miss confidence
JF-Expert Member
- Jul 9, 2016
- 393
- 273
Heshima zenu wana JF.
Katika harakati za kuendelea kukomesha tabia ya ubadhilifu wa Mali za umma mnamo tarehe 13 mwezi wa sita katika Bunge la serikali ya wanafunzi chuo kikuu cha dar es salaam (DARUSO- Mlimani campus) mbunge wa viti maalumu kutoka ndaki ya insia / College of Humanities (COHU) mwaka wa kwanza Mh Halima Juma John aliwasilisha hoja binafsi kuhusu ubadhilifu wa fedha za DARUSO katika serikali iliyopita 2016/2017 na hoja hiyo iliungwa mkono na wabunge wote wa bunge la DARUSO chini ya spika wa bunge hilo Mh Deogratius Mahinyila na kwa pamoja kama bunge waliadhimia uundwaji wa kamati maalumu ya kufuatilia ubadhilifu huo kama ulivyo bainishwa na Mh Halima Juma John katika hoja yake Bungeni.
Kamati ilipewa wiki mbili kwaajili ya kukamilisha majukumu yake ya kufuatilia mapato na matumizi ya DARUSO kwa mwaka wa masomo 2016/2018 ambapo kamati ilibaini ufisadi mkubwa sana uliofanywa na viongozi wa serikali ya DARUSO ya mwaka 2016/2017 iliuokuwa chini ya rais Leon Erasim... Baadhi ya mawaziri waliokumbwa na hatia katika ripoti ya kamati hiyo ni aliyekuwa waziri wa katiba na sheria DARUSO ndugu Boniventure Erick, aliyekuwa waziri mkuu wa DARUSO ndugu Boniphace Emmanuel, waziri wa fedha ndugu Gamba na aliyekuwa kaimu wa wizara ya mikopo Ndugu Makupa..
Ripoti imebainisha watu hawa wameiba zaidi ya milioni 20 za wana DARUSO kitu ambacho ni kinyume cha katiba ya DARUSO na katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania.
Naambatanisha na ripoti hiyo hapa chini wana JF muone jinsi gani mafisadi ya nchi hii tunavyokuwa nayo tangu huku chini na panapo fikia ngazi ya juu yanakuwa majizi yaliyokubuhu.
Katika harakati za kuendelea kukomesha tabia ya ubadhilifu wa Mali za umma mnamo tarehe 13 mwezi wa sita katika Bunge la serikali ya wanafunzi chuo kikuu cha dar es salaam (DARUSO- Mlimani campus) mbunge wa viti maalumu kutoka ndaki ya insia / College of Humanities (COHU) mwaka wa kwanza Mh Halima Juma John aliwasilisha hoja binafsi kuhusu ubadhilifu wa fedha za DARUSO katika serikali iliyopita 2016/2017 na hoja hiyo iliungwa mkono na wabunge wote wa bunge la DARUSO chini ya spika wa bunge hilo Mh Deogratius Mahinyila na kwa pamoja kama bunge waliadhimia uundwaji wa kamati maalumu ya kufuatilia ubadhilifu huo kama ulivyo bainishwa na Mh Halima Juma John katika hoja yake Bungeni.
Kamati ilipewa wiki mbili kwaajili ya kukamilisha majukumu yake ya kufuatilia mapato na matumizi ya DARUSO kwa mwaka wa masomo 2016/2018 ambapo kamati ilibaini ufisadi mkubwa sana uliofanywa na viongozi wa serikali ya DARUSO ya mwaka 2016/2017 iliuokuwa chini ya rais Leon Erasim... Baadhi ya mawaziri waliokumbwa na hatia katika ripoti ya kamati hiyo ni aliyekuwa waziri wa katiba na sheria DARUSO ndugu Boniventure Erick, aliyekuwa waziri mkuu wa DARUSO ndugu Boniphace Emmanuel, waziri wa fedha ndugu Gamba na aliyekuwa kaimu wa wizara ya mikopo Ndugu Makupa..
Ripoti imebainisha watu hawa wameiba zaidi ya milioni 20 za wana DARUSO kitu ambacho ni kinyume cha katiba ya DARUSO na katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania.
Naambatanisha na ripoti hiyo hapa chini wana JF muone jinsi gani mafisadi ya nchi hii tunavyokuwa nayo tangu huku chini na panapo fikia ngazi ya juu yanakuwa majizi yaliyokubuhu.