Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,499
- 113,609
Mkuu Morgan, kwanza naunga mkono hoja kuwa Masele amefanya kazi nzuri na Wanashinyanga bado wanamuhitaji hivyo asikatishwe tamaa na wasaka tonge, hata mimi binafsi Masele namkubali sana na niliwahi kumfagilia hapa*MAMBO 10 USIYOYAJUA KUHUSU JIMBO LA SHINYANGA MJINI (PARIS YA TANZANIA)JIMBO LA MH. STEPHEN MASELE(MB)*
Jimbo la shinyanga mjini ni moja ya mji wenye maendeleo ya mwendokasi chini ya uongozi wa mbunge kijana wa jimbo hilo Mh Stephen Julius Masele ambaye Pia ni Naibu Spika wa Bunge la Afrika( PAP).
Hakika mwenye macho haambiwi tazama, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni,Masele tumeona na tumeridhishwa na utendaji kazi wako.Hii ni kasi ya 5G ya maendeleo kutoka kwa mbunge kijana, msomi na mpenda maendeleo. Aluta kontinua Komredi Stephen Masele mbunge wa shinyanga mjini. Bado tunakuhitaji usikatishwe tamaa na wasaka tonge.
Sent using Jamii Forums mobile app
CHADEMA peleka Moshi Shinyanga ni ya CCMSafari hii hatiboi kwanza ana bifu na spika wa mabifu
Pili uchaguzi uluipita alibebwa safaru hii mziki ni mkali kwanza sisi kama Chadema lazima tulitwae jimbo kwa udi na uvumba
Unaweza kuwa sahihi...Lakini Mh. Masele akikosa jimbo hilo atafutiwe kazi nyingine...bado ana uwezo wa kusaidia kuiendeleza Tanzania tuitakayo...Masele hana chake hapo.
..Petrobas Katambi ndiyo mgombea wa ccm 2020.
Unaweza kuwa sahihi...Lakini Mh. Masele akikosa jimbo hilo atafutiwe kazi nyingine...bado ana uwezo wa kusaidia kuiendeleza Tanzania tuitakayo.
Mmmhhh..umemshauri vizuri Sana ... tatizo ni pale atakapokubali kuufanyia KAZI ushauri wako...atakuwa anathibitisha utata/conspiracy inayomkabili na alternative atakayoichukua...SASA sijui reaction itakuaje!?Mkuu Morgan, kwanza naunga mkono hoja kuwa Masele amefanya kazi nzuri na Wanashinyanga bado wanamuhitaji hivyo asikatishwe tamaa na wasaka tonge, hata mimi binafsi Masele namkubali sana na niliwahi kumfagilia hapa
Steven Masele atamkwe Shujaa wa Taifa! Ni kweli Balozi wa Uingereza ni Jasusi. To Hell with...!
Wanabodi, Ile siku Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhre. Stephen Masele, alipomtuhumu Balozi wa Uingereza nchini kwa tuhuma nzito za ujasusi!, nilipandisha uzi huu, Ujasusi wa Balozi wa Uingereza: Tanzania, Can We Stand?!.nikihofia Mhe. Masele kufanywa "kondoo wa kafara!". Baada ya tuhuma...www.jamiiforums.com
Lakini kwa vile hakuna hatimiliki ya jimbo lolote, wala hakuna mtu kuhodhi jimbo lolote, jambo la kwanza namshauri Masele, atengeneze 30 min video Documentary ya hayo mambo 10 uliyo eleza yawe kwenye Audio Visual, watu waone na wasikie. Kisha video hiyo irushwe kwenye TBC, ITV, Star TV, Channel Ten, na Azam TV kisha DVD zisambazwe zikiandamana na flash ya HD zigawiwe bure baa zote, hotels zote, saloons zote, sehemu zote za public na za starehe ili watu waone kilichofanyika.
Lengo la kufanya haya ni kitendo cha Masele kuonekana mwiba kwa bosi wake pale mjengoni Dodoma, na bosi wake na Mzee Baba ni dam dam hivyo it's possible no matter how good Masele is, hatapitishwa na chama chake, hivyo asipopitishwa, avuke upande wa pili, wananchi wake wamchague aendelee nao.
P
Unaweza kuwa sahihi...Lakini Mh. Masele akikosa jimbo hilo atafutiwe kazi nyingine...bado ana uwezo wa kusaidia kuiendeleza Tanzania tuitakayo.
Niliposoma umeandika Shinyanga haikuwa na shule ya Kidato cha Sita kabla ya Masele kuwa Mbunge, nikachana karatasi sikuendelea kusoma upuluzi mwingine.
