sulphadoxine
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 2,257
- 644
Nimkakati wa kuzuia kesi nzito za rushwa kuchunguzwa.
MKAKATI mzito unaandaliwa kumtisha Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk. Edward Hoseah, kwa nia ya kuzuia ukamilishwaji wa kesi nzito za ufisadi zinazochunguzwa na taasisi hiyo, baadhi ya mikakati hiyo ikielezwa kutumia vikao vya Bunge, imefahamika.
Habari kutoka Dodoma na Dar es Salaam zimeeleza kwamba tayari
watuhumiwa wakuu wa ufisadi wamekwishaandaa watu maalumu kutumia vikao vya Bunge vinavyoendelea mjini Dodoma kuwasilisha ujumbe utakaommaliza ama kumtisha Dk. Hoseah kwa nia ya kumpunguzia kasi ya kushughulikia majalada ya ufisadi.
Dk. Hoseah ambaye watuhumiwa wa ufisadi wamemuelezea kama mtu asiyetabirika, amekataa kuzungumzia mikakati hiyo alipohojiwa na Kulikoni hivi karibuni akielezea kwamba amezoea kukabiliana na
changamoto nyingi katika kazi zake na kwamba anachojitahidi ni kutenda haki bila kujali mamlaka na dhamana ya mtu kisiasa.
Sina taarifa za mikakati ya kunichafua, lakini nafahamu kwamba watu wanaojijua kuwa si wasafi wamechanganyikiwa na hakuna ajabu kusikia kwamba wanaingia gharama kunichafua. Ninachoweza kuwahakikishia Watanzania wenzangu ni kwamba nitawatumikia kwa uadilifu na nitatenda haki bila kujali nafasi ya mtu katika jamii, anasema Hoseah.
Source:Gazeti la kulikoni la leo tarehe 1-7 july 2011
MKAKATI mzito unaandaliwa kumtisha Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk. Edward Hoseah, kwa nia ya kuzuia ukamilishwaji wa kesi nzito za ufisadi zinazochunguzwa na taasisi hiyo, baadhi ya mikakati hiyo ikielezwa kutumia vikao vya Bunge, imefahamika.
Habari kutoka Dodoma na Dar es Salaam zimeeleza kwamba tayari
watuhumiwa wakuu wa ufisadi wamekwishaandaa watu maalumu kutumia vikao vya Bunge vinavyoendelea mjini Dodoma kuwasilisha ujumbe utakaommaliza ama kumtisha Dk. Hoseah kwa nia ya kumpunguzia kasi ya kushughulikia majalada ya ufisadi.
Dk. Hoseah ambaye watuhumiwa wa ufisadi wamemuelezea kama mtu asiyetabirika, amekataa kuzungumzia mikakati hiyo alipohojiwa na Kulikoni hivi karibuni akielezea kwamba amezoea kukabiliana na
changamoto nyingi katika kazi zake na kwamba anachojitahidi ni kutenda haki bila kujali mamlaka na dhamana ya mtu kisiasa.
Sina taarifa za mikakati ya kunichafua, lakini nafahamu kwamba watu wanaojijua kuwa si wasafi wamechanganyikiwa na hakuna ajabu kusikia kwamba wanaingia gharama kunichafua. Ninachoweza kuwahakikishia Watanzania wenzangu ni kwamba nitawatumikia kwa uadilifu na nitatenda haki bila kujali nafasi ya mtu katika jamii, anasema Hoseah.
Source:Gazeti la kulikoni la leo tarehe 1-7 july 2011