Maendeleo ya CHADEMA Njombe

....kwanza nimefurahi sana kwa harakati hizo ambazo mpenda maendeleo yeyote yule lazima akubali jitihada mnazofanya kuwa zina maana kwa taifa hili! Nilisikitika sana sana eti kuona Mh.Mkinda na Deo Filikunjombe wanapita bila kupingwa? wapi Demokrasia mkoa wa Njombe? Yes, wananchi wetu Njombe wanahitaji elimu ya kutosha juu ya Demokrasia ya kweli!

Juu ya ombi lako, hapo niliopohighlight, je, unahitaji contact za mtu YEYOTE yule? hata akiwa ni adui yenu? au unataka contact za mwanaharakati wa maeneo hayo? Kuna vijana hapa kama Fidel & Teamo wanaweza saidia sana hapa....!
Sio contacts za mtu yeyote kwa sababu tunazo hata za wanaCCM wa huko. Tunataka za watu ambao ni committed kwa mabadiliko. Tutashukuru ukitusaidia za wanaharakati wa Ludewa kwa sababu za Makete zimeanza kuingia japo bado tunazihitaji zaidi. Asante sana Mkuu
 
Wakuu tunashukuru kwa kutuunga mkono. Tunaomba muendelee kutusaidia kuwapata watu wa Ludewa hata makete milango bado iko wazi
 
Gerrard,
Mko juu kaka. Natamani ningelikuwepo huko kuwasaidia bahati mbaya niko nje ya nchi hii.
Nitarudi karibuni nami niwashe moto huko kwetu ingawa Chadema kwetu huko wako juu sana, natamani bendera zote za kijani zing'olewe kila mahali. Na hili linawezekana. Mafisadi wanaelekea mwisho wao. Msisahau kuwapatia nakala za Katiba wasije kuogopeshwa. Wasome na waone jinsi viongozi wetu wanavyoisigina katiba. Ni udikiteta tupu.
 
Saaafi. Nice move hadi public ijue kuwa JF ni jukwaa la kujadili maendeleo ya Chadema.
 
Kwa niaba ya M/kiti wa CDM Wilaya ya Njombe (mkoa mpya wa Njombe) napenda kuwafahamisha wapenda mabadiliko wote hasa wapenzi, wanachama, mashabiki wa CDM na wananchi kwa ujumla kwamba tunaendelea vizuri na kazi ya kusambaza moto wa mabadliko kama yalivyoasisiwa na Mh Thomas Nyimbo.
Wale wenye kumbukumbu mtakumbuka kuna siku nilileta hapa mada inayoeleza jinsi Mh. Nyimbo alivyojitolea kwa hali na mali kuwasha moto wa mabadiliko. Kwa hakika tumefanikiwa sana kwa ngazi ya jimbo la Njombe Magharibi na sasa tumeunganisha juhudi na Majimbo mengine ya Njombe kusin na Kaskazini. Kuanzia mwezi wa pili (Februari) tunatarajia kuwasha moto kuelekea LUDEWA na MAKETE kwa msaada mkubwa wa Mh. Nyimbo ili hatimaye mkoa wa Njombe uwe na nguvu kama ile ya Mwanza, Mbeya, Iringa, Arusha na Kilimanjaro.
OMBI MAALUM
Kama yupo mwanaJF anaweza kutusaidia contacts za mtu yeyote wa Makete na Ludewa tunaomba tafadhali sana atusaidie kabla ya Jumapili ya wiki hii ili tuwasiliane naye mapema iwezekanavyo. Tumefikia hatua hii baada ya jitihada zetu kuelekea kukwama. Tafadhali kama unayo namba ya mtu au watu au wewe mwenyewe tujulishe kupitia 0789149165 (M/Kiti CDM Njombe (W) au mgosa81@yahoo.com.
Tunawashukuru sana kwa support yenu

Hakuna kulala.........
Posted by Kiongozi

Kuhusiana na uimarishaji wa chama cha CHADEMA, nilikwishafanya mawasiliano na viongozi wa kitaifa juu ya nia yangu kushirikiana na watu wote wenye mapenzi mema kwa wilaya ya Ludewa, ambao wanahitaji sana mabadiliko lakini wamekosa uongozi thabiti. Strategy ya mwanzo imekuwa kufungua ofisi za Chama katika kila kata, mengine tutaongea zaidi tutakapowasiliana kwa njia za simu na vikao. Mimi binafsi nitafurahi sana kuunganisha nguvu zetu kwa pamoja ili kukamilisha lengo hili.

