Mafundi wa Tanzania mtabadilika Lini?

Mafundi wa Tanzania mtabadilika Lini?

MIGUGO

JF-Expert Member
Joined
Dec 3, 2011
Posts
2,137
Reaction score
3,942
Ikiwa Tanzania inaelekea kuwa nchi ya viwanda kama wasemavyo wangu ni wakati wa mafundi (fundi ujenzi,welding,umeme,fenicha nk) kuacha umagumashi.

Mafundi wa mitaani waongo,wezi,matapeli,wadhurumat,hawana bei standard,wanalipua kazi,hawafanyi kwa wakati.Yaani wamekaa kiujanjajanja.Mafundi badilikeni.

Hatutakuja kuendelea maana unakuta mfano kitu flani kumeharibika kinahitaji repair kidogo.Ni bora hata ununue kipya,vinginevyo itakugharimu sana.Wengi hususiwa na wateja wao.Ni bora ununue kabati mchina fomeka kuliko kukimbizana na fundi.

Ingekuwa vizuri huko vyuoni kama VETA wafundishe ethics za fundi.

Wadau mnasemaje?
 
Nitafute Mimi kwa kazi zote Za ufundi, u will never regret
 
Daah sijawahi kufanyiwa kazi vizuri na fundi cherehani (fundi nguo) nimeamua kujifunza ili niwe najishonea mwenyewe. Huo ujanja ujanja wa hawa mafundi ni fursa kubwa sana ya mtu kupiga hela. Unafanya yale ambayo yabawashinda na kujipigia hela unavyotaka.
 
Daah sijawahi kufanyiwa kazi vizuri na fundi cherehani (fundi nguo) nimeamua kujifunza ili niwe najishonea mwenyewe. Huo ujanja ujanja wa hawa mafundi ni fursa kubwa sana ya mtu kupiga hela. Unafanya yale ambayo yabawashinda na kujipigia hela unavyotaka.
Nimekumbuka msemo wa mzee mmoja kuwa kila mwanaume lazima awe na toolbox nyumbani kwake.Sio kila kitu unamwita fundi
 
Hili suala haliko kwa mafundi tu mkuu..hata watu au sehemu usizofikiria. UAMINIFU na UADILIFU ni mtihani sana hapa Bongo.

Niliwahi kupeleka saa yangu kwa matengenezo katika duka moja maarufu sana maeneo ya mjini karibu na askari monument. Nilipofika pale nikakuta wahindi wawili mtu na baba yake...na mafundi wa kibongo wako pembeni.

Wakaichukua saa waangalie tatizo ni nini. Baada ya muda kidogo yule Muhindi (Mtoto) akanifuata na kunijulisha ile saa imekufa utumbo...kwa hivyo gharama ya kuweka mashine mpya ilikuwa Tsh 400,000/=....niliishiwa nguvu palepale. Maana hiyo saa thamani yake mpya haikufika hiyo bei ya marekebisho.

Nilichofanya nilitoka kwa nje pembeni kuna fundi viatu. Na mimi nikatumia akili yangu ya Kitanzania nikapata namba ya yule fundi mtaalam wa pale ambaye ni Mbantu. Nikaelekezwa nimpigie simu baada ya saa 12 jioni. Nilifanya hivyo na kesho yake mapema nilikutana nae kabla hajaingia kazini nikamkabidhi saa. Jioni tukakutana akanikabidhi saa ikiwa inafanya kazi...nikamlipa 50,000/=. Akaniambia tatizo lilikuwa ni spring betri ilivuja ikapata hitilafu. Na haikuwa tatizo la kubadili mashine kama nilivyoelezwa awali.

Watanzania tunaumizwa kila kukicha. Ni kuwa makini tu.
 
Tatizo na mafundi wetu ni troubleshooting skills - uwezo wa kujua tatizo lipo wapi. Yupo fundi moja ameahangaika sana microwave oven iliogoma kuwaka. Isiwe taabu nimeirudisha nyumbani na kuzama intaneti -topic microwave oven repair. Kwa kifupi mlango microwave unao safety switch inayozuia microwave kuwaka iwapo mlango haujafunga vizuri(hatari ya miale ya microwaves kumdhuru mtumiaji). Mlango ulikuwa umepinda kidogo hivo switch hai engage. Baada ya kunyosha mlango kidogo oven linafanya kazi hadi leo hii.
 
