mladi wasiweke debe zima kwenye chakula.
 
Bila hiyo kama ni boys tupu lazima usodoma ukithiri,kuna age ya balehe apo niyakuangalia sana
 
Cha kushangaza ugonjwa ule wa kuchekecheka kwa wasichama mashuleni umetoweka kabisa.
 
Je ni salama kwa afya ya binadamu?
Ni kinyume cha haki za binadamu kuzuia mihemuko kwakuwa hiyo ni nature hivyo kuzuia ni unyanyasaji wa asili ya binadamu. Baadaye watoto wakiwa watu wazima wakiwa wavivu kama panda mtaanza kulalamika kwakuwa watakuwa hawazaliani kwakukosa mihemko matokeo yake watakuwa wanalala tu hata wakioana badala ya kushughuli na kuijaza dunia, Aliyeweka mihemuko hakuwa mjinga
 
tumekula sana chakula chenye mafuta ya taa huko boarding, sometimes yalikua yananukia kabisa hadi appetite inakata. tukilalamika wanaacha siku kadhaa alaf wanarudia tena kama kawaida. pocket money ni muhimu sana kama unamtoto yupo bweni.
 
Aaah hayo mambo nilikutana nayo Ndanda sekondari, siku moja mafuta yalizidi mpk tukaombwa msamaha
 
kama yamekusaidia kuondoa mihemko yako shida iko wapi?, sio kila sumu ni mbaya kwako, itategemea na ukubwa wa dozi/kiwango, afya ya mtumiaji, umri wa mtumiaji, na frequency ya utumiaaji. Hata sumu ya nyoka ikiwa kidogo mwilini ni kinga ya mwili, hata baadhi ya chanjo unazoziona ni zinatengenezwa na wadudu wa maradhi husika, usijali mdogo wangu, kuwa na amani mladi wasiweke debe zima kwenye chakula.
duu debe zima
 
mafuta huwa hawaweki hilo ninauhakika, chanzo cha halufu hiyo ni utunzaji mbovu wa unga wanaposaga hasa kama mahindi yamesangwa kwenye mashine za mafuta ya dizeli
 
Back
Top Bottom