Mafundi wa Tanzania mtabadilika Lini?

Mafundi wa Tanzania mtabadilika Lini?

Kuna aya katika quran inasema "usimwamini ila aliyeshika dini yako kisawasawa" sasa unapeleka kitu kwa fundi ambaye hana dini si Muislamu wala Mkristo yaani fundi awe ndo kirang.a unatarajia nini kama si kuibiwa.
 
Ikiwa Tanzania inaelekea kuwa nchi ya viwanda kama wasemavyo wangu ni wakati wa mafundi (fundi ujenzi,welding,umeme,fenicha nk) kuacha umagumashi.

Mafundi wa mitaani waongo,wezi,matapeli,wadhurumat,hawana bei standard,wanalipua kazi,hawafanyi kwa wakati.Yaani wamekaa kiujanjajanja.Mafundi badilikeni.

Hatutakuja kuendelea maana unakuta mfano kitu flani kumeharibika kinahitaji repair kidogo.Ni bora hata ununue kipya,vinginevyo itakugharimu sana.Wengi hususiwa na wateja wao.Ni bora ununue kabati mchina fomeka kuliko kukimbizana na fundi.

Ingekuwa vizuri huko vyuoni kama VETA wafundishe ethics za fundi.

Wadau mnasemaje?

Yaani Mkuu umegusia kitu kinachonitatiza kwa mda mrefu. Mafundi wengi ambao nimekutana nao..Kiukweli ni wababaishaji....kazi hawafanyi za kiwango.. hata kama you are willing to pay a fortune! wanaweka hela mbele na ukishamlipa hutamuona tena. Mfano juzi kati nilitaka kuchonga kabati la nguo..yaani I had terrible experience. Sasa najiuliza hawa ndugu zetu wataishije mjini? au ndo ule mwendo wa kulalamika tuu. Eti hela imepotea.

In Tanzania (atleast areas I know) si rahisi mtu akuulize fundi na um-recommend with confidence. Yaani sijui kwa nini ila hii fani nzima ya ufundi ni kama ina matatizo and I feel we are running out of time. Yaani tunalalamika kila siku eti wachina na wakenya wanachukua fursa lakini kiuhalisia hawa wenzetu wana commitment ya ajabu kwa kazi zao. Juzi kati nilichonga madirisha kwa mchina! You cant believe nililipa hela nyingi but I felt completely satisified! Na mchina anakwambia kabisa kama kazi hujaipenda au imekosewa..gharama ni zangu.

Kwa kweli waTanzania wenzangu tujifunze kuwa aggressive tuache politicking na mawazo ya kupata pesa bila kufanya kazi. Hela ambayo nimempa mchina ningempa mTanzania I am sure ingebadilisha maisha yake.

I repeat silaha kubwa ya fundi ni ubora wa bidhaa na uaminifu!
 
Sasa kwa haya yote wataishia kuwa wa viraka na repair ambayo Inaua ubunifu.

Wanatakiwa wajufunze kutroubleshoot kama Jamaa hapo alivyosema.

Research pia ni muhimu sio anaquote bei ambayo si rafiki kwa pande zote.
 
hata ma contractor hawana bei standard wanatofautiana experience, quality na hata mahitaji yako. pia nafkiri hoja pekee sio kwa fundi peke yake bali hata mhusika unam treat vp fundi. mmekubaliana kazi mil 1, unamlipa laki 5 na haja anza kazi, kesho akikosa hela ya kuwalipa vibarua wake unalalamika.

Poor excuse Mkuu. Then you have to learn to negotiate. Na kama nimekuumiza bei..well tell me in my face..mzee hii pesa unayoitoa hutapata kazi ya kiwango unayoitaka. So the choice is yours. Otherwise wengi tumekuwa wababaishaji. Na unajua hata mhitaji wa huduma anakulipa kutokana na anavyokuona, previsous kazi zako etc.

Hivi mfano nataka fundi wa tiles...ananiambia mzee kazi yangu niliyoifanya ni pale Serena hotel au nilibandika Tanga stones pale mlimani city...(mfano)...hivi unajua hata ku-mapproach mtu kama huyo itabidi nijipange? kwa sababu I know he represents quality.

Always, binadamu ndo ana determine value yake.
 
Wale unaojuana nao utakuta wanalalamika ukimpa kazi mtu mengine.Utaskia "boss umeninyima fursa mi wa mtaani kwako "
 
Wale unaojuana nao utakuta wanalalamika ukimpa kazi mtu mengine.Utaskia "boss umeninyima fursa mi wa mtaani kwako "
Tena hawa ndio usiseme mkuu. Nilimpa tenda kijana wa mtaani kunijengea kibanda kidogo cha kuku wa kienyeji wa kula nyumbani. Eeeeh bwana weee...nilikoma. Utafikiri nilikuwa najenga mradi wa uDART.
 