Halafu kuna kitendo flani cha mafundi wengi hasa hawa wa vitu vya umeme mfano television, Ukimpelekea na kumwambia tatizo utamuona kaifungua halafu katoa kifaa flani halafu anaanza kukigongagonga na bisibisi sambamba na kukipuliza

Sasa ukijaribu kuangalia anachokifanya hapo mara nyingi ni ujanja ujanja tu na maneno mengi, mwisho wa matengenezo atakutaja bei ya ajabu ajabu tu ilhali alichofanya hapo huoni kama kina thamani hiyo..mafundi tunawahitaji lakini sometimes mnakosa ukweli na uaminifu kwenye kazi zenu
 
Wahenga walisema Fundi ni mbuzi tu anakula majani anakunya Karanga
Ikiwa Tanzania inaelekea kuwa nchi ya viwanda kama wasemavyo wangu ni wakati wa mafundi (fundi ujenzi,welding,umeme,fenicha nk) kuacha umagumashi.

Mafundi wa mitaani waongo,wezi,matapeli,wadhurumat,hawana bei standard,wanalipua kazi,hawafanyi kwa wakati.Yaani wamekaa kiujanjajanja.Mafundi badilikeni.

Hatutakuja kuendelea maana unakuta mfano kitu flani kumeharibika kinahitaji repair kidogo.Ni bora hata ununue kipya,vinginevyo itakugharimu sana.Wengi hususiwa na wateja wao.Ni bora ununue kabati mchina fomeka kuliko kukimbizana na fundi.

Ingekuwa vizuri huko vyuoni kama VETA wafundishe ethics za fundi.

Wadau mnasemaje?
 
Ikiwa Tanzania inaelekea kuwa nchi ya viwanda kama wasemavyo wangu ni wakati wa mafundi (fundi ujenzi,welding,umeme,fenicha nk) kuacha umagumashi.

Mafundi wa mitaani waongo,wezi,matapeli,wadhurumat,hawana bei standard,wanalipua kazi,hawafanyi kwa wakati.Yaani wamekaa kiujanjajanja.Mafundi badilikeni.

Hatutakuja kuendelea maana unakuta mfano kitu flani kumeharibika kinahitaji repair kidogo.Ni bora hata ununue kipya,vinginevyo itakugharimu sana.Wengi hususiwa na wateja wao.Ni bora ununue kabati mchina fomeka kuliko kukimbizana na fundi.

Ingekuwa vizuri huko vyuoni kama VETA wafundishe ethics za fundi.

Wadau mnasemaje?
huhuu fundi ambaye hana magumashi ni kinyozi tuu maana waondoka ukiwa ushanyolewa wengine wotw magumash
 
Kuwa funding raha sana unawabamiza Wateja maana hawajui vitu vya kisayansi wakileta Gari fungua bonet mwambie cabuleta, otaneta na sensa vimeharibika. Kama ni redio utasikia transista zimeungua, halafu utaona funding anafungua nati zote anaweka kifaa pembeni anakwambia njoo kesho kutwa.
 
Kuwa funding raha sana unawabamiza Wateja maana hawajui vitu vya kisayansi wakileta Gari fungua bonet mwambie cabuleta, otaneta na sensa vimeharibika. Kama ni redio utasikia transista zimeungua, halafu utaona funding anafungua nati zote anaweka kifaa pembeni anakwambia njoo kesho kutwa.
Mafundi wa Kenya proffessinal zaidi. Anafungua kifaa anafanya uchunguzi(unalipia uchunguzi), halafu pale pale anakwambia hiki hiki kibovu. Inayo hiari kwenda kununua spare au unamwachia hela ashugulikie. Nimedili na mafundi Kenya mara ya kwanza TV na ya pili DVD player. Nimepeleka mzigo asubuhi amini usiamini kabla mchana napigiwa simu niende kuchukua mzigo!
 
Fundi aliyeniacha hoi alipelekewa mbao 8 zikiwa bado hazijakauka vizuri sasa baada ya wiki kadhaa jamaa akafuatilia kufika kwa fundi mbao zimebaki 4 kumuuliza fundi mbao mbona zimebaki 4? Fundi baada ya kukauka vizuri zimebaki hizo jamaa akabaki anacheka tu asijue hata la kumfanya?
 
hata ma contractor hawana bei standard wanatofautiana experience, quality na hata mahitaji yako. pia nafkiri hoja pekee sio kwa fundi peke yake bali hata mhusika unam treat vp fundi. mmekubaliana kazi mil 1, unamlipa laki 5 na haja anza kazi, kesho akikosa hela ya kuwalipa vibarua wake unalalamika.
 
Niliwahi peleka simu kwa fundi, Basi nilizungushwa mpaka nikaamua kumuuzia kama spare tu.
 
Back
Top Bottom