Mafundi lini mtabadilika?

Mafundi lini mtabadilika?

BABA E's

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2012
Posts
354
Reaction score
136
Mbona kila fundi ni muongomuongo tu, tapelitapeli tu.
Uwe fundi nguo, fundi ujenzi, ukishaitwa fundi tu ni kama vile laana, why?
Kwanini mpo hivyo?
Kwanini mnaharibu sifa zenu?
Tatizo ni nini?
 
Fundi mbao ni noma unakuta material uliyolipia anatumia kufanyia kazi ya mtu mwingine ambae alishakula hela ya material yake yani pesa yako ndiyo inatumika kureplace pesa ya watu aliyotafuna na hapo inabidi akukwepe mnoo mpaka apate mteja mwingine atakayempa pesa ya material mengine ndiyo atafanyia kazi yako yani ni chain wateja mnategemeana.
 
Fundi kinyozi?
Kuna kinyozi anaita makos alimnyoa polisi nusu alafu akamwambia hebu naomba malipo kabisa shemeji yako akanunue mafuta aendelee kupika. Polisi akampa hela jamaa akatoroka akaenda kunywa gongo hajarudi tena, yule askari ikabidi aingie kazini akiwa kanyolewa nusu na kumlazimu kuvaa likofia mwanzo mwisho maana ilikua ndiyo muda wa kureport kazini hakua na uwezo wa kwenda kumalizia saloon nyingine.

Kuanzia hapo simuamini hata kinyozi.
 
Mbona kila fundi ni muongomuongo tu, tapelitapeli tu.
Uwe fundi nguo, fundi ujenzi, ukishaitwa fundi tu ni kama vile laana, why?
Kwanini mpo hivyo?
Kwanini mnaharibu sifa zenu?
Tatizo ni nini?
Kwa mtazamo wangu.
Hawana utaratibu wa kupokea kazi,pengine kutokana na uhaba au kutokuwa na uhakika wa kazi, wanachukua kazi nyingi kwa wakati mmoja.
Kutokana na uhaba wa vitendea kazi na kukosekana mpangilio wa ufanyaji kazi, kazi huchukua muda mrefu, ukizingatia na wingi wa kazi za watu alizonazo, hawezi kutoa muda atakaomaliza kazi yako.
 
Mbona kila fundi ni muongomuongo tu, tapelitapeli tu.
Uwe fundi nguo, fundi ujenzi, ukishaitwa fundi tu ni kama vile laana, why?
Kwanini mpo hivyo?
Kwanini mnaharibu sifa zenu?
Tatizo ni nini?
Sio wote tuko hivo
 
Back
Top Bottom