Mafundi wa Kenya proffessinal zaidi. Anafungua kifaa anafanya uchunguzi(unalipia uchunguzi), halafu pale pale anakwambia hiki hiki kibovu. Inayo hiari kwenda kununua spare au unamwachia hela ashugulikie. Nimedili na mafundi Kenya mara ya kwanza TV na ya pili DVD player. Nimepeleka mzigo asubuhi amini usiamini kabla mchana napigiwa simu niende kuchukua mzigo!
wakisoma comment yako watajifunza sio kila wakipokea kazi cha kwanza ni kuomba advance
 
Nipeni mimi kazi za umeme wa nyumba yoyote ile...U will never regret..Im honest and I have much experience in that field...
 
Kiukweli hawa wanaojiita mafundi wanakera sana ni kweli kuna wkt hata huwezi kufikiria kumrecommend kwa mtu mnayeheshimiana.

Kuna mmoja tulikubaliana atengeze geti akasema atahitaji wiki mbili. Nilipata geti baada ya miezi 5 tena chini ya usimamizi wa polisi.
Kuna mwingine alitengeneza milango na mie nilikuwa safari sikupata muda wa kuona kazi. Akaniambia amekamilisha kazi nimpe chake.

Nikamwuuliza mara mbilimbili kama kweli alikamilisha kazi. Akadai ndio, nikamlipa hela yake. Nimerudi nakuta kazi haikwisha kama jamaa alivyonihakikishia kwenye simu. Nampigia ananiambia nitakuja kumalizia, sijamwonaga tena!!
 
Tena wengine wanatabia ya kuchomoa vifaa kwenye bidhaa ya mteja halafu wanauza.
Unapeleka kifaa kina tatizo moja unakuja kuambiwa kasoro zaid ya mbili jua kishauzwa umewekewa kibovu.
 
mkuu hongera kwa thread hii, miye laptop yangu sijui imekufa sababu ya mafundi njaa maana nimerudisha nyumbani baada ya kupita kwa mafundi watatu tofauti wote kinachofanyika ni try and error
 
Kama ndugu zangu mlio kwenye ujenzi ndio mnaumia kweli maana ninavyowasikia huku mitaani wanavyojisifia mimi mpaka napata hasira kabisa.....

Kwanini ndugu zangu msifanye hata window shopping ya vifaa hivyo at least hata wiki mbili kabla ya ujenzi wako.....

Unaenda dukani na fundi ndio huko huko anakwenda kukumaliza....maana wale jamaa maduka mengi wanafahamika....wanafanya wizi huo wakishirikiana na vijana wa dukani wasio waaminifu.....yaani kifaa cha elfu mbili unaweza ukaambiwa elfu kumi......kifaa cha elfu kumi unaambiwa elfu ishirini......

Ukimuuliza fundi lazima atakuelekeza kwenye duka la mwizi mwenzie....yaani wewe upo njiani wenzako wameshapigiana simu kuwa uchinjwe tu......

Ushauri wangu

Usiende kwenye duka la fundi mliloelewana au mtume mtu kesho yake aende akaulizie bei alafu ulinganishe na bei uliyoambiwa.....

Kama ukienda kwenye duka alilokuambia usinunue vitu siku hiyo hiyo ulizia tu bei........

Jitahidi ujue mahitaji ya ujenzi wako kabla ya kumuita fundi au kabla hujaanza ujenzi......

Unaweza ukamuita fundi aje akufanyie vipimo vya mradi wako na mahitaji ya vifaa huku ukimsisitizia kuwa bado hujajipanga kuanza ujenzi hivi karibuni....hiyo itamvunja moyo fundi na kukupa vipimo vya uhakika na mahitaji halisi ya vifaa vyako.....

Baada ya hapo kama huna haraka anza kununua mwenyewe vifaa taratibu....na ukifika huko madukani usigande sana na bei za duka moja...tembelea maduka mengi ili upate unafuu wa bei.....

NB; Kinachowaponza mafundi ni tamaa...
 
Kingine naona ndo ule wa ushauri wa Magufuli kwamba wote tupewe risit za EFD. kwa hizi risiti wizi utapungua. By the way hata sisi baadhi yetu clients tunapenda Magumashi. Please tujifunze kusacrifice tuingie gharama tupate vitu vizuri. Ila kwa sasa kama ni kazi serious Kiukweli Mchina anahusika. Ingawa naumia hiyo hela ningempa mswahili mwenzangu lakini....I am not prepared ku-spend 20 or 30 million on a poor product! Uzalendo unanishinda kwa hili.
 
1473910987776.jpg
 
kumrecommend mtu unayeheshimiana nae kwa fundi x, then yule fundi analeta uwongo uwongo, kuzungushana, mwishowe wote mnaonekana makajanja. mnashindwa hata kuangaliana.
 
Wakuu hao mnaowalalamikia ni vijana wanaofanya kazi kimazoea they Haven't enough skills to perform technically issue but in real mafundi tuliokaa darasani tunafahamu ethtics za Kifundi Uaminifu ni mkubwa na ubabaishaji ni kidogo sana mana hakuna kitu chenye 100% efficiency, Watanzania tuache kuwapa kazi unskilled technian hao wanafanya kimazoea na wana under standardize quality ya product, Gadget or Devices, I'm proud to be Technian
 
Back
Top Bottom