Sasa hivi nipo nje ya nchi lakini mara nikirejea katikati ya Februari, tutawasiliana. Nipo nanyi kwa hali zote. Tusiwe walalmishi bali watendaji, lazima tufanye kitu sasa kwaajili ya faida ya vizazi vijavyo. Taifa letu limekuwa la aibu kubwa kwa umaskini, siyo kwa sababu linahitaji kuwa hivyo bali kwa vile tumekosa uongozi, dhamira na mipango iliyo thabiti.

Nashauri kwa watu wote wanaouchukia umaskini, wanaochukia dhuluma, na wanaopenda wao wenyewe na watoto wasije kuishi kama tunavyoishi sisi leo, kila mmoja kuona atachangia namna gani kuleta mabadiliko, hasa katika majimbo yale ambayo CHADEMA imekosa wabunge na madiwani. Nia iwe ni kuwafikia wananchi wote wa Tanzania kabla ya uchaguzi wa serikali za mitaa.
 
Kwa niaba ya M/kiti wa CDM Wilaya ya Njombe (mkoa mpya wa Njombe) napenda kuwafahamisha wapenda mabadiliko wote hasa wapenzi, wanachama, mashabiki wa CDM na wananchi kwa ujumla kwamba tunaendelea vizuri na kazi ya kusambaza moto wa mabadliko kama yalivyoasisiwa na Mh Thomas Nyimbo.
Wale wenye kumbukumbu mtakumbuka kuna siku nilileta hapa mada inayoeleza jinsi Mh. Nyimbo alivyojitolea kwa hali na mali kuwasha moto wa mabadiliko. Kwa hakika tumefanikiwa sana kwa ngazi ya jimbo la Njombe Magharibi na sasa tumeunganisha juhudi na Majimbo mengine ya Njombe kusin na Kaskazini. Kuanzia mwezi wa pili (Februari) tunatarajia kuwasha moto kuelekea LUDEWA na MAKETE kwa msaada mkubwa wa Mh. Nyimbo ili hatimaye mkoa wa Njombe uwe na nguvu kama ile ya Mwanza, Mbeya, Iringa, Arusha na Kilimanjaro.
OMBI MAALUM
Kama yupo mwanaJF anaweza kutusaidia contacts za mtu yeyote wa Makete na Ludewa tunaomba tafadhali sana atusaidie kabla ya Jumapili ya wiki hii ili tuwasiliane naye mapema iwezekanavyo. Tumefikia hatua hii baada ya jitihada zetu kuelekea kukwama. Tafadhali kama unayo namba ya mtu au watu au wewe mwenyewe tujulishe kupitia 0789149165 (M/Kiti CDM Njombe (W) au mgosa81@yahoo.com.
Tunawashukuru sana kwa support yenu

Hakuna kulala.........
Posted by Kiongozi

Laiti ningekuwa huko nyumbani ningewasha moto wilaya yote ya Kilosa ili wakwetu waamke maana bado wapo wanaodhani kuvaa mabiramu (mabango) ya Nambari wani ni ujiko!
 
Hongera sana tunataka iringa yote iwe kama kilimanjaro soon, mimi naanzisha harakati jimbo la kilolo prof msolla kwaheli,vijana wachukue nafasi.
 
Cdm iangalie uwezekano wa kuwa na mwakilishi kwa kuanzia kila kata ya tanzania hii. Vijana wanaoishi mijini wa kila kata hapa nchini waangalie uwezekano wa kuchangia chama katika kata husika ,tuwe na kijana mwenye elimu ya kati asiye mwoga atusaidie kueneza chama. Mimi niko tayari kuanza na kata ya bomalangombe kilolo iringa mwezi wa tatu, makao makuu iangalie uwezekano wa suala hili bila kujali sehemu gani kwenye washabiki ,ni kata zote nchi nzima tunataka kwanza tupape wawakilishi wa kata kwa nchi nzima baadae wawakilishi katika kila kijiji. Ukombozi wa taifa hili umewadia.
 
Kazi nzuri sana, hasa kama inaanza wakati huu.....4 years to come mtakuwa mbali sana!
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom