ong'wafaza
JF-Expert Member
- Apr 30, 2012
- 252
- 108
Watu wengi wanashindwa maisha kwa kutoijua siri moja kubwa sana.
Kukopa kusiko na manufaa yoyote kuko kwa aina nyingi na pengine mtu anaweza kujidai kwamba mimi sijawahi kukopa na mwingine anaweza kujitapa kuwa ni mkopaji mzuri lakini pia mikopo yake yote anailipa kwa wakati na hadaiwi, kumbe ndiye ana madeni makubwa yasiyolipika.
Mkopo mbaya sana ambao ndio unawadumaza wengi kwenye harakati za kujiletea maendeleo ni mkopo wa muda. Pengine swali la kujiuliza ni je mtu anakopaje muda?.
Mtu anakopa muda kwa kutofanya jambo au shughuli sahihi kwa wakati sahihi.
Mfano unakuta mtu anatakiwa asafiri leo kwa ajili ya kufuata bidhaa fulani mahali fulani kwa ajili ya matumizi au biashara zake,lakini anaamua kuahirisha safari bila sababu za msingi na kusema atasafiri kesho yake.
Tukumbuke maisha hayasimami wala hayamngoji mtu huyo. Kesho ikifika unatokea msiba kwa jirani au anapatwa na dharura nyingine mpya hivyo anashindwa kuondoka na hivyo bidhaa aliyokuwa anakusudia kuifuata anashindwa kuipita kwa muda huo na hata akiipata baadaye anakuta kuna mabadiliko mengi yametokea ndani ya muda mfupi hata kupelekea bidhaa hiyo kukosa manufaa aliyotarajia kuyapata.
Matokeo yake mtu huyo anarudi nyuma kimaisha kwa sababu tu alikopa muda.
Kimsingi jamii inatakiwa ielewe kwamba muda ni mali, hivyo kuukopa au kuupoteza bure unaweza kukusababishia kupata hasara kubwa.
Watanzania tujitahiti kutokopa muda na tuzingatie usemi usemao LINALOWEZEKANA LEO LISINGOJE KESHO .
Hii ndio siri ya mafanikio katika maisha.
Je, wewe hujawahi kukopa muda?
Kukopa kusiko na manufaa yoyote kuko kwa aina nyingi na pengine mtu anaweza kujidai kwamba mimi sijawahi kukopa na mwingine anaweza kujitapa kuwa ni mkopaji mzuri lakini pia mikopo yake yote anailipa kwa wakati na hadaiwi, kumbe ndiye ana madeni makubwa yasiyolipika.
Mkopo mbaya sana ambao ndio unawadumaza wengi kwenye harakati za kujiletea maendeleo ni mkopo wa muda. Pengine swali la kujiuliza ni je mtu anakopaje muda?.
Mtu anakopa muda kwa kutofanya jambo au shughuli sahihi kwa wakati sahihi.
Mfano unakuta mtu anatakiwa asafiri leo kwa ajili ya kufuata bidhaa fulani mahali fulani kwa ajili ya matumizi au biashara zake,lakini anaamua kuahirisha safari bila sababu za msingi na kusema atasafiri kesho yake.
Tukumbuke maisha hayasimami wala hayamngoji mtu huyo. Kesho ikifika unatokea msiba kwa jirani au anapatwa na dharura nyingine mpya hivyo anashindwa kuondoka na hivyo bidhaa aliyokuwa anakusudia kuifuata anashindwa kuipita kwa muda huo na hata akiipata baadaye anakuta kuna mabadiliko mengi yametokea ndani ya muda mfupi hata kupelekea bidhaa hiyo kukosa manufaa aliyotarajia kuyapata.
Matokeo yake mtu huyo anarudi nyuma kimaisha kwa sababu tu alikopa muda.
Kimsingi jamii inatakiwa ielewe kwamba muda ni mali, hivyo kuukopa au kuupoteza bure unaweza kukusababishia kupata hasara kubwa.
Watanzania tujitahiti kutokopa muda na tuzingatie usemi usemao LINALOWEZEKANA LEO LISINGOJE KESHO .
Hii ndio siri ya mafanikio katika maisha.
Je, wewe hujawahi kukopa muda?
