Uchaguzi 2020 Maendeleo ya watu ndiyo Sera inayakubalika sasa. Je, kodi zetu ndio zimejenga barabara, reli na kununua vitu vilivyotuacha hohehahe?

GUSSIE

JF-Expert Member
Dec 2, 2014
3,866
11,100
Wanabodi,

Wananchi hawashibi barabara, ndege, madaraja au hospitali. Wananchi wanahitaji chakula na pesa mwaka huu 2020. Hili chama changu cha CCM ndio tunapaswa kulihubiri kwenye kampeni sasa"Maisha bora na maendeleo ya watu"

Mimi ni mwana CCM. Wakati huu wa kampeni sera ya maendeleo ya vitu inayohuburiwa na CCM imeshafeli kwa wananchi kwa sasa, watu wanahitaji pesa au hela mifukoni tu.

Sasa kila kiongozi wa CCM anajitetea na kujaribu kuunganisha kuwa ndege, barabara na madaraja ni maendeleo ya watu. Hii sio kweli wana CCM wenzangu.

Katika Economics vitu huongelea kwa pande mbili at Micro level (level ya familia au ya mtu mmoja mmoja) na Macro level (level ya kitaifa au mambo makubwa kubwa)

Sasa haya mabarabara na Mandege ni mambo makubwa ya kitaifa ambayo yameshindwa kuleta madhara kwa mtu mmoja mmoja au Familia kama ilivyotarajiwa

Wananchi wao wanahitaji mambo ya haraka haraka tu,Kwa sasa wananchi wengi maisha ni magumu kwao huo ndio uhalisia, Wanahitaji sera za maisha mazuri

Yafuatayo inabidi yafanyike na CCM mapema kuokoa jahazi:
Mosi, Kauli mbiu ya "Tunasonga Mbele Pamoja" inawakumbusha wananchi machungu ya maisha na hasira kuwa maisha yatazidi kuwa magumu zaidi. Hii kauli ibadilishwe mapema, itamkwe "Tunasonga Mbele na Maendeleo ya Watu"

Pili,Tundu lissu asijibiwe tunazidi kuharibu kabisa ,Tundu lissu ni mtu wa tactics anaanzisha jambo dogo mkijibu ndio anashambulia kwa makombora ambayo wananchi yanawakolea na kuwaingia.

Tundu lissu alichokifanya Zanzibar leo kwa kumuunga mkono Malim Seif wa ACT hili ni pigo na mtego kwa CCM. Hapa CCM ikimjibu ataleta mashambulizi wanayopenda wanzazibar kuwa zanzibar ni nchi na mambo ya serikali tatu. Akianza kuyaongelea mambo ya muungano ndio tutachakazwa kwa hoja kama Bunge la katiba na kujikuta tunatafuta hati za Muungano wakati wa JK.

Huu ndio ukweli mchungu hatuna uwezo wa kumjibu Tundu lisu kwa hoja. Tundu lissu Bunge la katiba ilifikia sehemu Waziri lukuvi alisema Tundu Lissu ana kamzizi ka ushawishi na kadawa kanakofanya watu wamsikilize.

CCM sasa muda bado tuanze kuelezea habari za maisha bora kwa wananchi kwa miaka mitano ijayo. Ajira zilizotolewa juzi za ualimu zimezima asilimia 50 ya hoja ya Lissu kuhusu elimu.
 
Hivi Kuna nchi gani hapa duniani watu wameendelea bila kuwa na vitu,

Yaani unakuta hakuna hospitali, hakuna bara bara, hakuna madaraja, hakuna hata usafiri wa ndege lakini wananchi wote Wana PHD na fedha zimejaa kwenye akaunti zao, nitajie.
 
Hivi Kuna nchi gani hapa duniani watu wameendelea bila kuwa na vitu,

Yaani unakuta hakuna hospitali, hakuna bara bara, hakuna madaraja, hakuna hata usafiri wa ndege lakini wananchi wote Wana PHD na fedha zimejaa kwenye akaunti zao, nitajie.
The united republic of Idiotness
 
Acha ubinafsi sisi tunapita bali nchi ipo. Kama wewe hutafaidi watafaidi vitukuu vyako. Ukiona miundo mbinu ya marekani imejengwa kwa karibia miaka 250. Hivyo JPM hakuangilii wewe na mimi lakini anatengeneza legacy ya regime yake. Miundo mbinu anayojenga itaishi over 100 years so for now fight for your needs
 
Hivi Kuna nchi gani hapa duniani watu wameendelea bila kuwa na vitu,

Yaani unakuta hakuna hospitali, hakuna bara bara, hakuna madaraja, hakuna hata usafiri wa ndege lakini wananchi wote Wana PHD na fedha zimejaa kwenye akaunti zao, nitajie.

Waganga njaa hawa, hawajui miundo mbinu ya USA imejengwa kwa miaka karibia 250. Wanajiangalia wao sababu wanakufa kumbe dunia ipo tu miaka 500 na zaidi. Waache ubinafsi tusipofaidi sisi watafaidi vitukuu vyetu
 
GUSSIE naona umeshakubali yaishe. Miaka mitano yote umepotexa muda wako maana ulimtetea sana humu.mpaka mishipa ikakuvimba.

Ole wake agussie majibu ya muungano hoja za Lissu.

Lissu yuko well informed kuliko mtu yeyote kwenye hayo makatiba ma mamiungano ya kikoloni. Akina Mwakyembe, Chenge na akina Mama Makinda bado hawajasahau mtiti wa bunge la katiba. Marehem Sita huko aliko hajasahau hoja za Lissu.

Ilifika mahali wakawa wanashangaa Lissu ana documments ambazo hata wao hawana na hawajawahi kuzisikia popote.
 
Waganga njaa hawa, hawajui miundo mbinu ya USA imejengwa kwa miaka karibia 250. Wanajiangalia wao sababu wanakufa kumbe dunia ipo tu miaka 500 na zaidi. Waache ubinafsi tusipofaidi sisi watafaidi vitukuu vyetu
USA wamejenga kwa miaka 250 nyie mnataka mjenge kwa miaka mitano huku mnapigamo na 10% za kumwaga. Msitufanye wajinga sisi.
 
Sasa wewe unatarajia kuna serikali itakuja kukulisha na kukujengea nyumba?
Acha ukike kwa kuwa na fikra za kupewa pewa, hata wa Dada siku hizi wenye kujielewa hawasubiri kuletewa.

Hata biblia imesema gonga mlango, utafunguliwa, maana tafuta utapata. Wewe unajilalia nyumbani unategemea kitakuja??

Barabara imewekwa ili uweze kutoka nyumbani kwako ukatafute.
 
GUSSIE naona umeshakubali yaishe. Miaka mitano yote umepotexa muda wako maana ulimtetea sana humu.mpaka mishipa ikakuvimba.

Ole wake agussie majibu ya muungano hoja za Lissu....
Kwa hiyo atashinda kwa kura za ZNZ wasiofurahi muungano huu?? U must be joking
 
Hivi Kuna nchi gani hapa duniani watu wameendelea bila kuwa na vitu,

Yaani unakuta hakuna hospitali, hakuna bara bara, hakuna madaraja, hakuna hata usafiri wa ndege lakini wananchi wote Wana PHD na fedha zimejaa kwenye akaunti zao, nitajie.


Elewa:-

Tatizo siyo ndege na viwanja vya ndege,

Tatizo NI utaratibu wa ununuzi wa hizo ndege una viashiria vya RUSHWA na ujenzi wa ndege CHATO una viashiria vya RUSHWA na UBINAFSI.
 
Back
Top Bottom