Amekesha BakurutuNavokujua Morgan leo utakua umelewa chakali balimi,utakua umesumbua nahiyo lakimoja.masele hawezi kukuacha kavu
Sent using Jamii Forums mobile app
Nyambafu,hivi ulishawahi fika Paris au unaisikia tu ? Shinyanga kuna metro,tram,train?.Uliambiwa Paris kuna shule za primary hazina canteen ? Yaani Masele hajafanya lolote. Mwambie aendelee kuloga .Shelembi ndo alitakiwa awe mbunge wa Shy town. Masele akakatiza maisha ya Shelembi. 2020 Masele Out.
Umekula mavi gani wewe, umeme vijijini ni mradi wa REA siyo wa Masele, ujenzi wa zahanati na vituo vya afya ni miradi ya nchi nzima, hospitali ya Kolandoto ni bora siku zote hata kabla ya Masele kuwa mbunge, maji ya bomba kayakuta ambao ni mradi ulioanzishwa na Lowassa kipindi akiwa Waziri wa maji, mradi wa maji toka ziwa Victoria kwenda miji ya kahama na shinyanga, vijiji yanakopita mabomba hayo pia vilinufaika kama vile Mwantini, Nindo, Lyabusalu, Lyabukande na kwingineko. Hizo nyumba bora za makazi kwani kajenga yeye? Sehemu yenye unafuu wa starehe shinyanga ni moja tu level 04 kwani ni ya kwake? Mwambie Masele kwamba wana JF wamekupinga*MAMBO 10 USIYOYAJUA KUHUSU JIMBO LA SHINYANGA MJINI (PARIS YA TANZANIA)JIMBO LA MH. STEPHEN MASELE(MB)*
Jimbo la shinyanga mjini ama PARIS YA TANZANIA kama linavyojulikana na wenyeji wa mji huo ni moja ya mji wenye maendeleo ya mwendokasi chini ya uongozi wa mbunge kijana wa jimbo hilo Mh Stephen Julius Masele maarufu kama PUTIN ambavyo wananchi wake wamembatiza kwa ukimya wake wenye kishindo wakimfananisha na Vladimir Putin Rais wa Urusi. Masele ambaye Pia ni Naibu Spika wa Bunge la Afrika( PAP). Tujikumbushe shinyanga ya kabla ya Masele na shinyanga ya sasa chini ya Masele:-
Shinyanga kabla ya Masele:-
1. Barabara ya lami moja tu kutokea stesheni ya treni kwenda kuelekea Japanese kona.
2.Maji ya visima yenye rangi kama chai ya maziwa.
3. Hospitali moja tu ya mkoani hapakuwa na vituo vya afya na zahanati za kata.
4. Hapakuwa na shule ya SEKONDARI kidato Cha tano na sita na ufaulu ulikuwa chini sana.
5. Umeme ulikuwa mjini kati tu. Mji ulikuwa hauna mvuto ukilinganisha na sasa.
Shinyanga ya Masele(Paris ya Tanzania):-
1. Mitaa imepimwa na kupangwa, nyumba nzuri na makazi bora.
2. Mtandao wa Barabara nzuri za lami zinazopitika na zenye taa za barabarani wakati wa usiku.Leo hadi ndala kuna lami....sikuwahi kufikiria lami itafika upongoji.
3. Maji ya zima Victoria vijiji na mitaa yote
4. UMEME mitaa na vijijini.
5. Zahanati na vituo vya afya vyenye ubora wa huduma haswa kwa kina mama, wazee na watoto. Hospitali mpya ya rufaa Negezi,kituo Cha afya Cha kisasa Kambarage na kinajengwa kingine Ndembezi.
6. Shule za kata zenye ubora Shycom iliyoboreshwa, Uhuru iliyoboreshwa, Mwasele, Old Shinyanga, Ibadakuli kwa uchache.
7.Kituo bora cha kulea wazee wasiojiweza Kolandoto.
8. Kituo bora cha watoto wenye mahitaji maalumu(Albinos) Ibinzamata.
9. Makazi bora ya wananchi na nyumba za kisasa kwa wananchi na watumishi wa umma.
10. Watu wazuri wenye afya, Kumbi bora za Starehe na viwanja vya burudani.
Hakika mwenye macho haambiwi tazama, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni,Masele tumeona na tumeridhishwa na utendaji kazi wako.Hii ni kasi ya 5G ya maendeleo kutoka kwa mbunge kijana, msomi na mpenda maendeleo. Aluta kontinua Komredi Stephen Masele mbunge wa shinyanga mjini. Bado tunakuhitaji usikatishwe tamaa na wasaka tonge.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nyumbani kwake ni Ngokolo ambapo hata njia ya kuchepuka kuingia nyumbani kwake ni mashimbo kashindwa hata kuweka karavatiHivi kwa Shy,nyumbani kwake ni eneo gani?ili tujue kama ni mwananzengo mwenzetu.